Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, ameibana serikali kuhusiana na suala la ajira kwa vijana wanaojitolea katika taasisi mbalimbali za umma. Akizungumza bungeni, leo Oktoba 29, 2024 Dkt. Tulia alisisitiza kuwa vijana hawa wanatoa mchango mkubwa kwa nchi, hivyo ni muhimu kwa serikali kuzingatia maslahi yao na kuhakikisha wanapata fursa za ajira rasmi.