Spika Ndugai: Baadhi ya wabunge wataondoka mikono mitupu kwa sababu wanaelemewa na madeni sugu

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Spika wa bunge mh Job Ndugai amesema wabunge wengi wanaelemewa na madeni na kuna uwezekano mkubwa baadhi yao wakaondoka mikono mitupu baada ya bunge kuvunjwa rasmi mwishoni mwa mwezi June.

Kwa kawaida wabunge hulipwa kiinua mgongo kila baada ya miaka mitano ya kuwatumikia wananchi.

Source Tanzania Daima.

Maendeleo hayana vyama!
 
Taifa la wajinga na matakataka imatuhusu nn sisi kujua hayo ya kuondoka mikono mitupu

Klmmyk

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walijua hilo ndiyo maana walikopa.
Ni aibu kwa bunge kuweka dhamana mshahara wa mbunge apate mkopo.

Hii inaashiria bungeni ni sehemu ya kupata mitaji na si kuwakilisha watu, kuna haja gani ya mbunge kukopa?,zamani wakati WA nyerere tuliambiwa wabunge walikuwa wanachelewa vikao vya bunge, wanashindwa kutembelea majimbo kutokana na miundombinu duni pia kukosa usafiri WA uhakika na ndipo walipoanza kukopeshwa magari .

Je, Leo kuna ulazima WA kukopesha gari?

Tujifunze kwa watu.
US, miongoni mwa ofisi za Congress ni pamoja na zile zilizoko majimboni ikiwemo staff na Mali zote. Pale panapokuwa hakuna mbunge kwa kifo au kujiuzulu ofisi inakuwa chini ya congressional cleck.
Yaani magari, katibu wa mbunge na ofisi za majimbo zinapaswa kuwa Mali ya bunge na havitakiwi kuwa personal na ndiyo maana wabunge Ama wanafaidi au wananyonyoleka.

Hawa si wabunge wetu ni ubunge wao na uwakilishi wao.
 
Heri yao yeye ataondoka na korona tumsahau kabisa,sura imevimba kama kala amira

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anataka kutuaminisha kwamba wabunge wana hali mbaya zaidi ya watumishi wa umma na wale watanzania wanaotambulikana na mzee fulani kwa jina la wanyonge.
 
So what ???

Waondoke na lolote wasiondoke na chochote inamsaidia nini mwananchi?


Ujinga mzigo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…