Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Bara, Stephen Wasira, amemjibu Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche, kuhusu hoja ya umri wake, akisisitiza kuwa uwezo wa mtu hautokani na miaka aliyoishi bali akili alizonazo.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mkoani Geita leo Januari 29, 2025, Wasira amesema umri wake hauathiri uwezo wake wa kufikiri wala kufanya maamuzi sahihi.
"Mimi nina umri mkubwa lakini akili ni za miaka 55. Heche (John) akitaka akaulize madaktari wa India na Muhimbili, wamesema nina akili safi kabisa. Gari ni injini, siyo bodi," alisema Wasira huku akiwataka wapinzani wake kuzingatia hoja badala ya umri wake.
Wasira ametoa mfano wa Donald Trump, ambaye amechaguliwa kuwa Rais wa Marekani katika uchaguzi wa hivi karibuni, akisema kuwa licha ya umri wake mkubwa, Wamarekani walimchagua kwa sababu ya sera zake na si kwa kuangalia umri wake.
"Heche akitaka ushahidi aende Marekani akawaulize Wamarekani kwanini walimchagua Donald Trump mwenye umri kama wangu na wakamuacha Kamala Harris mwenye miaka 60," alisisitiza Wasira.
Kauli hiyo imekuja muda mchache baada ya John Heche, akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye makao makuu ya CHADEMA, kudai kuwa Wasira amekaa serikalini kwa muda mrefu na hawezi kuleta mawazo mapya kwa kizazi cha sasa chenye changamoto za ajira.
"Nimemuona Mzee Wasira amekuwa serikalini tangu akiwa na miaka 20, mimi sijazaliwa… Wasira hawezi kuja na mawazo mapya kwa watu wamemaliza vyuo vikuu na hawana ajira," alisema Heche.
Chanzo cha maandishi haya au andiko hili ni kutoka Jambo Tv Online. Mimi Mwashambwa Sijaweka neno langu hata moja.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara mkoani Geita leo Januari 29, 2025, Wasira amesema umri wake hauathiri uwezo wake wa kufikiri wala kufanya maamuzi sahihi.
"Mimi nina umri mkubwa lakini akili ni za miaka 55. Heche (John) akitaka akaulize madaktari wa India na Muhimbili, wamesema nina akili safi kabisa. Gari ni injini, siyo bodi," alisema Wasira huku akiwataka wapinzani wake kuzingatia hoja badala ya umri wake.
Wasira ametoa mfano wa Donald Trump, ambaye amechaguliwa kuwa Rais wa Marekani katika uchaguzi wa hivi karibuni, akisema kuwa licha ya umri wake mkubwa, Wamarekani walimchagua kwa sababu ya sera zake na si kwa kuangalia umri wake.
"Heche akitaka ushahidi aende Marekani akawaulize Wamarekani kwanini walimchagua Donald Trump mwenye umri kama wangu na wakamuacha Kamala Harris mwenye miaka 60," alisisitiza Wasira.
Kauli hiyo imekuja muda mchache baada ya John Heche, akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye makao makuu ya CHADEMA, kudai kuwa Wasira amekaa serikalini kwa muda mrefu na hawezi kuleta mawazo mapya kwa kizazi cha sasa chenye changamoto za ajira.
"Nimemuona Mzee Wasira amekuwa serikalini tangu akiwa na miaka 20, mimi sijazaliwa… Wasira hawezi kuja na mawazo mapya kwa watu wamemaliza vyuo vikuu na hawana ajira," alisema Heche.
Chanzo cha maandishi haya au andiko hili ni kutoka Jambo Tv Online. Mimi Mwashambwa Sijaweka neno langu hata moja.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.