Stand up comedy: Kenya kuna Eric Omondi, Uganda kuna Kansiime na Bongo kuna nani?


Duh hawaoni aibu kucopy na kukubali hawana kipaji bali wanalazimisha...kweli inaboa na kupoteza mashabiki kwa mtu kama amekutana na hiyo ya kukopi...tena miaka hii.
 
Nimejaribu kucheki stand up comedy za idris sultan..jamaa is a fake, hachekeshi ata kidogo.
 
Tusiwalaumu sana Kuna wengine wazuri kama joti, mpoki ila tatizo lugha ya kingereza na Kuna wengine wanajua lugha ila hawajui kuchekesha kama mc pilipili, evance na idris nikiwatizamaga hata sioni wanachochekesha.

Umemaliza lugha ndio tatizo... Kutoa kichekesho chake kwenye Kiswahili kiende kwa kingereza hapo ndio majanga
 
Honestly, mimi hata huyo eric omondi huwa hanichekeshi....Kansiime clip zake chache zinachekesha.....Kibongo bongo Kitale (Mkude Simba) huwa anajitahidi sana...Japo sidhani kama stand up anaziweza
 
Stand up comedy ni kitu cha tofauti. Ukifanikiwa kuigiza movie yenye vichekesho haimaanishi utakuwa vizuri kwenye stand up comedy.

Stand up comedy inataka uwe na uwezo wa kubadilisha materials ukiwa stejini hivyo inahitaji kipaji haswa as hakuna cha editing pale.

Unaweza enda kuchekesha watu mahali ukakuta materials zako zote haziko relevant kwa audience uliyokutana nayo na hili unalitambua unapokuwa jukwaani hivyo kupaswa ku-switch ghafla. Ndio maana wataalamu wanakwambia stand up comedy ni ngumu sana. Siyo ya kuamka na kusema mimi ni stand up comedian.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…