Spika Ndugai: Sheria ya kutaifisha ng'ombe wanaoingia hifadhini ni dhuluma. Ilipita tukiwa tumelala?

Spika Ndugai: Sheria ya kutaifisha ng'ombe wanaoingia hifadhini ni dhuluma. Ilipita tukiwa tumelala?

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema Sheria ya Serikali kutaifisha Ng'ombe wanaoingia maeneo ya Hifadhi ni tatizo, akiita kuwa Sheria yenye dhuluma.

Amesema, "Hii Sheria sijui ilipita wapi, tulikuwa tumelala au ilikuaje. Ile kwamba Ng'ombe wakiingia kwenye Hifadhi wanataifishwa wote, hapana! Kama ni ya miaka ya karibuni sijui nilikuwa nimesafiri nimeenda wapi".

Ameeleza, Tembo kutoka Hifadhini wanazurura na kula mazao ya watu akisema kuwepo usawa kwenye suala hilo na kuitaka Serikali kuliangalia.
 
Ndugai anatakiwa ajiulize kama umeweka sheria ya kutaifisha na bado watu wanaingiza mifugo, ukiitoa hiyo sheria je?

20210527_213348.jpg
 
Watu takribani 400 wanapokaa na kufanya maamuzi ta hovyo hovyo. Kujua ng'ombe na mbusi ni sawa na nyumbu na swala wanao walinda kwenye hizo hifadhi imewawia vigumu. Ubaguzi wa kimaumbile wa wanyama.

Sheria hii itenguliwe maramoja wafugaji wspewe elimu ya jinsi ya kutunza mazingira. Wajue faida zake na umuhimu wa kufanya hivyo. Ziwepo faini za kumfundisha na wala si kumkomoa atakaye shindwa kutii.
 
Hivi huyu jamaa yuko poa upstairs? Mbona ni kama mtu aliyechanganyikiwa hivi?
 
Retired huyu alikua wapi kabla ya msiba?
Ilipita kwa sababu mlikuwa mkimuogopa magufuli,hakuna mswada hata mmoja ambao ulikwama kupitishwa wakati wa magufuli leo ndugai anastaajabu nini wakati yeye ndiye alikuwa tatizo hapo bungeni maneno anayoongea ndugai cku hizi hapo bungeni uatafikiri ndio kwanza anaingia bungeni.
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema Sheria ya Serikali kutaifisha Ng'ombe wanaoingia maeneo ya Hifadhi ni tatizo, akiita kuwa Sheria yenye dhuluma.

Amesema, "Hii Sheria sijui ilipita wapi, tulikuwa tumelala au ilikuaje. Ile kwamba Ng'ombe wakiingia kwenye Hifadhi wanataifishwa wote, hapana! Kama ni ya miaka ya karibuni sijui nilikuwa nimesafiri nimeenda wapi".

Ameeleza, Tembo kutoka Hifadhini wanazurura na kula mazao ya watu akisema kuwepo usawa kwenye suala hilo na kuitaka Serikali kuliangalia.
Sijawahi kuona Spika mnafiki kama Ndugai tangu tupate Uhuru.
 
Upinzani ukihoji Alikuwa anawafungia miezi kadhaa Hakuna vikao
 
Ni kweli kama anavyosema mwenyewe Ndugai kua walikua wamelala na sasa pengine ndio wanakurupuka kutoka usingizini!

Zipo sheria nyingi za hovyo na zakushangaza kama ile ya mtu akikutwa na hatia ya kusafirisha kilo 50 za mirungi anahukumiwa kifungo cha MAISHA jela! Kisa mirungi imewekwa kwenye kundi la dawa za kulevya.

Jambazi wa kutumia silaha au mbakaji wao ni miaka 30 tu jela. Lazima mtu uhoji utimamu wa afya ya akili ya waliotunga hizo sheria
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema Sheria ya Serikali kutaifisha Ng'ombe wanaoingia maeneo ya Hifadhi ni tatizo, akiita kuwa Sheria yenye dhuluma.

Amesema, "Hii Sheria sijui ilipita wapi, tulikuwa tumelala au ilikuaje. Ile kwamba Ng'ombe wakiingia kwenye Hifadhi wanataifishwa wote, hapana! Kama ni ya miaka ya karibuni sijui nilikuwa nimesafiri nimeenda wapi".

Ameeleza, Tembo kutoka Hifadhini wanazurura na kula mazao ya watu akisema kuwepo usawa kwenye suala hilo na kuitaka Serikali kuliangalia.
This is a proof that the speaker is never serious!
 
Wazee wa kukurupuka kwa midundo na mapambio... utawala ukibadilika na wao wanabadilika tabia!!!
Tukirudi kwenye mada: Na wanyamapori wakiingia kijijini wataifishwe na kijiji au wenye mashamba kufidia uharibifu uliofanyika na uvamizi huo ".... au nasema uongo ndugu zangu?"
 
Back
Top Bottom