Step 10: Nilivyowekeza laki moja hadi kuanza kutengeneza milioni moja kila siku 3 (step by step)

Mkuu Michael Mkwanzania natakajua bei ya hilo lijisaa la ukutani lenye miji herufi mikubwa.

Ndugu zanguni jaribu fursa hiyo maana wateja tumo hata humu, kunabwana huko unguja huwa anaposti hapa JF kuwa anauza mi TV akaweka na namba yake, nikampigia nikamwambia aina nitakayo akanambia bei, nikamtumia pesa nikamwambia mtu wa logistic huko unguja akampatia mzigo, ukatiwa kwa ndege nikaupata arusha, ilichukua masaa matatu tu toka kulipa hadi kupokea mzigo, ktoka unguja to arusha.
 
Salute Mkuu.. ila changamoto Ipo Kwenye Bidhaa Kuchelewa Kufika Mimi Kuna Bidhaa Naagiza Ila Imeshachukua miezi Miwili... Kenya Wanaiba Sana Mizigo
Mimi sijawahi kuibiwa mzigo hata siku moja, mizigo ikiwa na a proper tracking number haipotei kirahisi. Ila kuna mtu nilikutana nae posta pale aliibiwa simu, mtu wa posta pale akamwambia imepotelea kenya (nmeagiza simu kupitia posta, nimezipata zote zingine zimepitia kenya), ila kwa kuwa mizigo inayopitia kenya pia hua inachelewa sana, inabidi ujue postal service ipi inapitia kenya ili u avoid, Post NL(netherland post) inapitia kenya, supplier akiniambia antuma kwa post NL huwa namuomba achagua kwingine ikishindikana kabisa ndo nakubali... Singapore post haipitii kenya, hongkong post na china post hazipitii kenya. So kama unahofia mizigo kupotea kenya, fuatilia ni post gani wanatumia na fanya research kama inapitia huko na omba supplier abadili njia ya kutuma, hauhitaji DHL wala nini kwa mizigo midogo.
 

Saa zote zina bei tofauti, tafadhali bonyeza hapa uingie kwenye page ya facebook upitie na kuweka order kupitia namba iliyopo pale, bei zinaanzia 49,000 hadi 75,000..
 
Mkuu asendia kwenys shipping huwa mzigo unapitia wap
 
Nishajaribu hii kitu ila napata challenge kubwa mzigo ukiagiza unachukua muda mrefu kufika hadi inaboa sometimes had zaidi ya siku 50
 
Sawa lakin Vp kuhusu muda shipping maana ukiingia let say alibaba wao unakuta wanasema shipping 23 had 40 days . sasa unafanya Vp kupata mzigo kwa wakat mfupi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…