Spika Ndugai haya uliyosema kuhusu Wabunge wa CHADEMA waliofukuzwa mbona mwaka 2017 hukuyasema wabunge wa CUF walipotimuliwa?

Akili za huyo Spika ni kielelezo cha viongozi wa CCM na wanachama wake.

Hivi mambo kama haya anayofanya huyo mgogo kwa kuvunja katiba aliyoapa kuilinda hawezi kushitakiwa kwa TREASON? TLS ndio mambo mnayotakiwa kuyashuhulikia kulinda heshima ya taaluma yenu! Ndugai ni mhaini.
 
Mimi nadhani kumlaumu mtu ambae uwezo wake ni mdogo na wewe unajua kabisa ana uwezo mdogo ni kosa pia...nilimsikiliza anasema : "walioneshwa presentation China kuhusu bandari ya bagamoyo akiwa amepelekwa na balozi wa Tanzania huko China"
nilihudhunika sana kwa kweli hawa ndio aina ya viongozi tunataka Nchi iendelee kazi tunayo kwa kweli...
 
Upo sahihi kabisa maana hii ni aibu ya mwaka .
Haijawahi kutokea bunge la tanzania kuingia kwenye hii aibu.
 
Kama Nape Nnauye atakomaa nao lazima watatolewa nduki bungeni.

Nyuma ya Nape kuna nguvu kubwa isiyoonekana ambayo imeapa kuvisambaratisha vikaragosi vyote vya naniliu!
Namshukuru sana Mungu kwa kukuondolea mauza uza ya ccm kichwani mwako na sasa upo huruuuu.

Nayakemea mapepo toooooka
Nayakemea mapepo tooooka
 
Naomba wataalamu wa Sheria watuambie, Je HAIWEZEKANI kwenda kuiomba Mahakama ifanye Judicial Review ya hii issue?
 
Mimi naamini Mama yuko nyuma ya Nape na watu wasidhani hawa jamaa walioamua kufunguka wanakurupuka, bali wajue wana support kubwa tu ya watu wazito katika chama na serikali.
Ndugaye ndiyo safari yake ya kustaafu inaanza kuingiwa na mikosi.

Jiwe angekuwepo wala kusingekuwa na mashaka sana kwa Ndugaye.
 
Upo Sawa kumwonea huruma, na ni desturi zetu waafrika kuwaonea Huruma na kuwafariji waliopatwa na msiba! Nakuunga mkono na nitafuata nyayo zako! Kufiwa na #munguwakabudi ambaye ni #yesuwalugola siyo jambo dogo!
Umemsahau na Ally Kesi
 
Naomba wataalamu wa Sheria watuambie, Je HAIWEZEKANI kwenda kuiomba Mahakama ifanye Judicial Review ya hii issue?
Hata kama binafsi sina ABC za sheria lkn naona lipo wazi sana .

Inawezekana kabisa kwenda mahakamani kuomba tafsiri ya sheria inayotumika kuwaweka hawa wabunge wasiyo na chama.
 
Nami sitoshangaa kama Baraza kuu la chama mpaka kufika 2025 litakuwa halijaketi kusikiriza hizo rufaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…