Mkuu pasco hoja zinajibiwa kwa hoja. Nimeshangaa umetangulizi suala la mahaba ya wasiokubaliana nawe kwa Chadema! huo ni ufinyu au uhaba wa hoja. Hakuna uchama hapa na wengine hatujui hivyo vyama, lakini tukae kimya kama mazuzu tukinajisiwa akili na akina Tulia
Umeandika mambo mengi na kuficha hoja muhimu kwa bahati mbaya wewe ni mwanasheria tena mwanafunzi wa Tulia Akson PhD na kuna kila sababu ya kuwa na shaka na hilo darasa, sorry!
- Hili jambo limeanzishwa na Chadema kususia kutambua matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita, ikasema hailitambui Bunge na haitambui Rais
Hii point ina maana na umuhimu gani? Hoja ni COVID19 wameteuliwaje na nani na kikao gani.
Hata kama wameteuliwa na 'kigogo' , je huo ndio utaratibu wa katiba unayosema inavunjwa?
Kukitokea mgogoro wowote wa Uchaguzi, kwa mtu yoyote kupinga ushindi wa mgombea mahakamani, huyo Mbunge ataendelea kuwa mbunge mpaka mahakama itakapotoa hukumu.
No no! wewe ni mwanasheria you should know this better. Mgogoro ukitokea kuna scenario hizi
1. Mhusika anaweza kuamua kutokwenda mahakamani akapoteza ubunge.( Sophia Simba, Zitto)
2.Mhusina anaweza kwenda mahakamani shauri lake lisikizwe akiwa nje ya Bunge
3. Mhusika anaweza kwenda mahakamani kutaka zuio la kuondolewa hadi kesi yake itakapokwisha
Si kweli unachosema sana ni uongo!. Wanachama wa CUF walipoteza Ubunge mara moja
Tundu Lissu kesi yake haijaisha na si mbunge kuna ''replacement'' tayari
Sheria za Bunge ni zipi? Za Ndugai au za Tulia Akson PhD!
Lakini pia unajichanganya, tambua kwamba kubaki na ubunge ni amri ya mahakama
Kumbuka hii hoja halafu utaona tatizo hapa chini
- Na kukitokea mgogoro wa kichama, mbunge yoyote kufutwa uanachama na chama chake, anapaswa kupoteza ubunge wake automatically ila akiliarifu Bunge kuwa amepinga mahakamani kuvuliwa kwake uanachama, Bunge litamkingia kifua kusubiria aumuzi wa mahakama.
Uongo uongo uongo! mkubwa. Mnadhalilisha taaluma ya sheria wewe na mwalimu wako Tulia Akson PhD.
Huwezi kwenda Bungeni na kusema umechaguliwa na NEC na Bunge likakuruhusu kuingia kwasababu umelitaarifu kwa barua . Huo si utaratibu lazima uwe na nyaraka za NEC na vitambulisho vingine.
Huwezi kumwandikia barua Spika eti unakwenda mahakamani na Spika huyo akakubali, huu niu upuuzi mkubwa. Spika anafanyia kazi taarifa za kiofisi si vijibarua visivyo na ushahidi
Spika Tulia Akson PhD alipaswa kuomba apewe barua ya mahakama kwamba lipo shauri, siyo barua za ''mapenzi' tu kutoka COVID.
Hili halihitaji kujua sheria linahitaji weledi tu na nakuhakikishia watu wanaojua wanamuona Tulia Akson PhD mtu wa ajabu sana! hakuna kitu pale , empty !
- Hivi ndivyo ilivyofanyika kwa Hamad Rashid Mohammed, David Kafulila na Zitto Kabwe. Na baada ya uamuzi wa mahakama, walivuliwa ubunge, Zitto alijivua na kuaga rasmi Bunge.
Nimekupa scenario pale juu, pia utambue suala la Tundu Lissu lipo mahakamani kavuliwa ubunge. Hivi huoni double standard na kwa PhD holder hili halikupawa kufanywa kizembe namna ile. Professor ? real .
- Hivyo jana asubuhi kupitia Bunge live, Spika alizungumza huku nikimuona kwa macho yangu na kumsikia kwa masikio yangu, alitangulia kupokea taarifa ya kina Mdee kufungua kesi mahakamani kupinga kuvuliwa uanachama, kwa kutaja siku, saa na dakika, kabla ya kupokea taarifa rasmi ya Chadema kuwafuta uanachama. Hivyo Spika Tulia yuko right na Bunge liko right kuwakingia kifua.
Rejea hapo juu! nilipokueleza kuwa T.Akson PhD anafanyia kazi taarifa rasmi na ndicho walichosema wakati Chadema walipodai kupeleka barua.
Job Ndugai alisema hawezi kufanyia taarifa za kusikia anataka taarifa ya chama.
Akaonyeshwa dispatch book na kunywea hadi alipovurunda siku hizi anazungumza vichochoroni
Mwambie Mwalimu wako Tulia Akson PhD kwamba anachokifanya ni majungu.
Taarifa ya kwenda mahakamani inathibitishwa na nyaraka za mahakama siyo hadithi.
P huwezi kwenda na kudai CCM wamekteua kuwa Mbunge na eti T. Akson PhD akakubali tu kwasababu anakujua ni mwanafunzi wake na unaandika makala magazeti! hell no! that is stupid
Kazi za umma zinafanywa kwa taratibu na nyaraka, alipaswa kuwaambi wampe barua ya mahakama
Hivi Chadema wangeandika barua in advance ya kumwambia wanachama wamefukuza leo hapa pangekalika! Please usitetee upuuzi wa kuvunja sheria za nchi. Tulia anavurunda tu! shame on her! Hivi mtu na PhD anadhalilikaje kirahisi namna hii! kibaya zaidi huyu anatoa maamuzi yanayoathiri watu milioni 55!
Pasco please
- Hii due process ingebainisha kuna forgery, forgery ni jinai, walipaswa kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai ufanyike na hiyo barua yao ya utambulisho, iwe authenticated na ingebainika ni forgery, wala sio Bunge bali ni NEC ndio wangetengua zile barua zao za uteuzi na wangevuliwa ubunge.
Chadema walijua mchezo wa Serikali, Bunge na Mahakama. Kutafuta nani amefanya forgery ingechukua miaka 10. Hawa si ndio wanamsubiri dereva wa Tundu Lissu?
Polisi wana intelejensia ya kubaini uhalifu tuhuma za Chadema zilitosha zinatoka katika taasisi. Hilo linawezekana huko kwenye Polisi wa kweli, hapa kwetu ni kichekesho tu
Kwa taarifa yako kesi ya COVID19 itaisha 2025 December.
Mahakama imepokea maagizo ya mhimili wa Tulia Akson PhD na ukumbuke mahakama inaongozwa na Mwalimu wako CJ ibrahimu aliyesema '' mahakama ziangalie mihimili mingine inasema nini'' jana tumeona kauli yake Mhimili wa Bunge umesema wa mahakama umetekeleza
Hoja usiyojibu, mawakili wa serikali wanamwakilisha nani?
Kesi ni ya wanachama na chama chao, hao mawakili ni kwa ajili ya nani
Ni hitimishe kwa kukuambia Pascal hoja zinajibiwa kwa hoja, unachoeleza kwa maelezo mengi ni kutaka kupoteza wasomaji. Tulia Akson PhD na Professor hakufuata au hajui taratibu za ofisi
Inasikitisha Spika wa Bunge anafanyia kazi taarifa za majungu na si za kiofosi.
Spika alikuwa na barua ya CDM ya kiofisi si vikaratasi vya COVID. Barua ya mahakama ni ya kiofisi
Suala zima limemuonyesha Tulia, Tuna tatizo nchini, huyu anaongoza mhimili wa kutunga sheria! eee mola! ee mungu inusuru nchi hii.