Starlink internet sasa yaingia Zambia, Wazambia sasa kupata internet ya kasi isiyo na kikomo


Sasa wambia kufuruhikia internet ya satellite hata ukiwa mashambani...Tanzania,Congo,Uganda tunajifikiria bado. walipofikia Kenya vitu vinashuka sisi bado tuko na bando zakupimiana GB.Mkonga wa taifa mixer 5G kuna watu hawataki ushindani.
 
Hii kitu ni nzuri,lkn kwa usalama wa taifa sio poa kabisa.
Marekani wanatumia Paypal mpk bitcon kama njia ya kununua na kuuza bidhaa.

Bunduki, Marekani zinauzwa kwenye maduka km bidhaa zingine, ukifikisha miaka 18 unaenda kununua bunduki.
Nguo zinazofanana na sare za jeshi, zinauzwa marekani mitaani lkn bado ni taifa lenye nguvu na uchumi mkubwa.

Tanzania ambayo hakuna kutumia paypal, wala bitcon wala bunduki haziuzwi na kuna rasilimali nyingi lkn bado ni nchi masikini sana. Tangu 1961 bado serikali inahangaika na matundu ya choo, maji masafi, afya na umeme. Leo umeme ni wa mgao

Huo usalama wa taifa sijui ndiyo nini? Bongo bahati mbaya
 
Binafsi nampinga Nape kufanya gharama za internet kuwa ghali sana nchini Tanzania. Huko Zambia hata hao Starlink wasipokuwepo bado makampuni yaliyopo yanauza bundle bei rahisi sana. Nilienda Tunduma nikaona mitandao ya Zambia wanauza 2Gb kwa kwacha 10 kama Tsh 1170/=..
 
Kwahiyo unataka na sisi tuwe tunauziana bunduki? Una hoja nzuri ila umetoa mifano ya hovyo sana.
 
Broadband ni tofauti na hizi mobile data, nchi nyingi duniani Mobile data ni Ghali, Hata uuziwe GB 5 kwa 1000 still kwa dunia ya leo utajibana Bana hata Full HD hutaangalia.

Cha muhimu pigeni kelele Fiber, 5G, Copper, hizo low orbit satelite na tech nyengine za kupata unlimited internet zisambae, bando za simu sio suluhisho.
 
Nape ametunyima hii fursa, najua Rostam ndiye kinara wa hili ili afaidi na Tigo lake.
Nape amehongwa si bure
 
Kwahiyo unataka na sisi tuwe tunauziana bunduki? Una hoja nzuri ila umetoa mifano ya hovyo sana.
Uelewa wako ni mdogo sana kama jina lako.
Umeizidi nini USA zaidi ya kuwa masikini tu?
Huwezi kupokea pesa kwa Paypal na bado tangu 1961 mnahangaika na matundu ya choo kwa shule za msingi na sekondari.
Dunia ya sasa Internet ni anasa kwa nchi ya Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…