St. Francis Mbeya kuna siri gani?

St. Francis Mbeya kuna siri gani?

Maswali mepesi lakini mbona wanafunzi wengine kule Kazulamimba wanafeli? Hawa watoe strategies tujue wengine waige vipi. Inaniuma kuona karne hii wanafunzi wanashindwa kufaulu hata kidato cha nne. Kuna jamaa yangu alifeli form 2 nilisoma name shule moja ya ajabu ajabu uko. Juzi akanambia eti daktari alivyompima akamwambia anaumwa ugonjwa unaitwa "INFECTIONS", nikamuuliza mara mbili na akasisitiza sana.

Sasa taifa linakuwa na watu wa hivi hata kutumia mbolea shambani hawataweza, lishe kwa watoto hawawezi, uzalishaji wao kitaifa ni duni. Shule walienda kuishi, kuvaa sweta na kunywa uji. Elimu ya bongo hasa uswahilini uko ni ile wazazi wanawaambia watoto wao wakiwa wamefunga eti "mmetuchosha hebu shule zifunguliwe wazazi tupumzike". Hapo usitegemee maajabu ya kufaulu. Sasa hawa waliofaulu wangetoa strategies imekuwaje ingesaidia wengine
😅🤣🤣🤣
 
Hao wanafunzi wanaotoka Tanzania one huwa wanaishia wapi au wengine sahiv ni viongozi wakubwa...eee Elimu imenifanya niwe masikini.
 
Hamna siri yoyote ni kwamba wanachukuasawa na watoto cream kabisa, sasa inaachaje kuwa na matokeo safi
Hiyo ni shule private ya vipaji maalum ndio maana huchuja sana na kuchukua cream tu sawa na shule za serikali vipaji maalumu huchukua wale waliofaulu kiwango cha juu sana tu
 
Sie Waswahili tumewekeza sana kweny ufaulu na si ueleawa

Hizi division one kalikali zinapoteleaga wapi hadi hazionekani tena?

Tanzania one wa form four walio graduate sambamba na Samia Suluhu miaka hiyo sijui sasa hivi yupo pori gani wakati mwenzie sasa ni Rais?
Tena anaewachachafya chadema hatari🤣
 
Maswali mepesi lakini mbona wanafunzi wengine kule Kazulamimba wanafeli? Hawa watoe strategies tujue wengine waige vipi. Inaniuma kuona karne hii wanafunzi wanashindwa kufaulu hata kidato cha nne. Kuna jamaa yangu alifeli form 2 nilisoma name shule moja ya ajabu ajabu uko. Juzi akanambia eti daktari alivyompima akamwambia anaumwa ugonjwa unaitwa "INFECTIONS", nikamuuliza mara mbili na akasisitiza sana.

Sasa taifa linakuwa na watu wa hivi hata kutumia mbolea shambani hawataweza, lishe kwa watoto hawawezi, uzalishaji wao kitaifa ni duni. Shule walienda kuishi, kuvaa sweta na kunywa uji. Elimu ya bongo hasa uswahilini uko ni ile wazazi wanawaambia watoto wao wakiwa wamefunga eti "mmetuchosha hebu shule zifunguliwe wazazi tupumzike". Hapo usitegemee maajabu ya kufaulu. Sasa hawa waliofaulu wangetoa strategies imekuwaje ingesaidia wengine
Huyo daktari yupo sahihi.

Huenda huyo rafiki yako ana infections kwenye damu ambayo kitaalami wanaita Septicemia.
 
Mitihani ya siku hizi hamna kitu 1. Rais wa kwanza wa Tanzania ni nyerer......... 2. Binadamu ana macho mawi.......
kwanini wengine wafeli kama ni hivyo au wengine wanapewa mitihani tofauti? hujawaza kabla ya kutuma
 
Kwanza sipeleki mtoto huko, nampeleka kata hizo Hela namuwekea Kama mtaji, div 3 inatosha na Hela ya mtaji juu
Mtoto huwa harithishwi mtaji na mzazi hurithishwa biashara ambayo iko tayari ,kaulize wahindi,waarabu na wapemba

Huna biashara halafu unasema utamrithisha mtaji wewe mwenyewe huwezi kumpa biashara hiyo DNA uliyozalisha ndio itaweza?

Kama huna biashara hadi sasa ya kumpa msomeshe elimu bora akahangaike mwenyewe huko mbele

Huo utapeli wako wa kujitia eti unamuwekea hela ya mtaji baki nao mwenyewe

Rithisha biashara ambayo tayari inesimama

Acha utapeli
 
Hamna siri yoyote ni kwamba wanachukua watoto cream kabisa, sasa inaachaje kuwa na matokeo safi
Bora shule kama Tusiime, Loyola, Alpha, Shaaban Robert ,St Anthony wanachukua wanafunzi wa kawaida lakini wanatoka vizuri japo wapo makando kando wanaopata matokeo ya wastani.
 
Mimi binafsi nakataaa hayo matokeo aisee, hata kama wana akili huo ufaulu wa kiasi hicho kuna kitu cha ziada... Hiyo shule ichunguzwe vzuri kuanzia miezi mitatu kabla ya kufanya mtihani na siku za mitihani
Kinachofanyika wakati wa usaili wa kujiunga na kidato Cha 1,watahiniwa Huwa ni wengi nakumbuka 2015 nilimupeleka Binti yangu kufanya usaili walikuwa 850 .wakati wa kuchagua matokeo hupangwa kulingana na ufaulu . cut off ya uchaguzi huishia no 92 ,ambayo ndio idadi wanahohitaji.Wale wote waliochaguliwa ni top cream hivyo wanafundishika au darasani wanaongezewa Kwa kile walichokuwanacho kichwani .Hata continues assessment zao Kwa miaka 4 ni za ufaulu wa juu.Inapofika mtihani wa taifa lazima wafaulu Kwa kiwango Cha juu .Kwa hiyo hakuna kilicho kibaya juu ya ufaulu wao isipokuwa ni uwezo wao kiakili kufundishika
 
Hakuna ugonjwa unaitwa infection, infection ni maambukizi lazima u specify ni maambukizi ya nini?
Maambukizi yamefika mpaka kwenye damu kutoka kwenye source nyingine ambayo huenda ikawa ni skin, respiratory, urinary tract nk.

Sasa yakishafika kwenye damu wana term hivyo Septicemia .
 
Hizi shule mbali na kufundishwa vyema ila Huwa wanawezeshwa sana sitasahua kipindi Niko pugu tunajiandaa na mitihani ya form 6 necta nakuja kuamshwa na Mwana kwamba Kuna practical ya physics imetoka Marian Girls Bagamoyo hivyo tunatakiwa kui solve kabla ya alfajiri nilikesha nayo mpaka asbhi na tukaikuta vile vile.
 
Kinachofanyika wakati wa usaili wa kujiunga na kidato Cha 1,watahiniwa Huwa ni wengi nakumbuka 2015 nilimupeleka Binti yangu kufanya usaili walikuwa 850 .wakati wa kuchagua matokeo hupangwa kulingana na ufaulu . cut off ya uchaguzi huishia no 92 ,ambayo ndio idadi wanahohitaji.Wale wote waliochaguliwa ni top cream hivyo wanafundishika au darasani wanaongezewa Kwa kile walichokuwanacho kichwani .Hata continues assessment zao Kwa miaka 4 ni za ufaulu wa juu.Inapofika mtihani wa taifa lazima wafaulu Kwa kiwango Cha juu .Kwa hiyo hakuna kilicho kibaya juu ya ufaulu wao isipokuwa ni uwezo wao kiakili kufundishika
Pia nidhamu inapewa kipaumbele sana.

Mpaka nidhamu ya kula, pale ukibakisha chakula jiandae kwa suspension.
 
Hio shule inanunua mitihani na kufanya mwezi mmoja kabla ya mitihani ya taifa na huwa maswali yanarudiwa kwa msisitizo mkubwa Sana ......

Hao watoto wanaomaliza huko hawana uwezo kabisa wa kufaulu hivyo, never ever....

Hapa bongo ukishakuwa na pesa hakuna kinachoshindikana, paper za NECTA zinanunuliwa na watoto Wana solve mapema kabisa ...

Hio shule ada yake tu unaweza kula mwaka mzima ,kununua pepar wizaran kupitia kwa mamuruki ni kitu rahisi Sana .....mbaya zaidi wafanyakazi wengi wa serikali dawa yao ni pesa ,kwa million 20 anakuletea pepar la necta lotee mwezi mmoja kabla .....


Niamaini Mimi haya nayoyasema
hiyo ni kabisa hakuna mkate mgumu mbele ya hela halafu uwe na swaiba wako jikoni
 
Duniani kote kuna shule za serikali na private za vipaji maalumu ambazo huchukua the best only kujiunga nazo

Mfano kwa Tanzania vipaji maalumu ziko kama Mzumbe sekondari, tabora boys, kibaha sekondari nk huko hupelekwa vipanga waliofaulu hasa mitihani yao

Private pia kuna shule za watoto vipaji maalumu wenye ufaulu mkubwa kujiunga ndizo kama hizo St Francis nk usishangae hilo liko pote duniani

Hata vyuo vikuu kuna ambavyo huchukua vipanga tu asikikia kubwa kwa Tanzania ni UDSM na Muhimbili
Naomba urudie kusoma swali langu alafu uje tena kuangalia ulichojibu utaona kwamba ulichojibu haujajibu swali langu bali kuweka mambo ambayo ni public knowledge...

By the way hizo Tabora Boys na Mzumbe hazifukuzi watu wala kuchuja..., Binafsi nilisoma Tabora Boys na ninakwambia kuna watu walisoma PCM hawakuwahi kupata mwalimu wa Pure hata siku moja..., Chemistry miaka miwili labda mwalimu aliingia mara kumi... alikuwepo mwalimu wa physics yeye anatoa summary baada ya miezi sita ashamaliza syllabus mpaka za form six....; ila watu walipiga point tatu.... na tofauti na kina Mzumbe huko Tabora wala Paper halifiki (kuvuja) tofauti na miji mingine....

Now back to the topic at hand..., Ukichukua Crème de la Crème, alafu ukawafundisha alafu wakawa wasongo..., alafu paper kulenga ni rahisi sana wewe cheza na past papers tu maswali yatatoka humo humo..., kwahio watu kupata point tatu au saba wala sio ajabu tena....

Narudia tena my main point kwangu mimi shule zinazofundisha ni zile zinazochukua average students maybe F students wakati wanaingia kwahio wanafunzi hawa hata mwisho wa siku wakipata C au D that is job well done....
 
Maambukizi yamefika mpaka kwenye damu kutoka kwenye source nyingine ambayo huenda ikawa ni skin, respiratory, urinary tract nk.

Sasa yakishafika kwenye damu wana term hivyo Septicemia .
Septicemia sawa maana ni maambukizi ya bacteria kwenye mfumo wa damu ila ukimwambia mtu una maambukizi tu bila ku specify ni maambukizi ya aina Gani SI sawa unakuwa huna tofauti na wale jamaa wa herbal clinic anamsambia mgonjwa
DX ; Stress
Treatment; Apunguze mafuta ale mboga mboga na matunda na hapo keshakufanyisha kipimo Cha mwili mzima bill inakuja laki 350.
 
Huyo daktari yupo sahihi.

Huenda huyo rafiki yako ana infections kwenye damu ambayo kitaalami wanaita Septicemia.
Daktari alivyomueleza mgonjwa alikuwa sahihi, mgonjwa alivyoelewa sio. Kuna ugonjwa unaitwa malaria ila hakuna ugonjwa unaitwa "infections".

Mtu anakuwa na infections ila hawi na ugonjwa wa infections.
 
Back
Top Bottom