Spika wa bunge kugeuka mpiga debe wa Wachina ni aibu kubwa

Spika wa bunge kugeuka mpiga debe wa Wachina ni aibu kubwa

Kijogoodi

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2021
Posts
1,362
Reaction score
2,373
Naam.

Tangu mwaka 2018 pale spika Ndugai alipolipiwa kila kitu na wachina kwenda kuonyeshwa presentation ya namna bandari ya Bagamoyo itakavyokuwa ikijengwa, basi amegeuka mpiga debe wao!

Ndugai akiulizwa kwani bandari zilizopo zina kasoro gani hadi upigie debe Wachina kiasi hiki? Ndugai hana jibu ila yeye anachotaka bandari ijengwa.

Ndugai akiulizwa atoe mifano ya nchi zilizofanyiwa uwekezaji wa namna hiyo na wachina alafu zikafanikiwa hataji, akiambiwa mbona Srilanka, Mombasa, Zambia wanalia kwa uwekezaji na namna hii? Ndugai hana jibu ila anachotaka ni bandari tu ijengwe.

Ndugai akiulizwa, alikuwa wapi toka mwaka 2018 alipobaini rais Magufuli amedanganywa kutoa ukweli wote hadharani bungeni ? Alikuwa anaogopa nini wakati spika hawezi kutumbuliwa na rais? Ndugai hana jibu ila anachotaka tu wachina wapewe Bagamoyo!

Ndugai akiulizwa huo mkataba unaousema ni mzuri uko wapi uweke hadharani ili kila mtanzania ajiridhishe na matunda yatakayopatikana baada ya wachina kuwekeza Trilioni 23? Ndugai hana jibu!

Kiukweli ni aibu kubwa sana kwa nchi yetu kama mtu anaweza kufikia ngazi ya spika wa bunge alafu akashabikia na kuwa mpiga debe kwa faida ya nchi nyingine.
 
Hawezi kutumbuliwa?mwenyekiti wa chama akimuundia zengwe anafukuzwa uanachama ubunge hana tena
 
Nyiie mnaopinga Wachina mbona mkiulizwa mna mbadala gani hamtoi? Au mnafurahia Meli kuishia kule Baharini na kupakua mwezi mzima???
 
Ni zaidi ya aibu,
Auweke mkataba bungeni waujadili na pia raia nao wapewe access ya kuona mkataba huo waupitie nao
Siyo watu wachache tu wanataka kufanya maamuzi waupitishe,yawazekana kuna watu
Hapo wana maslahi huwezi jua

Ova
 
Auweke mkataba bungeni waujadili na pia raia nao wapewe access ya kuona mkataba huo waupitie nao
Siyo watu wachache tu wanataka kufanya maamuzi waupitishe,yawazekana kuna watu
Hapo wana maslahi huwezi jua

Ova
Ni kweli mkuu halafu wanataka watulazimishe kukubaliana nao ,

Wauweke wazi kwenye gazeti la serikali tusome.
 
Ni kweli mkuu halafu wanataka watulazimishe kukubaliana nao ,

Wauweke wazi kwenye gazeti la serikali tusome.
Waweke wazi tu wataalam waipitie
Wasitake kufanya mambo juu kwa juu
Mara kesho au kesho kutwa wakafanya
Maamuzi

Ova
 
Katumwa kupima upepo huyu,anacho sahau Ayubu ni kuwa,hilo zigo la mavi alilobebeshwa,harufu atanuka yeye wabebeshaji wakimruka na kubana pua zao.(Nje ya mada;hivi arv zaweza punguza uwezo wa mtumiaji wake kufikiri eeeh!)
 
Huna akili wewe.

Bandari ya DSM imeshachimbwa meli yenye ukubwa wowote inatia nanga tangu mwaka 2019

China ya sasa siyo china ya Mao. Kama hatutokuwa makini kwa tamaa zetu za maendeleo ya haraka tutaingia mikataba ije kuviumiza vizazi vyetu vijazo,ila kwa mtu ambaye ana mawazo ya leo tu anasema najinufaisha mimi tumbo langu hao wanaokuja watajua wenyewe.Na tatizo kubwa ambalo linatugharimu hatuna umoja.Maskini spika wa Bunge ana mawazo ya leo tu kesho amuachie mzigo anayekuja.hebu tujaribu kusoma historia ya mkataba wachina na uingereza jimbo la Hong Kong.
 
China ya sasa siyo china ya Mao. Kama hatutokuwa makini kwa tamaa zetu za maendeleo ya haraka tutaingia mikataba ije kuviumiza vizazi vyetu vijazo,ila kwa mtu ambaye ana mawazo ya leo tu anasema najinufaisha mimi tumbo langu hao wanaokuja watajua wenyewe.Na tatizo kubwa ambalo linatugharimu hatuna umoja.Maskini spika wa Bunge ana mawazo ya leo tu kesho amuachie mzigo anayekuja.hebu tujaribu kusoma historia ya mkataba wachina na uingereza jimbo la Hong Kong.
Wachina wako vizuri tu kwenye uwekezaji. Ndio wawekezaji wakubwa duniani siku hizi kwa kuwa wana mapesa mengi.

Hata mradi wa bomba la mafuta uliosainiwa jana,pamoja na wafaransa,wachina ni wanahisa wakubwa pia.

Lakini pia,kwenye uwekezaji wa Bagamoyo,kuna Oman ndio wanaotoa pesa. Wachina ni utaalamu na uendeshaji kwa kuwa wanauzoefu na mambo ya bandari.

Kwa ujumla,mradi huu ni mzuri mno,una manufaa makubwa kiuchumi. Kuhusu terms,tunaweza kunegotiate tukapata nzuri. Biashara huwa ni kubargain.
 
Back
Top Bottom