Spika Ndugai, ili kujenga heshima jiuzulu Uspika wa Bunge

Spika Ndugai, ili kujenga heshima jiuzulu Uspika wa Bunge

Kwa sasa Ndugai anahesabika kama kibaraka wa Magufuli! Hawezi kuongoza bunge kwa raha aliyoizoea na hana confidence ya kuikaripia serikali tena!
 
SPIKA NDUGAI AJIUZULU USPIKA

Mjukuu wa Mwalimu

Kujiuzulu uspika wa Bunge ndiyo ushauri wa haraka ambao ningeweza kumshauri Job Ndugai, kama ningekuwa mshauri wake wa masuala ya kisiasa.

Kwanini?

1. Spika kwenye Bunge la Tanzania anatokana na chama cha siasa. Vyama huchuja na kupitisha mtu mmoja ili akagombee uspika kisha hupigiwa kura na wabunge. Mwenyekiti wa chama chako akitamka hadharani kauli zinazoonesha wewe hutoshi au hufai kukalia kiti cha uspika, busara ni kuachia ngazi.

2. Spika ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, chombo chenye nguvu zaidi ya kufanya maamuzi ya mara kwa mara, kwa kukasimiwa madaraka na vyombo vingine vya chama. Huko katika vikao vya Kamati Kuu, Rais Samia ndiye mwenyekiti wa vikao na tayari ameonesha kuwa mjumbe mmojawapo (Spika) hana nia njema na serikali pamoja na utekelezaji wa ilani ya chama. Hivyo anayetuhumiwa busara ni kukaa pambeni.

3. Spika amesemwa hadharani na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama chake pia kuwa mawazo yake yapo kwenye jinsi atakavyonufaika na uchaguzi mkuu wa 2025. Lolote atakalofanya bungeni la kuibana serikali itaonekana ni harakati zake za uchaguzi wa 2025 na akiisifia au kuiunga mkono serikali itaonekana anafanya UNAFIKI TU. Hivyo, hakuna atakalofanya lisilete maneno. Busara ni kujiuzulu.

4. Kwa utamaduni wa CCM, NI LAZIMA Rais aliyeongoza muhula mmoja AACHIWE kugombea tena muhula wa pili. 2021 - 2025 ya Rais Samia inahesabika muhula wa kwanza. Mtu kama Spika anayetokana na CCM kutangazwa hadharani kuwa ana HOMA YA 2025, na pengine ana JAMBO LAKE tofauti na utamaduni na utaratibu wa chama, busara ni KUPISHA. Iwe ni kweli au lah busara ni kujiuzulu tu.

Utamaduni wa kujiuzulu haujazoeleka sana Afrika na Tanzania. Kwa wenzetu, watu hujiuzulu si kwasababu tu wamekosea bali hata kama mawazo yako yametofautiana sana na wenzako walio wengi au mkuu wako.

KWETU TANZANIA licha ya Spika kuwa mkuu wa muhimili wa Bunge kama alivyo Rais ambaye ni mkuu wa muhimili wa Serikali lakini kama Spika na Rais wanatoka chama kimoja hasa CCM, basi Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama tawala ndiye bosi wa Spika. Kutoa kauli zinazotafsiriwa kama ni za kumpinga au kumzodoa Rais na mwenyekiti wa chama chako hasa kama mawazo yako hujayatolea ndani ya vikao halali vya kikatiba na kisheria ni DOSARI KUBWA.

#BUNGEHURU

View attachment 2068729
Unasemea huku sio kawaida ku resign shida ni kuwa huku kwetu ni njaa Sana.
Mtu mwenye njaa akili yako haipo vizuri mkuu. Ila aliyeshiba analinda jina lake kuliko chochote huyo bado analinda ugali wake
 
Spika kwenye Bunge la Tanzania anatokana na chama cha siasa. Vyama huchuja na kupitisha mtu mmoja ili akagombee uspika kisha hupigiwa kura na wabunge. Mwenyekiti wa chama chako akitamka hadharani kauli zinazoonesha wewe hutoshi au hufai kukalia kiti cha uspika, busara ni kuachia ngazi.

Spika ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, chombo chenye nguvu zaidi ya kufanya maamuzi ya mara kwa mara, kwa kukasimiwa madaraka na vyombo vingine vya chama. Huko katika vikao vya Kamati Kuu, Rais Samia ndiye mwenyekiti wa vikao na tayari ameonesha kuwa mjumbe mmojawapo (Spika) hana nia njema na serikali pamoja na utekelezaji wa ilani ya chama. Hivyo anayetuhumiwa busara ni kukaa pembeni.

Spika amesemwa hadharani na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama chake pia kuwa mawazo yake yapo kwenye jinsi atakavyonufaika na uchaguzi mkuu wa 2025. Lolote atakalofanya bungeni la kuibana serikali itaonekana ni harakati zake za uchaguzi wa 2025 na akiisifia au kuiunga mkono serikali itaonekana anafanya UNAFIKI TU. Hivyo, hakuna atakalofanya lisilete maneno. Busara ni kujiuzulu.

Kwa utamaduni wa CCM, NI LAZIMA Rais aliyeongoza muhula mmoja AACHIWE kugombea tena muhula wa pili. 2021 - 2025 ya Rais Samia inahesabika muhula wa kwanza. Mtu kama Spika anayetokana na CCM kutangazwa hadharani kuwa ana HOMA YA 2025, na pengine ana JAMBO LAKE tofauti na utamaduni na utaratibu wa chama, busara ni KUPISHA. Iwe ni kweli au lah busara ni kujiuzulu tu.

Ndugai Kutoa kauli zinazotafsiriwa kama ni za kumpinga au kumzodoa Rais na mwenyekiti wa chama chako hasa kama mawazo yako hujayatolea ndani ya vikao halali vya kikatiba na kisheria ni DOSARI KUBWA.

#BungeHuru
 
Hivi kwa kuvuliwa nguo vile unawezaje kwenda kuongoza kikao cha bunge!? Nadhan hata wabunge wakicheka anawezadhan anachekwa yeye.
 
Kwa uelewa wangu spika aliharibu sana kuomba msamaha kwani he had very little to lose.
1. Yeye sio waziri, kwamba rais anaweza tengua uteuzi wake. So mamlaka ya KIDEMOKRASIA aliyonayo rais kwa spika ni kidogo sana.

2. Kwa sasa rais, kwa ajili za kawaida kabisa, hawezi kuvunja bunge akaitisha uchaguzi.... hata yeye anajua kuwa hajajiestablish vyema kuwa na confidence ya kuchaguliwa na WANYONGE ambao bado mzimu wa mwendazake unawasumbua. Besides, hata miongoni mwa wabunge kuna anaona sense ya alichokiongea spika.

3. Tuchukulie worst case scenario, kwamba utawala wa sharia haukufuatwa na badala yake FIGISU NA FITNA zikatamalaki, akatemeshwa uspika. Bado angebaki kuwa mbunge, lakini ni mbunge aliyepigania anachokiamini, to the better or bitter end.

Though a civil gesture, but kwa nafasi hakupaswa kuomba msamaha
 
Kwa mtu mzima ambaye amekuwa kiongozi kwa muda mrefu, naamini Mh Job Yusto Ndugai ataamua kuachia ngazi ili kulinda kaheshima alikonako. Asipoachia ngazi kabla ya Bunge kuanza basi mambo mawili yanaweza kumtokea:
Ima CCM imuite, imuhoji na kumnyang’anya uanachama na hivyo kupoteza Uspika na Ubunge ama Bunge litoe hoja ya kumvua Usipika na kubaki na ubunge wake. Vyovyote itakavyokuwa, sioni Ndugai akikalia kiti cha Uspika kwenye kikao kinachoanza mwishoni mwa mwezi huu ama mapema mwezi ujao. Ndugai anaondoka, atumie busara kuchagua anaondoka vipi. Aondoke kwa kupokwa uanachama wa kijani ba hivyo kukosa Ubunge na Uspika au ajiuzulu Uspika na kubaki na ubunge wake au wabunge wamuondoe! Bora aondoke mwenyewe as this option is a lesser devil for his situation.

Kwa upande mwingine nilimsikia Mh Rais akisema nyumba ya akina Kassim ilikuwa inasema serikali yake ni ya mpito. Kassim (naamini ni PM), ni kiongozi wa shughuli za serikali Bungeni, sasa kama Bunge, ambalo yeye ni Mbunge No 1, linamsema Mh Rais basi ni vyema PM naye akaangalia busara katika hilo na hivyo kuachia tu ngazi ili Mh Rais apate nafasi ya kuunda serikali upya kama atataka kumrudisha basi atamteua. Pia Mh Rais kasema kuna Mawaziri wanaoangalia 2025 badala ya kufanya kazi na hivyo atawatoa; PM kama mkuu wa Mawaziri anatakiwa kutumia busara na kuandika kwa Mh Rais ili akae kando na kumpa nafasi Mh Rais kupanga vyema Serikali yake na kuondoa wale wote wenye matamanio ya 2025. Kumbuka PM akijiuzulu Baraza la Mawaziri linapoteza uhalali hivyo kumlazimu Rais kuunda upya serikali kuanzia PM.

Ni imani yangu kwamba kwa hali ilivyo hawa wakuu wawili wanatakiwa kutumia busara na kuamua kumpisha Mh Rais.
 
Back
Top Bottom