Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Chaneli za ndani ya nchi zinalipiwa siku hizi?? Maana kisimbusi changu kinaonyesha chaneli mbili tu Tbc 1 na Tv 1.. chaneli zingine zinadai nilipie ili nione.. nikaongea na huduma kwa wateja nikaambiwa kuwa baadhi ya visimbusi inabidi chaneli za ndani zinalipiwa.. swali kwenu.. je serikali imebadili sheria ya mawasiliano hasa kwa chaneli za ndani au ni nyinyi wenyewe mmeamua kuchukua pesa zetu kimya kimya?

Na kama kuna mabadiliko ya sheria mbona hatujatangaziwa? Pia hizo Tbc 1 na Tv 1 zenyewe hazistahili kulipiwa?? Au hizo pekee ndio chaneli za ndani ya nchi?

Namba ya kisimbusi ni 01 81 90 21 787.. nipo mtoni kijichi..
 
kisimbuzi changu kinagoma kuwaka kila saa kinaleta ujumbe wa OTA Download, hakiendelei kufanya kazi kama kawaida yake, nipo morotown, nifanyeje?

Nambari ya smart card yangu ni 02035480511
 
Habari star times......

Maeneo ya mtwara m'meshafika......je mnapatikanaje ?!

Maaana naona ni azam tu ndio wapo nyie hamuonekani hata kidogo......
 
tatizo langu king'amuzi changu kinasema no signal sasa ni kama miezi miwili sijaona msbadiliko naomba msaada maana namisi sana habari
 
 
 
naomba kufanyiwa activation ya Huduma, Niko Rombo mkoani Kilimanjaro namba ya kadi yangu ni 01819374635
 
Yaani mnaboa mpaka...niwaza azam sasa hivi.....inakuwaje mitambo ipo kisarawe gongo la mboto signal iwe dhaifu.....???
 
startimes. Mjirekebishe na uroho wa fedha, utawapotezea wateja wengi sana.

Bei za vifurushi ni kubwa mno na chanel zenu siyo nzuri sana kulingana na ualisia wa bei ya malipo ya kifurushi husika.

Pia kumlazimu mteja kulipia elf 6 ili aweze kufunguliwa huduma pia itawapotezea ela maana watu wengine walikuwa wanalipia hata buku kuona kile anachotaka kuona kwa siku husika. Hivyo kwa kumpangia kiwango mtawapoteza watu wengi.
 
Hello startimes mimi nipo Mwanza lakini Clouds Tv haionekani lakin kwenye vipeperushi inaonyesha kuwa ipo lakin haionekan. Nina king'amuzi cha antena na ninatumia kifurushi cha Mambo
Kwakuwa aliyeanzisha hii thread kazi imemshinda wacha nimsaidie majukumu.

Mwanza huwezi kupata clouds tv mpaka utumie Antena ya juu na siyo ile ya ndani.
 
Naomba kujua, kwa kifurushi kipi cha chini, ambacho nitapata local Chanel tu?
Kwa mujibu wa maelezo ya Tcra, local chanel sio bure?
 
Tena nyie startimes nataka kuwahama sababu ni wezi nimelipa mwezi mmoja haujaisha mmeniwekea kibahasha kesho mnakata.
 
Hamjibu maswali.

Kwa nini azam hawapo kwenye list lkn wao tv zenu zipo kwenye list yao?
 
Startimes acheni ubabaishaji. mbona channel nyingi hazionekani hata baada ya kulipia vifurushi? Halafu namba zenu za huduma kwa wateja hampokei na hata katika kurasa zenu za mitandao ya kijamii hamjibu maswali.

Kuna nini kimejificha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…