Spika wewe ni kiongozi wa Mhimili wa Bunge, iache Serikali ijipambanie yenyewe sakata la sukari

Spika wewe ni kiongozi wa Mhimili wa Bunge, iache Serikali ijipambanie yenyewe sakata la sukari

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Katika hili sakata,

1. Inashangaza kwamba spika ndio umekuwa wa kwanza badala ya Waziri Bashe au upande wa serikali kumtaka Mpina alete uthibitisho au maelezo kwamba Waziri Bashe amelidanganya bunge katika suala la upungufu wa sukari na mchakato mzima uliofutia wa manunuzi ya sukari ya ziada nje ya nchi.

2. Inashangaza kwamba unasema Mpina amekiuka taratibu za bunge kwa kuwasilisha taarifa yake mbele ya umma wakati kanuni za bunge zinakataza kuwasilishwa kwa umma taarifa mahususi ambayo imeandaliwa kwa ajili ya kuwasilishwa bungeni. Taarifa ya Mpina ni mahususi? Mbunge akisema bungeni Tanzania ina raia milioni 70 halafu mbunge mwingine akabisha kwa kuonyesha ripoti ya sensa inayoonyesha Watanzania wako milioni 60 hiyo taarifa ya sensa inakuwa taarifa mahususi?

Kuna umahususi gani kwenye kusema fulani amedanganya na kutumia taarifa au nyaraka public kuonyesha uongo wake?! Hata hivyo taarifa ya Mpina bado sio mahususi kuwasilishwa bungeni kwa sababu spika au kamati yake wanaweza wasiiwasilishe bungeni, hio sio taarifa kama taarifa rasmi za kamati za bunge, hotuba za bajeti au kamati teule kama ile ya Mwakyembe sakata la Richmond ambazo hakuna namna spika anaweza kuzuia kuwasilishwa bungeni.

3. Jambo la kushangaza zaidi spika anaisifia serikali kwa utulivu! Kwa kukaa kimya na kutojibu hoja za Mpina!. Hapa mimi ndio nimechoka zaidi.
 
Spika yuko kwenye kamati ya kuwaombea watuhumiwa wa report ya CAG msamaha. Wale watuhumiwa wa report ya CAG huwa wako wanao ombewa msamaha na Spika wa Bunge.

Usitegemee kitu hapo
 
Kuna aina ya viongozi wa juu wametuvunja moyo tunaopambana na "nadharia potofu!"
Watu wa "vitabu kale" wanazid kuimarisha nadharia zao.
Najua mmenielewa.
 
Ana maslahi na Serikali, mumewe aliteuliwa na Raisi. Huyo betina hayuko na wananchi, yuko kupambania familia yake na Serikali.

Katika kitu tunakosea ni kupachika watu vyeo vikubwa, bila kuangalia kwa jicho la 3. Betina na Bashe ni wa kuachia ngazi watuposhe.
 
Tulia spika wa Serikali

Yeye hajali wananchi tumeumizwa kiasi gani kwa kulanguliwa kwenye sukari ili Mafisadi waweze kupiga hela!
 
Tunapitia kipindi kigumu mno Mungu atunusuru na hawa mafisadi
 
Kheri yule bwana ana kuua uku ana kuangalia usoni sio hizi pimbi
 
Katika hili sakata,

1. Inashangaza kwamba spika ndio umekuwa wa kwanza badala ya Waziri Bashe au upande wa serikali kumtaka Mpina alete uthibitisho au maelezo kwamba Waziri Bashe amelidanganya bunge katika suala la upungufu wa sukari na mchakato mzima uliofutia wa manunuzi ya sukari ya ziada nje ya nchi.

2. Inashangaza kwamba unasema Mpina amekiuka taratibu za bunge kwa kuwasilisha taarifa yake mbele ya umma wakati kanuni za bunge zinakataza kuwasilishwa kwa umma taarifa mahususi ambayo imeandaliwa kwa ajili ya kuwasilishwa bungeni. Taarifa ya Mpina ni mahususi? Mbunge akisema bungeni Tanzania ina raia milioni 70 halafu mbunge mwingine akabisha kwa kuonyesha ripoti ya sensa inayoonyesha Watanzania wako milioni 60 hiyo taarifa ya sensa inakuwa taarifa mahususi?

Kuna umahususi gani kwenye kusema fulani amedanganya na kutumia taarifa au nyaraka public kuonyesha uongo wake?! Hata hivyo taarifa ya Mpina bado sio mahususi kuwasilishwa bungeni kwa sababu spika au kamati yake wanaweza wasiiwasilishe bungeni, hio sio taarifa kama taarifa rasmi za kamati za bunge, hotuba za bajeti au kamati teule kama ile ya Mwakyembe sakata la Richmond ambazo hakuna namna spika anaweza kuzuia kuwasilishwa bungeni.

3. Jambo la kushangaza zaidi spika anaisifia serikali kwa utulivu! Kwa kukaa kimya na kutojibu hoja za Mpina!. Hapa mimi ndio nimechoka zaidi.
Aisee, hii ya 3 ndio imenishangaza. Hii ina maana hata kwa ule ushahidi yeye anaona serikali haina cha kujibu. Huyu mama nadhani alihisi mpina hana ushahidi.
Hii nchi inapitia kipindi kigumu sana.
 
Mara kadhaa nimeandika huku ndani Tanzania hakuna Bunge bali kundi la wachache watumia Kodi za walalahoi.
 
Spika Tulia anatumika na serikali kumtuliza na kumzima Mpina.

Nkonyofu fijho unkikuru ujhu.
 
Back
Top Bottom