Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi

hilo Kabisa kabisa Kabisa
 
Nadhani NEC ilipitisha hao 19 wawe wabunge baada ya kujilidhisha na uteuzi wao ukiwa na sahihi zote za wahusika. Siyo maamzi ya mtu binafsi bali ni maamzi ya taasisi. Haiwezekan taasisi makini kama NEC nihitaji waraka wa Chadema then niletewe wa Mbowe tu eti niukubali.😁
 
Mkuu samahani mm sijawahi kuanzisha thread hata siku moja kazi yangu huwa ni kuchangia pekee
 
Ukijadili hili jambo kwa akili nzuri, bila ujinga na ushabiki wa kipuuzi, utaelekeza mawazo yako kwenye eneo moja zaidi;
"Mahabusu kutolewa usiku ili kuapishwa kuwa mbunge kesho yake"
Hayo mengine yote yatapata uelekeo hapo.
Mijadala mingine ni hekaya kama za abunuwasi.
 
Kesi iliyopo mahakamani si ya kisiasa but waliofungua kesi wanaona wamenyimwa HAKI yao, mahakama hazisikilizi kesi za kisiasa
 
Mkuu pasco hoja zinajibiwa kwa hoja. Nimeshangaa umetangulizi suala la mahaba ya wasiokubaliana nawe kwa Chadema! huo ni ufinyu au uhaba wa hoja. Hakuna uchama hapa na wengine hatujui hivyo vyama, lakini tukae kimya kama mazuzu tukinajisiwa akili na akina Tulia

Umeandika mambo mengi na kuficha hoja muhimu kwa bahati mbaya wewe ni mwanasheria tena mwanafunzi wa Tulia Akson PhD na kuna kila sababu ya kuwa na shaka na hilo darasa, sorry!
  1. Hili jambo limeanzishwa na Chadema kususia kutambua matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita, ikasema hailitambui Bunge na haitambui Rais
Hii point ina maana na umuhimu gani? Hoja ni COVID19 wameteuliwaje na nani na kikao gani.
Hata kama wameteuliwa na 'kigogo' , je huo ndio utaratibu wa katiba unayosema inavunjwa?
Kukitokea mgogoro wowote wa Uchaguzi, kwa mtu yoyote kupinga ushindi wa mgombea mahakamani, huyo Mbunge ataendelea kuwa mbunge mpaka mahakama itakapotoa hukumu.
No no! wewe ni mwanasheria you should know this better. Mgogoro ukitokea kuna scenario hizi
1. Mhusika anaweza kuamua kutokwenda mahakamani akapoteza ubunge.( Sophia Simba, Zitto)
2.Mhusina anaweza kwenda mahakamani shauri lake lisikizwe akiwa nje ya Bunge
3. Mhusika anaweza kwenda mahakamani kutaka zuio la kuondolewa hadi kesi yake itakapokwisha

Si kweli unachosema sana ni uongo!. Wanachama wa CUF walipoteza Ubunge mara moja
Tundu Lissu kesi yake haijaisha na si mbunge kuna ''replacement'' tayari

Sheria za Bunge ni zipi? Za Ndugai au za Tulia Akson PhD!

Lakini pia unajichanganya, tambua kwamba kubaki na ubunge ni amri ya mahakama
Kumbuka hii hoja halafu utaona tatizo hapa chini

Uongo uongo uongo! mkubwa. Mnadhalilisha taaluma ya sheria wewe na mwalimu wako Tulia Akson PhD.

Huwezi kwenda Bungeni na kusema umechaguliwa na NEC na Bunge likakuruhusu kuingia kwasababu umelitaarifu kwa barua . Huo si utaratibu lazima uwe na nyaraka za NEC na vitambulisho vingine.

Huwezi kumwandikia barua Spika eti unakwenda mahakamani na Spika huyo akakubali, huu niu upuuzi mkubwa. Spika anafanyia kazi taarifa za kiofisi si vijibarua visivyo na ushahidi

Spika Tulia Akson PhD alipaswa kuomba apewe barua ya mahakama kwamba lipo shauri, siyo barua za ''mapenzi' tu kutoka COVID.

Hili halihitaji kujua sheria linahitaji weledi tu na nakuhakikishia watu wanaojua wanamuona Tulia Akson PhD mtu wa ajabu sana! hakuna kitu pale , empty !
  1. Hivi ndivyo ilivyofanyika kwa Hamad Rashid Mohammed, David Kafulila na Zitto Kabwe. Na baada ya uamuzi wa mahakama, walivuliwa ubunge, Zitto alijivua na kuaga rasmi Bunge.
Nimekupa scenario pale juu, pia utambue suala la Tundu Lissu lipo mahakamani kavuliwa ubunge. Hivi huoni double standard na kwa PhD holder hili halikupawa kufanywa kizembe namna ile. Professor ? real .
Rejea hapo juu! nilipokueleza kuwa T.Akson PhD anafanyia kazi taarifa rasmi na ndicho walichosema wakati Chadema walipodai kupeleka barua.

Job Ndugai alisema hawezi kufanyia taarifa za kusikia anataka taarifa ya chama.
Akaonyeshwa dispatch book na kunywea hadi alipovurunda siku hizi anazungumza vichochoroni

Mwambie Mwalimu wako Tulia Akson PhD kwamba anachokifanya ni majungu.

Taarifa ya kwenda mahakamani inathibitishwa na nyaraka za mahakama siyo hadithi.

P huwezi kwenda na kudai CCM wamekteua kuwa Mbunge na eti T. Akson PhD akakubali tu kwasababu anakujua ni mwanafunzi wake na unaandika makala magazeti! hell no! that is stupid
Kazi za umma zinafanywa kwa taratibu na nyaraka, alipaswa kuwaambi wampe barua ya mahakama

Hivi Chadema wangeandika barua in advance ya kumwambia wanachama wamefukuza leo hapa pangekalika! Please usitetee upuuzi wa kuvunja sheria za nchi. Tulia anavurunda tu! shame on her! Hivi mtu na PhD anadhalilikaje kirahisi namna hii! kibaya zaidi huyu anatoa maamuzi yanayoathiri watu milioni 55!

Pasco please
Chadema walijua mchezo wa Serikali, Bunge na Mahakama. Kutafuta nani amefanya forgery ingechukua miaka 10. Hawa si ndio wanamsubiri dereva wa Tundu Lissu?

Polisi wana intelejensia ya kubaini uhalifu tuhuma za Chadema zilitosha zinatoka katika taasisi. Hilo linawezekana huko kwenye Polisi wa kweli, hapa kwetu ni kichekesho tu

Kwa taarifa yako kesi ya COVID19 itaisha 2025 December.

Mahakama imepokea maagizo ya mhimili wa Tulia Akson PhD na ukumbuke mahakama inaongozwa na Mwalimu wako CJ ibrahimu aliyesema '' mahakama ziangalie mihimili mingine inasema nini'' jana tumeona kauli yake Mhimili wa Bunge umesema wa mahakama umetekeleza

Hoja usiyojibu, mawakili wa serikali wanamwakilisha nani?
Kesi ni ya wanachama na chama chao, hao mawakili ni kwa ajili ya nani

Ni hitimishe kwa kukuambia Pascal hoja zinajibiwa kwa hoja, unachoeleza kwa maelezo mengi ni kutaka kupoteza wasomaji. Tulia Akson PhD na Professor hakufuata au hajui taratibu za ofisi

Inasikitisha Spika wa Bunge anafanyia kazi taarifa za majungu na si za kiofosi.

Spika alikuwa na barua ya CDM ya kiofisi si vikaratasi vya COVID. Barua ya mahakama ni ya kiofisi

Suala zima limemuonyesha Tulia, Tuna tatizo nchini, huyu anaongoza mhimili wa kutunga sheria! eee mola! ee mungu inusuru nchi hii.




 
Pole sana,
Kwa kufuata maelekezo kutoka mamlaka ya uteuzi watz na hata TAASISI zao wamekuwa wanafanya vioja. Lakini maadam kesi iko mahakamani tutafika patamu kama ilivyokuwa kwenye kesi ya ugaidi.
Alieutengeneza huo waraka atajulikana mchana kweupe. Na hii itaimarisha mahitaji na madai ya Katiba Mpya badala ya hii mbofumbofu iliyopo.
 
SAFI KABISA
 
Uhusiano wako na Pascal Mayalla ninawaachia wenyewe mtajuana, ila napenda kutoa comment sehemu uliyoandika kuhusu Lissu.

Ninavyoelewa ni kuwa Lissu alikwenda mahakamani baada ya kuwa ameshafukuzwa ubunge. Hawa wanawake wamekwenda mahakamani kabla CHADEMA haijafikisha kwa Spika taarifa ya kufukuzwa kwao uanachama, hivyo status quo inatumika. It works both ways, iwapo Spika angepokea taarifa ya kufukuzwa kwao uanachama na akawafuta ubunge lakini wao kesho yake wakaja kulalamika kuwa wamekata rufaa, status quo itatumika tena kwa maana ya kuwa wataendelea kuwa nje ya bunge hadi rufaa yao itakapotolewa hukumu.

Issue kubwa hapa ni timing, kwa sababu jambo likishafika mahakamani basi status quo ina kick-in. Nakumbuka kuwa Zitto naye alikwenda mahakamani, kuzuia kufutwa kwake uanachama na hivyo akaendelea kuwa mbunge hadi taratibu za kimahakama zilipokamilika.
 
Nilicho muelewa bwana Pascal Mayalla hayupo kujadili goli ni halali ama si halali,bali anataka kujadili build up ya goli,yaani kabla ya goli la speaker je movement nzima ya goli imeanzia wapi?!!

Na kingine nilichojifunza CCM wanatumia sana madhaifu ya CHADEMA kuwaburuza...mh.spika nahisi kaisha jua wapi palivuja hivyo anachokonoa[emoji23][emoji23] mpaka pajulikane wazi wazi...

Natamani nijue ombi(request) la jamaa wa juisi ya ikulu kwa mama katika hili.
Nahisi kabisa hili liligusiwa na namna gani walicheze.
 
Kama hili linajulikana ni kipi kinachowazuia kuchukua hatua juu ya mwenyekiti?

Kwa kumbukumbu zangu jamaa si mara ya kwanza anachoma dawa ya mbu disko.
 
Project yenu ya kuiua cdm bado inalipa??
 
Mhuni hapo ni CHADEMA au Mbowe? CDM kama taasisi wako sahihi kabisa, kama Akina Mdee na Mbowe walifanya makubaliano ya kihuni huko vichochoroni hili ni lao wamalizane wenyewe. Lakini chama kama chama lazima kisimame.

Mkuu faateni tu utaratibu vinginevyo mtakaa mahakamani sana na Halima Mdee na wenzake hamtaweza watimua
 
Muulize pasco mwanasheria uchwara kipi kimetangulia na kilimfikia spika mapema Kati ya

1).barua ya chama ya maamuzi ya kuwavua uanachama

2)taarifa ya kuazimia kufungua kesi mahakamaniya akina mdee

3) uamuzi wa mahakama. Kulinda ubunge na siyo uanachama

Sasa Pasco huyo spika anawezaje kufanya kazi taarifa ya mwisho ambayo imekuja kwa kuchelewa? Na imetangiliwa na taarifa rasimi ya mkutano
 
Dogo mabo ya ki ccm ya kumwabudu mtu unalinganisha na taasisi imara kama chadema.

Kama mwenyekiti alikuwa na mmaamuzi yake nje ya vikao rasimi vya chama shauuri yake, ndo mjue chadema ni taasisi imara na ipongezwe kwa kusimamia haki na maadili bila ya kujali msimamo wa wenyekiti

Dogo ningekuona una akili kama ungewapongeza cdm kwa kusimamia maadili na kumpuuza mwenyekiti na vikao vyake vya Siri, kitu ambacho huwezi ona ndani ya ccm
 
Hapa ndipo pamenifanya kubaini kuwa kila ulichoandika ni porojo tu, chama gani kinachojijenga kwa sasa zaidi ya CHADEMA mpaka kinakuwa gumzo at whatever they do.
[emoji116]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…