Spika na wabunge warejea kutoka Misri wataka kocha wa Taifa stars mh Amunike ni dalali atimuliwe mara moja

Spika na wabunge warejea kutoka Misri wataka kocha wa Taifa stars mh Amunike ni dalali atimuliwe mara moja

Wabunge wa ccm bana wanachekesha ile mbaya, baada ya kuona jinsi watu walivyofurahia hiyo timu kufungwa wanatafuta pa kutokea. Ukweli ni kuwa sisi hatuna uwezo wa soka na gundu lilizidi ccm walivyoanza kuweka kimbelembele kwenye hiyo timu. Ni kweli Amunike sio kocha, je ilikuwaje huo upuuzi wanaoongea sasa hawakuongea wakati timu ilipofuzu kwenda Afcon? Sisi tunajua timu iliyofungwa sio ya taifa bali ni ya ccm.
Mkuu mbona wabunge wa chadema wapo wengi yi wameenda?
 
Spika Ndugai pamoja na wabunge wote walioenda Misri kuishangilia Taifa stars wamerejea na kutoa shutuma nzito kwa kocha Amunike.

Juma Nkamia amesema Amunike ni dalali aliyeokotwa jalalani huko Sudan na hana ujuzi wowote wa ukocha.
Nkamia amesema aliongea na Rais wa shirikisho la soka la Nigeria aliyemhakikishia kuwa Amunike siyo kocha na kwamba kama TFF wangeomba ushauri basi wangewakataza kuingia mkataba na kocha Amunike.
Naye mh Bulembo amedai kuwa Amunike si lolote wala chochote na kwamba wabunge wengi walishikwa na tumbo la " kuendesha" kwa namna timu yetu ilivyokuwa inaboronga.

Spika Ndugai amesema wataongeza bajeti ya michezo katika bunge lijallo ili michezo ianze kufundishwa mashuleni.

Source Clouds tv!

Maendeleo hayana vyama!
Vyama havina maendeleo
 
Wa TZ!!! hasa politikishiani, na hasa kutoka chama kubwa you have lost, nyamazeni tu, no comments no whatsoever/ wakati tuanafaulu kuingia AFCON2019 you were there na mlishangilia Amunike na kuitwa timu ikawa ya makada wa lichama likubwa, leo tumepigwa mbili na SENEGAL li timu likubwa mnakuja na manaeno ya kuchefua. GOD FORBID!!, what did you do kuiandaa timu!?!, ni porojo gani mlipiga huko mjengoni angalau kusaodia soak la nchi hii?!?, mmepigania katika bajeti zitengwe TZS ngapi kwa ajili ya soka letu?!?. acheni unafiki kabla ya kuhukumu wengine mjitathmini what have you done?!?. ifikirieni tu hata ligi kuu yetu maana ndio msingi wa kupata timu ya taifa iliyo bora haina mdhamini anayeweza kufoot cost zote what have you done about that?!?. TUACHENI TULIE WENYEWE!! msitukumbushe mbali
 
Spika Ndugai pamoja na wabunge wote walioenda Misri kuishangilia Taifa stars wamerejea na kutoa shutuma nzito kwa kocha Amunike.

Juma Nkamia amesema Amunike ni dalali aliyeokotwa jalalani huko Sudan na hana ujuzi wowote wa ukocha.
Nkamia amesema aliongea na Rais wa shirikisho la soka la Nigeria aliyemhakikishia kuwa Amunike siyo kocha na kwamba kama TFF wangeomba ushauri basi wangewakataza kuingia mkataba na kocha Amunike.
Naye mh Bulembo amedai kuwa Amunike si lolote wala chochote na kwamba wabunge wengi walishikwa na tumbo la " kuendesha" kwa namna timu yetu ilivyokuwa inaboronga.

Spika Ndugai amesema wataongeza bajeti ya michezo katika bunge lijallo ili michezo ianze kufundishwa mashuleni.

Source Clouds tv!

Maendeleo hayana vyama!
Ndugai anafanya nini bungeni? Tanzania tuna Bunge? Mbona hajatimuliwa? he is just a stooge of a president! Afadhali tumefungwa 2, yeye bunge is absolutely stupid so called bunge!
 
Nina imani Taifa stars sasa watapumua na Kenya tutamfunga!
Mliteka timu ya Taifa na kuifanya timu ya chama, Leo mnakuja na bla bla nyingi, porojo za kitoto..? Rudisheni timu ya Taifa kwa Watanzania na mkiri mmepotoka. Acheni tabia ya kujikweza kwa mafanikio msiyochangia na kubinafisisha vitu vya kitaifa kuwa vya chama chenu.
 
Ni kocha mzuri sema ameingia kwenye nchi yenye maneno mengi mpaka atajuta, angekuwa kocha mbaya leo hii msingekuwa Egypt na msingeleta haya maneno kutoka huko. Chanzo ch kuboronga ni maandalizi hafifu,kuna video zilisambaa humu zikionyesha bondia wetu alivyokuwa anafanya mazoezi kwa kutumia matairi ya gari, tukasema serikali nzima ina kosa budget ya kulipia wana michezo wake gym nzuri ili wanamichezo wakajenga miili na stamina, matokeo yake ndo yale walikuwa wakisumwa wanaanguka wenyewe, hawana nguvu, miguu kama inadegedege kocha afanye nini? misingi mibovu ya michezo.

Kosa la kocha ni moja tu kwangu, kupanga watu wenye lishe duni, mabeki wafupi ambao hawakuweza kuhimili wachezaji wa Senegal, naona tutafungwa 10 za Algeria , Tanzania tunatakiwa tuje na mpango kwanza wa kuimarisha afya bora kwa watoto wetu katika ngazi za familia na mashuleni, tuanzishe programme muhimu ya lishe maziwa kuanzia majumbani, na mashuleni, shuleni iwekwe ratiba ya watoto kunywa maziwa kila siku pakiti mbili, baada ya hapo tuhamasishe michezo katika ngazi zote, baada ya hapo tuchague vijana watakao tuwakilisha vyema katika michezo mbalimbali na tuwaandae vizuri. Hatuwei kuwa na vijana legelege tukatarajia matokeo makubwa tunajidanganya, chukueni Africa mashari ,utagundua ni Tz pekee ndio tuna miili hafifu, programme zetu za lishe majumbani na mashuleni ni 0, na maandalizi yetu ya michezo ni F.

Ushauri ni wa bure, kila mtu akapitie Hotuba ya Prof Lipumba juzi katika mkutano wake Diamond jubilee akizindua sera mpya, ameeleza jinsi report za kimataifa zinaonyesha ni jinsi gani ya kuandaa watoto kwa taifa imara lijalo, Tanzania hatuchachelewa.
HII INANIKUMBUSHA UMISETA KATIKA SHULE MOJA HIVI YA SERIKALI MWALIMU AKAMCHEZESHA DOGO MMOJA KIKOSINI BILA KUJUA KUWA ALIKUWA TANGU ASUBUHI HAJALA CHOCHOTE TANGU ALIPOTOKA NYUMBANI ASUBUHI. JAPO DOGO ALIKUWA NA MOYO SANA WA KUJITUMA KUICHEZEA SHULE YAKE NA UKIZINGATIA HATA CHAKULA CHA MCHANA WAZAZI WAMESHINDWA KUMLIPIA SHULENI. ILE SIKU ALIZIMIA UWANJANI AKAENDA KUZINDUKIA HOSPITALINI KESHO YAKE.
 
kipimo kizuri cha Taifa Stars ni mechi yao na Kenya, ndio tutapata picha halisi ya ubora wao, kuwapima na senegal ni kuwaonea tu
 
Tz kila mtu kochaa....
Huyu spika nae ubongo wake unaoza taratibu...
Tusimlaumu
 
Kwa kosa lipi? Kwanza wangetafakari Burundi ni ka nchi kanakozidiwa ukubwa hata na mkoa mmoja tu wa Tz Leo wana timu bora kuliko Tz yenye population Ya watu milioni hamsini!
 
Spika Ndugai pamoja na wabunge wote walioenda Misri kuishangilia Taifa stars wamerejea na kutoa shutuma nzito kwa kocha Amunike.

Juma Nkamia amesema Amunike ni dalali aliyeokotwa jalalani huko Sudan na hana ujuzi wowote wa ukocha.
Nkamia amesema aliongea na Rais wa shirikisho la soka la Nigeria aliyemhakikishia kuwa Amunike siyo kocha na kwamba kama TFF wangeomba ushauri basi wangewakataza kuingia mkataba na kocha Amunike.
Naye mh Bulembo amedai kuwa Amunike si lolote wala chochote na kwamba wabunge wengi walishikwa na tumbo la " kuendesha" kwa namna timu yetu ilivyokuwa inaboronga.

Spika Ndugai amesema wataongeza bajeti ya michezo katika bunge lijallo ili michezo ianze kufundishwa mashuleni.

Source Clouds tv!

Maendeleo hayana vyama!
Ujinga wa kiwango cha juu...wameshakula perdiem wameshiba sasa wanannii! Kwa mtu wmenye akili timamu alitarajia Timu yetu ifanye nini kule Misri ! Kutegemea miujiza katika soka ni kumkosea MUNGU! Mungu ametupa Talanta sisi tumezifukia then unataka uwafunge Snegal!
Kwa maandalizi yapi,Mpira ni kufanya uwekezaji tena wa muda mrefu! Kwa viwango vya Vilabu ndio unaweza kuweka malengo ya miaka 2,na ukaweza kununua wachezaji bora ...kama alichofanya MO kwa Simba .Kinyume cha hapo ni unafiki na uzandiki.
Mimi sina uhakika kama Amunike ni kocha aua la ...ila ninachojua ni kuwa kiwango chetu ni kidogo mno kwa kuwa menejimenti (Kama ilivyo kwa mamabo mengine yote) ya soka ni mbovu.
Hawa Wabunge watulie tu ,,hizo ndio akili zetu
zinawakilishwa na wao!
 
Back
Top Bottom