Spika Ndugai ameitaka Serikali iache kutoa visingizio kuwa malori ya Dangote yanaharibu barabara ya Mtwara

Spika Ndugai ameitaka Serikali iache kutoa visingizio kuwa malori ya Dangote yanaharibu barabara ya Mtwara

Mbona yeye anaikanyaga katiba ya nchi kwa kutokuifuata!
 
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai ameitaka Serikali iache kutoa visingizio ambavyo havina msingi kuwa malori ya kampuni ya Dangote yanaharibu barabara za mikoa ya Lindi na Mtwara.

Amesema kinachotokea ni barabara hizo kujengwa chini ya kiwango, kwani ni jambo linalofahamika kwamba malori hayo yanapimwa uzito, hivyo kampuni ya Dangote haistahili lawama.

Kabla ya kauli hiyo ya Spika, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Sera na Watu Wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama alisema Serikali itapitia upya ujenzi wa barabara hizo ambazo zimekuwa zikiigharimu fedha nyingi.

Awali wabunge wa kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara walilalamikia jinsi Serikali inavyotumia fedha nyingi katika kuikarabati wa barabara hiyo ukarabati ambao hauna tija kwa kuwa imekuwa ikiharibika.

ITV
Imekuwa kila leo Spika anaikosoa Serikali. Mara Serikali ipitie upya mkataba wa bandari ya Bagamoyo. Mara Serikali, kupitia TRA, itoze kodi namna fulani. Na sasa Serikali isitoe visingizio kuhusu ubora wa barabara inazozijenga. Kuna Bunge, Mahakama, na Serikali. Kila mojawapo ya mihimili hiyo ina majukumu yake. Kazi ya Bunge ni kutunga sheria tu. Baada ya hapo sheria hizo zinatafsiriwa na Mahakama; na baadaye Serikali inatekeleza yaliyoamuliwa na Mahakama. Spika anayo majukumu ya kutosha kuyafanyia kazi. Kudodosa yanayojiri siku kwa siku Serikalini ni kuingilia muhimili mwingine. Sanasana aweke hoja ya kutunga sheria fulani na kama Bunge litaipitisha Serikali italazimika kulitekeleza suala hilo. Hizo kauli anazozisema sasa hivi Serikali inaweza kuzipuuza tu na hakuna atakachoifanya.
 
Dangote anaambiwa malori yake yanaharibu barabara, kama ni kupima uzito mizani hakuna lori lisilopima uzito, tatizo ni huko kwa hao wapimaji wanaona malori ya Dangote ndio yanafaa "kupiga"
Sasa yanaharibu vipi kama sio kwa kuzidisha uzito? kama wanazidisha uzito ndio maana wana ambiwa hivyo.maana yake wao ndio wanaongoza kuzidisha uzito na kuharibu barabara
 
Ndungai amezaliwa upya
Huyu anatapatapa tu hana lolote. Kaona Mama SASHA hana time nae wala haangaiki nae kama ilivyokuwa enzi za mwendazake. Wakati huo alikuwa akimwagiwa sifa kem kem namna alivyokuwa akiwasakama Wapinzani.

Sasa Mama kaingia hana habari nae utafikiri hayuko. Kwamaana hiyo ataacha kweli kupiga piga kelele Mama atambue uwepo wake??

Pili anajaribu kujijenga mwenyewe baada ya kuona mshika mbeleko keshaenda zake. Hili nalo halitamsaidia kwani alishaoza. Anajaribu kujipulizia manukato.
 
Sasa yanaharibu vipi kama sio kwa kuzidisha uzito? kama wanazidisha uzito ndio maana wana ambiwa hivyo.maana yake wao ndio wanaongoza kuzidisha uzito na kuharibu barabara
Faini hazijasaidia?
 
Barabarani ya Tanzam iko busy na loaded kuliko hiyo mbona hatusikii visingizio vya kuharibiwa na malori?

Hizo zilijengwa chini ya kiwango
 
Kwahio Sababu yanapimwa ndio ina maana hayawezi kuzidisha uzito ?, Je kama yanajazwa over-capacity ? (Au kwenye malori na barabara hakuna uwezekano wa overcapacity)?
 
Kuna kipande hiyo barabara ilianza kubonyea kabla hata haijafikisha mwaka mmoja, hovyo sana mafisadi......
 
Ndugai wa 2020 akikutana na ndugai wa 2021 watapigana sana
 
Ndugai kafufuka [emoji23][emoji23][emoji23]
E2crFWzWQAQ3bBp.jpg
 
Michango kutoka upinzani imekosekana anaona sasa aongoze mashambulizi kuikosoa serikali bunge limekuwa mzigo wa chama kimoja,wapo wanasinzia tu.
 
Ngudai bana utafikiri sio yeye CCM kwa unafiki hawajdmbo , naona na mkewe alikuwa mkurugenzi wa Bahi , pamoja na kupata hati chafu ya CAG mama kampandisha cheo kuwa RAS kufa kufaana , chupa mpya mvinyo uleule kijani kibichi .
 
Imekuwa kila leo Spika anaikosoa Serikali. Mara Serikali ipitie upya mkataba wa bandari ya Bagamoyo. Mara Serikali, kupitia TRA, itoze kodi namna fulani. Na sasa Serikali isitoe visingizio kuhusu ubora wa barabara inazozijenga. Kuna Bunge, Mahakama, na Serikali. Kila mojawapo ya mihimili hiyo ina majukumu yake. Kazi ya Bunge ni kutunga sheria tu. Baada ya hapo sheria hizo zinatafsiriwa na Mahakama; na baadaye Serikali inatekeleza yaliyoamuliwa na Mahakama. Spika anayo majukumu ya kutosha kuyafanyia kazi. Kudodosa yanayojiri siku kwa siku Serikalini ni kuingilia muhimili mwingine. Sanasana aweke hoja ya kutunga sheria fulani na kama Bunge litaipitisha Serikali italazimika kulitekeleza suala hilo. Hizo kauli anazozisema sasa hivi Serikali inaweza kuzipuuza tu na hakuna atakachoifanya.
Utakua ulisoma civics ya nchini Burundi au msumbiji
 
Back
Top Bottom