Kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke? Ikiwa Yehova Mungu ana nguvu zote, ana upendo, hekima, na haki, kwa nini ulimwengu umejaa chuki na ukosefu wa haki?
Biblia hueleza hivi waziwazi: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” Unapofikiria hilo. Ulimwengu unaonyesha utu wa kiumbe huyo wa roho asiyeonekana, “anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa. Shetani ana chuki, ni mwongo, na mkatili. Kwa hiyo, ulimwengu ulio chini yake umejaa chuki, uwongo, na ukatili. Hiyo ni sababu moja inayowafanya wanadamu wateseke sana leo.
Sababu ya pili ni kwamba wanadamu si wakamilifu nao wamekuwa watenda-dhambi tangu uasi ulipoanza katika bustani ya Edeni. Wanadamu wenye dhambi hung’ang’ania utawala, na hilo hutokeza vita, ukandamizaji, na kuteseka.
Sababu ya tatu ni “wakati na tukio lisilotazamiwa.” Waswahili wanaita "Bahati mbaya". Katika ulimwengu usiotawaliwa na Mungu (kulingana na Biblia ulimwengu kwa sasa unatawaliwa na shetani) , watu wanaweza kuteseka kwa sababu ya kuwa mahali pasipofaa wakati usiofaa.