[QUOTE="Paprika
Mama alikua hanipi hela ya kutumia (walikua hawatuzoeshi kushika pesa kabisa). Atanipikia vitu na kuniwekea kwenye lunch box na water bottle ya kamba.[/QUOTE]
Mimi hela nilikuwa napewa, maana sikuwa napikiwa na kupewa chakula kwenda nacho shule. Hata hivyo, nilianza kupewa sh.20 ile ya duara ile inafanana na sh.10. Hapo ni darasa la kwanza, mpaka la tatu.
Hiyo Sh.20 nilinunua ice cleam moja, na muhogo/andazi/kitu
mbua,n.k.....
Kuanzia la darasa la nne mpaka darasa la sita hela ya matumizi ikapanda, ikawa sh.50(hapo napata ice cleam moja na maandaz mawili saa nne, na mapumziko ya mchana napata ice cleam moja na andazi moja)
Darasa la saba ndo salio likapanda, nikawa napewa sh 100. Hapo sasa ni mwendo wa ubwabwa wa sh.50, saa nne asubuh, na saa 6:30 mchana.
Kipindi hiko hatukuzoeshwa kupewa hela, na hata ukipewa unapewa kidogo, na sio mara zote. Lakini tulikuwa tunaridhika, na maisha yakaenda. Na tulikuwa tunapendana sana, nakumbuka kwa wale wasio nacho tulikuwa tunawapunguzia ice cleam, tunagawana maandazi, tunachoteana ubwabwa, n.k
Maisha yalikuwa mazur sana, na tuliishi kwa umoja sehemu kubwa.
Yote ya yote, kubwa kuliko ilikuwa ile siku ya kumaliza mtihani wa mwisho, wa kuhitimu elimu ya msingi, hususani kwenye suala la menu, hapa watu walibeba mapocho pocho ya maana, wali, pilau, ugali, kuku, ndondo, n.k na tulishirikiana kula pamoja...unakuta mtu kaja na pilipili mfuko mzima(ile ya kaki ile inayotokana na mifuko ya saruji ya enzi zile) hafu anaweka yte kwenye wali wake wa ndondo ulioungwa kwa nazi ili ale peke yake, lkn watu tuliunga tela na kula huku tukitokwa na machozi. Acha kabisa!!!Kitu cha wali ndondo kilihusudiwa kuliko wali nyama.
Acha tu, "kila ufalme na zama zake" yale maisha tuliyafurahia sana.... Ndo hivyo wakati ni moshi, ukishatoka haurudi! Ila yale yalikuwa maisha ya upendo sana