Stephen Hawking's Final Book Says There's 'No Possibility' of God in Our Universe

Sasa sayansi imefanya nini hebu toa jibu moja ueleweke.
 
Siwezi kuwa nimemaliza kama hujanijibu hata kama ngwe ya kwanza umeielewa au hujaielewa.

Sijaelewa bado_Naona unanikanganyia habari

kuwa complex kwa nanasi kuna fanana vipi na kuwa complex kwa Mungu....!?

Nanasi mimi nimelikuta sijaliunda ninapohitaji huduma yake kwa wingi nalipanda linajikuza lenyewe katika ubora wake

Mungu kwa mlinganisho wako uliofananisha na nanasi inakuwaje...!? sielewi

Kwamba anapandika kama nanasi au ni mtamu kama nanasi_sijaelewa
 
Suala la kusema Mungu huyo hayupo ndio unashindwa kueleza ni vp iwe hayupo? Hilo jibu la hayupo linapatikanaje hapo?
 
Nani aliwahi kusema kuwa Mungu kaumbwa hadi uniulize kaumbwa na nani? Ndio maana nimeuliza kipi kinafanya ufikiri Mungu kaumbwa?


Ndio maana tunakuambia hakuna mungu

Suala la mungu linatakiwa libaki kama neno linaloekezea the whole universal na si mungu wa kutungwa wa warabu na wayahudi
 
Ndio maana tunakuambia hakuna mungu

Suala la mungu linatakiwa libaki kama neno linaloekezea the whole universal na si mungu wa kutungwa wa warabu na wayahudi
Mbona umewataja waarabu na wayahudi tu ina maana hapa duniani wanaoamini Mungu ni hao tu?
 
Mbona umewataja waarabu na wayahudi tu ina maana hapa duniani wanaoamini Mungu ni hao tu?

Warabu na wayahudi wao ndio wanadai kuwa dunia imeumbwa na mungu wao

Lakini wengine wao hata hawana habari ya kufanya dunia kuwa imeumbwa na mungu wao

Mfano mungu kama Zeus marduku Ra-ammon budha wao wapo kimya ndio maana sikuwataja

Jina mungu libaki kuwa univrsal na si kama yupo kweli
 
Suala la kusema Mungu huyo hayupo ndio unashindwa kueleza ni vp iwe hayupo? Hilo jibu la hayupo linapatikanaje hapo?
Mungu mjuzi qa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote angekuwepo, ulimwengu usingeweza kuwa na mabaya, mabaya yana contradict Mungu huyo kuwepo.

Huwezi kuwa na ulimwengu ambao mabaya yanawezekana, na Mungu huyo pia yupo. Hiyo ni contradiction kama mtoto aliyezaliwa na mama kuwa mama mzazi wa mama yake mwenyewe.

Ni kitu cha kufikirika. Hakiwezekani kwenye uhalisia.

Mabaya yanawezekana kuwepo.

Hivyo, Mungu huyo hayupo.
 
Unakubali nanasi liko complex?
 
Kwahiyo kumbe tatizo lako ni kuumbwa dunia na si madai ya kuwepo Mungu?
 
Kwanini iwe Mungu ndio hayupo na isiwe vinginevyo?kama kuna contradiction kwanini majibu ya hiyo contradiction yawe hakuna Mungu?
 
Kwanini iwe Mungu ndio hayupo na isiwe vinginevyo?kama kuna contradiction kwanini majibu ya hiyo contradiction yawe hakuna Mungu?
Kwa sababu, ukifuata logic, vitu viwili vilivyo "mutually exclusive" haviwezi kuwepo vyote pamoja.

Na usipofuafa logic, hutaweza hata kuuliza swali lako, kwa sababu swali lako lenyewe linafuata logic.
 
Kwa sababu, ukifuata logic, vitu viwili vilivyo "mutually exclusive" haviwezi kuwepo vyote pamoja.

Na usipofuafa logic, hutaweza hata kuuliza swali lako, kwa sababu swali lako lenyewe linafuata logic.
Sawa haviwezi kusawa vyote kwa pamoja,hoja yangu hilo jibu la kuwa hakuna Mungu umelipata vp?

Kwanini isiwe kuwa sifa ya upendo ambayo tunaambiwa anayo Mungu si kweli na ndiyo maana imetokea hiyo contradiction au kwamba Mungu huyo hajaumba huu ulimwengu ndio maana kuna contradictions.
 
Ukishaongelea habari ya sifa ya upendo si kweli, umekubali kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujui wote na upendo wote hayupo, ni hadithi tu, kitu ninachosema.

Umekubali kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo na ni hadithi tu?
 
Ukishaongelea habari ya sifa ya upendo si kweli, umekubali kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujui wote na upendo wote hayupo, ni hadithi tu, kitu ninachosema.

Umekubali kwamba Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo na ni hadithi tu?
Nimekuuliza swali na nikatoa hiyo mifano,jibu swali kwamba hilo jibu la kuwa hakuna Mungu umelipata vp kwanini isiwe tofauti?
 
Naongelea Mungu gani?
Mungu ambaye tunaambiwa ana upendo wote ujuzi wote na uwezo wote,ambaye wewe unapinga madai yanayosema kwamba Mungu huyu kaumba huu ulimwengu,unasema kwamba inakuwa contradiction.
 
Ukiwa na mwaka mmoja tarehe 6 December SAA 8 na nusu unajua ulikuwa wapi?
Mimi siwezi nikajitambua niko wapi katika umri wa mwaka mmoja, ila mzazi wangu ndio anaweza akajua kwasababu yeye ni mtu mzima

Kwaiyo unataka kusema mungu alikua na mwaka mmoja hivyo hakuweza kujitambua alikua wapi?
 
Jibu swali acha longo longo
 
Jibu swali acha longo longo
Katika hizi mada mara zote nyie mmekuwa mkiuliza maswali tu na kutaka kujibiwa ila nyie hamuulizwi maswali,hali hii inawafanya hata nyie mshindwe kujua udhaifu wa msimamo mlionao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…