Uchaguzi 2020 Steven Wassira atangaza kugombea ubunge Jimbo la Bunda, Adai 2015 aliibiwa kura

Hawa wazee wawaachie vijana nao wapate uzoefu. Binafsi sitajali ni kijana wa ccm au chama cha upinzani, lakini sio hawa wazee. Tunawaheshimu sana, lakini watupishe! Wabakie kushauri tu.
 
Siyo dalili njema hii.Kwanza kakamia sana.Pili ana hasira/mihemuko ya 2015...Nakumbuka huo mchuano,kuanzia Kwenye media mpaka uwanjani na kwinginiko.Pili.alishitukizwa kama vile.

Sipati picha,akikatwa safari hii.....
 
Hiyo haina mashaka lkn je kwa umri wa huyo mzee wetu ana uwezekano wa kumsomesha hadi mtoto huyo ambaye leo ananyonya akamaliza chuo?

Lifespan yetu Waafrika ipo chini sana mkuu
Mwisho unapata dementia mtoto haelewi ni nini.
 
Duu!! Kwa umri ule bado ana watoto wananyonya!!!! Labda wanamsingizia
Tatizo la Wasira ni njaa, kale ka pensheni kake anaona hakamtoshi maana nasikia ana watoto hadi sasa wengine bado wananyonya.

Sasa kwa umri ule alio nao atawasomeshaje hao vichekechea?
 
Wassira amehudumu tangu serikali ya Nyerere, kama Nyerere aliamua kustaafu uongozi na siasa na kwenda kulima butiama, kwake yeye kuna tatizo gani..
 
Shikamoo !!

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Tangu miaka ya 1970 mpaka leo 2020 mzee bado anang'ang'ana tu!

Mhhhhh! Hii kali!
 


Raid Magufuli anaondoka madarakani Wassira anabaki....YUPO!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…