St. Francis Mbeya kuna siri gani?

St. Francis Mbeya kuna siri gani?

Mdwe
Elimu ya siku hizi imekuwa mdebwedo sana! Ukitaka kujua hili waulize walimu wa vyuo na waajiri. Binafsi sio Mara moja nimewafanyia interview vijana kwenye mambo ya kazi na naishia kusikitika jinsi uelewa wao ulivyo wa mashaka.
Mdwebedo huo upo kwa private tu ambao mtihan ni mmoja lakini ukienda serikali huko vijijin ni masifuri na four😂
 
Ujinga punguza kaangalie majina ya hao watoto kama kuna mnyakyusaa
 
Watanzania tuko kinyume sana na mafanikio ya wengine......mioyo yetu na akili zetu muda wote zinatarajia habari mbaya na maanguko ya watu baada ya mafanikio......

Taarifa za mafanikio ya mtu au kikundi cha watu tunazipokea kwa mshituko wa chuki na hasira ili kufurahisha mioyo yetu hasi tunatafuta namna ya kuyatia doa mafanikio hayo.......

Wengi wetu hatutambui na kuthamini juhudi za watu wengine juu ya mafanikio yao badala yake tunawapachika majina mabaya......

Ili uishi Tanzania unatakiwa kuwaelewa watanzania na hawa ndio waTanzania kwa wingi wao......

Hongereni ST FRANCIS MBEYA juhudi zenu zimeonekana na kuwaangaza kwa watu wanaoshangilia na kufurahia mafanikio ya watu.....
Hujakosea hata kidogo,Watanzania wengi tumeumbwa na roho za ajabu sana,kupongeza juhudi na mafanikio ya mtu ni nadra sana,mtu akiwa tajiri ni mwizi au freemason anaua ndugu zake wakati wewe unashinda kutwa Simba ,Yanga.
Nimewahi kusikia wakati wa Ndalichako hizi St kuwa zilikuwa zinapendelewa,mbona Ndalichako hayupo na bado zinadunda?Tupunguze wivu.....Hongereni sana wale mliofanya vyema
 
Na mwaka wamefanya tena kinyaa
 

Attachments

  • Screenshot_2024-01-25-19-39-42-78.png
    Screenshot_2024-01-25-19-39-42-78.png
    33.8 KB · Views: 8
Aliyefaulu kiukweli bila kuiba mtihani ni huyo wa Ilboru, kipindi nimeenda advance level darasa letu lilikuwa na hao waliotoka st Francis na kila mtu aliwaogopa chakushangaza mtihani wa kwanza marks walizopata ni tofauti na hizo one zao. Huko private ni business kwa kwenda mbele na solving za paper kwa ajili ya kupata A za kutosha wakati zikija kitaa inputs yake ni zero kabisa
Vyuoni wengine wanaacha vyuo kabisa
 
Hujakosea hata kidogo,Watanzania wengi tumeumbwa na roho za ajabu sana,kupongeza juhudi na mafanikio ya mtu ni nadra sana,mtu akiwa tajiri ni mwizi au freemason anaua ndugu zake wakati wewe unashinda kutwa Simba ,Yanga.
Nimewahi kusikia wakati wa Ndalichako hizi St kuwa zilikuwa zinapendelewa,mbona Ndalichako hayupo na bado zinadunda?Tupunguze wivu.....Hongereni sana wale mliofanya vyema
Ila yeye anaetuhumu akipata utajiri ni halali,waafrika bure kabisa!
 
Ujinga punguza kaangalie majina ya hao watoto kama kuna mnyakyusaa
Ungemrekebisha katika hoja yake, ila kusema Wanyakyusa hawapo ni kujidanganya. Kuna wanyakyusa kwa majina yao na kuna wasiotumia majina ambayo yana identify asili yao.
 
Vyuoni wengine wanaacha vyuo kabisa
Kwa hiyo watu wanavyoshonana huko kila mwaka kutafutia watoto wao nafasi kwenye hizo shule, lengo lao ni watoto wakifika vyuo vikuu wakimbie elimu?
Nitafutie mmoja tu unayemjua wewe aliyetoka hizo shule ambaye alikimbia chuo sababu ya ugumu wa masomo.
 
Ungemrekebisha katika hoja yake, ila kusema Wanyakyusa hawapo ni kujidanganya. Kuna wanyakyusa kwa majina yao na kuna wasiotumia majina ambayo ya identify asili yao.
Yaan siko hanta into wanyaki .nachukia maukanda na maukabila hiyo shule haihusiani lolote na mbeya pride ikihamia zanzibar itapata the same marks heshima iende kwa kanisa katoliko
 
Yaan siko hanta into wanyaki .nachukia maukanda na maukabila hiyo shule haihusiani lolote na mbeya pride ikihamia zanzibar itapata the same marks heshima iende kwa kanisa katoliko
Ndiyo maana nikakushauri kwamba, mrekebishe katika namna ya kuto dis wengine, wengi tunachukia ukanda sababu una madhara kuliko faida.
Jinsi ulivyoiweka inaonyesha unawachukia watu wa kanda fulani, kama yeye anavyojaribu kuwapa sifa watu wa kanda hiyo.
 
Hahahah hizi Ilboru, Kibaha, Mzumbe, Tabora, Kilakala na shule zingine kongwe za serikali zinakuwaga na majitu yenye akili za kutisha. Imagine mwaka 2006 Tanzania one form six katoka Tosamaganga. Raha ni kwamba hawa majamaa hadi chuo yanakimbiza hatari kabisa.
Ndiyo wewe nini? Nilikipiga hapo!!
 
Sio kwamba hawafundishi ila naomba kujua data kama tatu:-

Wote walioingia walikuwa na Passmark kiasi gani (creme de la cream)
Michujo ilifanyika kiasi gani (yaani potential failures wote kuondolewa)
Ufundishaji mzuri na kulenga mitihani (sijajua uelewa wa hawa vijana wala thinking capacity yao ila Mitihani hii ilivyo unaweza ulenga mitihani kwa kukariri hata kama thinking capacity yako ni ndogo)

Kwahio binafsi ubora wa shule naupima kwa mtu kumtoa point A kwenda B; bila mchujo wala kuchagua wanaojiweza pekee..., kama mtu amekuja hajui kitu na after four years akapata hata three huenda shule hio imefanya kazi kuliko kuchukua the best na katika hao best wale wote ambao ni better kuwabakisha madarasa (hio haijengi sababu hata Div 1 mpaka Three kwa form four bado ni ufaulu na kuna a long way forward na kuna a room for improvement
Duniani kote kuna shule za serikali na private za vipaji maalumu ambazo huchukua the best only kujiunga nazo

Mfano kwa Tanzania vipaji maalumu ziko kama Mzumbe sekondari, tabora boys, kibaha sekondari nk huko hupelekwa vipanga waliofaulu hasa mitihani yao

Private pia kuna shule za watoto vipaji maalumu wenye ufaulu mkubwa kujiunga ndizo kama hizo St Francis nk usishangae hilo liko pote duniani

Hata vyuo vikuu kuna ambavyo huchukua vipanga tu asikikia kubwa kwa Tanzania ni UDSM na Muhimbili
 
Hivi pale St. Francis Girls Mbeya pana siri gani wazee? Mwaka huu licha ya kwamba imekuwa ya pili kitaifa lakini ufaulu wake ni wa ajabu na kuogofya sana.

Picha linaanza darasa lina watahiniwa 92 ambao wote wamepata div 1, hii si ajabu sana ajabu ni hili hapa kati ya hizo 1- 92, div 1.7 ambazo ndo ufaulu wa juu kabisa nchi hii kwa upande wa olevel zipo 79 yani 1.7 pale St Francis Girls zipo 79 kama utapata shida kuelewa na maanisha hivi wanafunzi waliopta A saba kwenye jumla la masomo yao wapo 79.

Mwanafunzi wa mwisho pale yani mwenye ufaulu dhaifu au unaweza kuuita goigoi ama kilaza, mmoja ana div 1.14 na mwingine ana div 1.13 na wapo wawili pekee.

Mabinti wamejua kukung'uta aisee div 1.10 ipo moja, 1.9 zipo 6 na 1.8 zipo 4

Kama unadhani maajabu yao mwaka huu ni hayo tu basi Pole mabinti hawa wameendeleza maajabu mpaka kwenye Wanafunzi bora ambapo kumi bora imepambwa na wao.Hatari sana hii mwanafunzi 1-5 kwenye kumi bora anatoka kwao afu wanajichomeka others kwenye 6,kisha namba 7 wanarudi wao afu 8,9 wanajikongoja fedha na ilboru kisha kumi kitabe kabisa wanamaliza wao. Kifupi 10 bora wanafunzi 7 wote wametoka St FRANCIS.

1. Consolata Prosper Luguva - St. Francis Mbeya🔴

2. Butoi Ernest Kangaza - St. Francis🔴

3. Wllhemia Steven - St. Francis 🔴

4. Cronel John - St Francis🔴

5. Merry George Ngoso - St Francis🔴

6. Holly Beda Lyimo - Bright Future
Girls🔴

7. Brandina - St. Francis🔴

8. Imamu Suleiman - Feza Boys

9. Mfalme Hamis Madili - Ilboru

10. Clara Straton - St. Francis🔴

Huu ufaulu si wa kitoto, sasa nauliza siri yao hasa ni ipi maana tangu miaka hiyo hawa mabinti wamekuwa moto ina maana shule zingine wameshindwa kabisa kujifunza?

View attachment 2082037

View attachment 2082038
Watu wanagonga A maths as fuq
 
Back
Top Bottom