Spika mstaafu Job Ndugai hana gari na dereva wa Serikali?

Inawezekana kaamua kuendesha mwenyewe. Sio kila kitu ukionacho kwa nje ndo kilivo kwa ndani.
 
Kayataka
 
Bro, unachofanya ni kueneza udaku wa uongo na si sawa kabisa! Kwanza, Spika Ndugai ana haki ya kuishi maisha yake binafsi bila watu kumdhalilisha kwa kumwaga details kama namba za gari.

Dodoma ni mji wake, si ajabu kumwona akiendesha gari lake mwenyewe, si kila kitu lazima kiwe na dreva wa serikali. Siyo kila mtu anataka kuishi maisha ya kiserikali 24/7, na hio unayosema kuhusu 'kutelekezwa' ni kupotosha watu. Kila mtu ana uhuru wake wa kufanya anavyopenda na kuendesha gari lake kama kawaida bila drama. Koma kutafuta kiki na kuchafua jina la watu bila sababu!
 
Uko sahihi kaka
 
Mwache mzee afanye mazoezi Huwa ana utamaduni huo Toka akiwa spika siku Moja Moja kujikumbusha ungekuwa makini Huwa huyupo peke yake kama unavyodhani
 
Naona tuna-comment kwa kukataa na kukubali bila kujiridhisha ukweli wa taarifa iliyobandiwa hapa jukwaani. Mwambieni mleta Mada atuwekee picha au video kama evidence, unless otherwise ni muendelezo wa uzushi, uongo na propaganda za Chadema tu.

Cc Moderator
 
Kwani lazima atumie dereva? Ni hivi vi-nchi vyetu vya kiafrika ndivyo viongozi wanataka ufahari wa kila kitu, nchi zilizoendelea viongozi wengi wanaendesha wenyewe.
 
Bongo bana Kina Bush Junior tu pamoja na Kuwa marais wa taifa kubwa kabisa kama US lakini bado wana drive Pick up zao Za GMC na kwenda nazo mashambani pamoja na kuwa anakuwa na walinzi ila bado ana drive mwenyewe binafsi hata niwe nani kuna mambo siwezi kuyaaacha ikiwemo driving
 
Labda ni uamizi wake mwenyewe
yes hili ndio jibu sahihi. Kila mbunge analipwa fedha za wasaidizi 3,dereva, msaidizi na mhudumu wa ofisi. Ukimuona mbunge yoyote anajiendesha ni anapenda mwenyewe kwa mazoezi.

Speaker mstaafu anapewa gari, dereva na lita 70 za wese kila wiki,hii haimzuii speaker kujiendeshea gari of his choice na kujijazia mafuta. Rais Uhuru Kenyatta akiwa ikulu, siku za weekends on his private missions, anavuta mwenyewe ile SUV yake Range Sport, no bodyguards no ving'ora,no nothing.

One day a traffic lady stopped his SUV,aliporuhusu Uhuru akampungia ,traffic kumuona ni CinC kijasho chembamba,due to shock akaanza ghafla,na yale mavazi meupe ya traffic... you can imagine!.After one week akapokea ujumbe ameitwa Ikulu, akajua she is fired, kumbe it was to be decorated!

p
 
Museven na Kagame ni ma Rais ila kuna wakati huwa wanaendesha magari wenyewe kwahiyo ni vibe tu ya mtu, kwa Ndugai dereva anae ila ni maamuzi yake kuendesha gari mwenyewe na hata kama serekali isingempa dereva bado anao uwezo wa kuajiri dereva.

Hayo ni mambo madogo sana sijui kwanini umelichulia kama jambo kubwa hivyo
 
Nilipokuwa mtoto mdogo nilikuwa siwezi kutofautisha mimea ya uleI na mpunga
 
Ukiona hivyo ujue anataka kwenda kwa mchepuko hivyo hataki shobo ya dereva. Umalaya unamsumbua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…