Stiegler’s Gorge yaanza kwa kasi

Stiegler’s Gorge yaanza kwa kasi

esther mashiker

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
616
Reaction score
552
1129610


WAZIRI wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 2,115 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Ru ji (Stiegler’s Gorge) umean- za kwa kasi kubwa. Amesema mradi huo unaotekelezwa na Kampuni ya ubia ya Arab Contractors na Elsewedy Electric za Misri umeanza kwa kasi baada ya vifaa vyote husika kukishwa eneo la mradi.

Waziri Kalemani alisema hayo juzi baada ya kutembelea ujenzi wa mradi huo mkubwa na kujionea jinsi ulivyoanza kwa kasi kwa vifaa vyote atakavyotumia mkandarasi wa ujenzi kuwasili.

“Kila kitu kipo eneo la mradi na hatua ya ujenzi inaendelea na umeanza kwa kasi, wakandarasi wapo eneo la mradi na wasimamizi ambao ni wazawa...kulingana na matayarisho ya mkandarasi alivyonipitisha hatua ya ujenzi sasa zinaenda kutekelezwa kwa vile mabuldoza na matingatinga na magari yapo eneo la mradi, na kazi hii itakamilika kama ilivyopangwa Juni mwaka 2022,” alisema.

Waziri Kalemani alisema wakandarasi walio eneo la mradi wanasema hawana vikwazo na wanaendelea na ujenzi wa mradi huo. Aliitaka kampuni ya ubia inayojenga mradi huo kutoa kipaumbele cha kutumia wataalamu wa ndani wenye uwezo katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa mradi huo mkubwa nchini.

Aliwataka wakandarasi wanao- jenga kingo ya kuzuia maji katika mradi huo wa aina yake nchini kujenga kwa kutumia muda mfupi ili waweze kumaliza ujenzi huo na kuendelea na hatua nyingine za ujenzi huo. “Ujenzi wa kingo ya kuzuia maji mkandarasi alipanga kutumia miezi 12 lakini tumemwomba ajenge ndani ya miezi tisa au 10 ili kutoa fursa ya kuendelea na kazi nyingine kwani wafanya kazi 420,” alisema.

Pamoja na hayo, Waziri Kale- mani aliwaagiza wakandarasi wa kampuni inayojenga mradi huo kutumia vifaa vya ujenzi ambavyo vinapatikana ndani ya nchi isipokuwa vile visipopatikana hapa nchini.

“Hili ninarudia wakanda- rasi wa mradi hakikisheni vile vifaa vya ujenzi vinavyopatikana nchini kama nondo, saruji na bati isipokuwa ambavyo havipatikani kulinda viwanda vya ndani,” alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo aliwataka vijana kujitokeza kupata ajira katika mradi huo na wawe waaminifu wakati wa ujenzi wa mradi huo. “Miradi mingi mikubwa inayoendelea kumejitokeza wizi wa vifaa na mafuta unaofanywa na Watanzania wasio waaminifu,” alisema Chonjo na kuongeza vijana 400 waliojiunga na jeshi la akiba ndio watapewa kipaumbele katika mradi huo ili wawe ni walinzi kuona mradi hauhujumiwi kwa namna yoyote ile,” alisema.

Mkataba wa mradi huo uliosainiwa Desemba mwaka 2018, ni wa Sh trilioni 6.5 na utatekelezwa kwa miezi 36 kupitia Kampuni ya ubia ya Arab Contractors na Elsewedy Electric kutoka nchini Misri. Katika kuhakikisha mradi huo unapewa msukumo mkubwa, Oktoba 4, mwaka 2018, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alitembelea na kukagua maendeleo ya mradi na alimtaka kila mmoja aliyepewa jukumu la kusimamia mradi huo ahakikishe anawajibika kikamilifu ili mradi huo ufanikiwe.
 
May 21, 2018
Kilombero, Morogoro

Mradi mdogo wa umeme katika mkoa wa Morogoro wa umeme unaozalisha kwa kutumia maporomoko ya maji katika Kijiji cha Mbingu huko Tanzania unahudumia Zaidi ya watu 300,000. Awali mradi huo mdogo wa umeme ulikuwa unaendeshwa kwa kutumia jenereta inatotumia mafuta na ulikuwa ghali sana kuendesha. Hata hivyo kutokana na kuwepo kwa maporomoko wa maji mradi wa umeme ukabadilishwa toka kutumia mafuta na kuendeshwa kwa maporomoko ya maji na kuufanya mradi ulio nafuu Zaidi kuuendesha na kuhudumia shughuli mbalaimbali za kijamii kama matumizi hospitalini, mashuleni na majumbani.



Hydro Power for the Development of a Community in Mbingu Village
 
Sisi yetu macho kwsa maana sifa kubwa ya watanzania wa leo, ni kusifia kila kitu, kila wakati, na hasa kwa mapenzi makubwa kisiasa. Time will tell...kila kitu kimefika kwenye eneo la mradi....!!!
View attachment 1129610

WAZIRI wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa megawati 2,115 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Ru ji (Stiegler’s Gorge) umean- za kwa kasi kubwa. Amesema mradi huo unaotekelezwa na Kampuni ya ubia ya Arab Contractors na Elsewedy Electric za Misri umeanza kwa kasi baada ya vifaa vyote husika kukishwa eneo la mradi.

Waziri Kalemani alisema hayo juzi baada ya kutembelea ujenzi wa mradi huo mkubwa na kujionea jinsi ulivyoanza kwa kasi kwa vifaa vyote atakavyotumia mkandarasi wa ujenzi kuwasili.

“Kila kitu kipo eneo la mradi na hatua ya ujenzi inaendelea na umeanza kwa kasi, wakandarasi wapo eneo la mradi na wasimamizi ambao ni wazawa...kulingana na matayarisho ya mkandarasi alivyonipitisha hatua ya ujenzi sasa zinaenda kutekelezwa kwa vile mabuldoza na matingatinga na magari yapo eneo la mradi, na kazi hii itakamilika kama ilivyopangwa Juni mwaka 2022,” alisema.

Waziri Kalemani alisema wakandarasi walio eneo la mradi wanasema hawana vikwazo na wanaendelea na ujenzi wa mradi huo. Aliitaka kampuni ya ubia inayojenga mradi huo kutoa kipaumbele cha kutumia wataalamu wa ndani wenye uwezo katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa mradi huo mkubwa nchini.

Aliwataka wakandarasi wanao- jenga kingo ya kuzuia maji katika mradi huo wa aina yake nchini kujenga kwa kutumia muda mfupi ili waweze kumaliza ujenzi huo na kuendelea na hatua nyingine za ujenzi huo. “Ujenzi wa kingo ya kuzuia maji mkandarasi alipanga kutumia miezi 12 lakini tumemwomba ajenge ndani ya miezi tisa au 10 ili kutoa fursa ya kuendelea na kazi nyingine kwani wafanya kazi 420,” alisema.

Pamoja na hayo, Waziri Kale- mani aliwaagiza wakandarasi wa kampuni inayojenga mradi huo kutumia vifaa vya ujenzi ambavyo vinapatikana ndani ya nchi isipokuwa vile visipopatikana hapa nchini.

“Hili ninarudia wakanda- rasi wa mradi hakikisheni vile vifaa vya ujenzi vinavyopatikana nchini kama nondo, saruji na bati isipokuwa ambavyo havipatikani kulinda viwanda vya ndani,” alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo aliwataka vijana kujitokeza kupata ajira katika mradi huo na wawe waaminifu wakati wa ujenzi wa mradi huo. “Miradi mingi mikubwa inayoendelea kumejitokeza wizi wa vifaa na mafuta unaofanywa na Watanzania wasio waaminifu,” alisema Chonjo na kuongeza vijana 400 waliojiunga na jeshi la akiba ndio watapewa kipaumbele katika mradi huo ili wawe ni walinzi kuona mradi hauhujumiwi kwa namna yoyote ile,” alisema.

Mkataba wa mradi huo uliosainiwa Desemba mwaka 2018, ni wa Sh trilioni 6.5 na utatekelezwa kwa miezi 36 kupitia Kampuni ya ubia ya Arab Contractors na Elsewedy Electric kutoka nchini Misri. Katika kuhakikisha mradi huo unapewa msukumo mkubwa, Oktoba 4, mwaka 2018, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alitembelea na kukagua maendeleo ya mradi na alimtaka kila mmoja aliyepewa jukumu la kusimamia mradi huo ahakikishe anawajibika kikamilifu ili mradi huo ufanikiwe.
 
Mradi wa umeme wa maporomoko madogo ya maji katika Kijiji cha Matembwe Njombe Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania. Matembwe Village Company limited ndiyo wamiliki wa mradi huo uliofunguliwa awamu ya kwanza mwaka 1986 na awamu ya pili ilifunguliwa mwaka 2016. Mradi huu wa umeme unamilikiwa na vijiji viwili na wananchi wenyewe na hivyo wanakijiji kuulinda na kuuenzi mradi walioubuni wenyewe .


Matembwe Village Southern Highlands of Tanzania mini Hydroelectric power
 
Tutapokuja ambiwa maji hayatoshi tena na umeme hauzalishwi baada ya muda mfupi tutawatapisha hela zote waliofosi mradi huu bila tathmini nzito ya mradi husika hasa utadumu muda gani. Utakuwa ni uhujumu uchumi
 
Tutapokuja ambiwa maji hayatoshi tena na umeme hauzalishwi baada ya muda mfupi tutawatapisha hela zote waliofosi mradi huu bila tathmini nzito ya mradi husika hasa utadumu muda gani. Utakuwa ni uhujumu uchumi
Yesu amwambia, ".......kaa kushoto shetani wee unawaza ya wanadamu sio ya Mungu...."
 
Nenda ukafanye kibarua cha kuchimba kifusi si kukesha hapa JF halafu unavizia vyakula misibani
Hah haha Haa huko misibani si ndio tunako onana mzee? Nakumbuka msiba wa juzi, umelia weeee eti marehemu alikuwa rafiki Yangu, hata gari anayotembelea ni Mimi nimemnunulia, kumbe amefariki mtoto wa Siku moja.
Hebu acha ufala
 
May 2, 2016
Wilaya ya Hai, Kilimanjaro

Kikuletwa Hydro power Station 17MW kiliacha kutoa umeme miaka 20 iliyopita lakini Chuo cha ATC kimechukua jukumu la kukifufua kituo hicho na uzalishaji wake utakuwa mkubwa kuliko Kituo Cha uzalishaji wa Umeme huko Nyumba ya Mungu Kilimanjaro http://www.tanesco.co.tz/index.php/nyumba-ya-mungu :


Chuo cha ufundi Arusha kimetambua kituo cha kuzalisha umeme wa maji cha Kikuletwa kama eneo linalofaa kwa ajili ya uanzishwaji wa kituo cha mafunzo ya nishati ya umeme utokanayo na maji. ATC iliiomba serikali kumilikishwa kituo cha kuzalisha umeme cha Kikuletwa kutoka TANESCO (mmiliki wa wakati huo). Serikali liilikubali ombi la ATC kwa msajili wa Hazina kuidhinisha kuhamisha mali zote za kituo cha kuzalisha umeme cha Kikuletwa kwa chuo cha cha ufundi Arusha mnamo Julai 2012. Kwa upande mwingine, TANESCO ilikabidhi mali na haki zote za kituo cha umeme cha Kikuletwa kwa ATC mwezi Aprili mwaka 2013. Serikali ya Norway imeshiriki katika kufanikisha mradi huo kama mdau wa maendeleo kusaidia chou hicho cha ATC kufanikiwa kufufua mradi na utunzaji wa mazingira ya mito kumi na saba inayowezesha kupatikana maji kuendesha mitambo hiyo ya umeme kwa kutumia maji .

  1. Kituo hiki cha Mafunzo kitatumika kama kitovu cha kuhudumia maendeleo ya sekta ya nishati ya umeme wa maji katika Tanzania. Katika uendelezaji wa kituo cha Kikuletwa shughuli zilizopangwa ni pamoja na:
  2. (i) Ukarabati na uendeshaji wa kituo cha kuzalisha umeme cha Kikuletwa,2MW
  3. (ii) Kuanzishwa kwa kituo kitakachohusika na mafunzo na utengenezaji wa mitambo midogo midogo ya kuzalisha umeme (iii) Uongezaji wa uwezo wa kuzalisha umeme kwa kuendeleza maeneo mapya ktk mto Kikuletwa (cascading),
  4. (iv) Kuhifadhi mazingira yaliopo
  5. (v) Kujenga uwezo na kuendeleza wafanyakazi katika kila hatua ya mradi.


Source: Arusha Technical College
 
May 2, 2016

Kijiji cha Chemsha ,
Kikuletwa Kilimanjaro Tanzania

Chuo cha Arusha chapanda Miti kwenye vyanzo vya Maji vya Kituo cha Kikuletwa Hydropower station ili kusaidia kudaka maji kwani wataalamu wanasema msitu unaozunguka mlima Kilimanjaro pekee yake hautoshi kudaka maji ili mradi wa umeme wa maji wa Kikuletwa uwe endelevu kwa miaka mingi bila kukosa maji.




Source: Arusha Technical College

Je tutarajie nini mradi wa Stiegler's Gorge ambao bado wataalamu wa ekolojia hawajajitokeza kuelezea watafanya mikakati gani kuhakikisha maji ktk bwawa tarajiwa litakalojengwa katika bonde la Rufiji kuzalisha umeme wa 2,000 MW halitapungukiwa na maji yanayotoka katika vyanzo vya mito mbalimbali inayomwaga maji katika mto Rufiji n.k.
 
Hizi mbwembwe za Arab contractors ni porojo tu mbona kama ingelikuwa kuna ukweli tungewekewa mavideo na mavideo huku viongozi na matumbo yao makubwa wakisifu na kuimba.
 
Hizi mbwembwe za Arab contractors ni porojo tu mbona kama ingelikuwa kuna ukweli tungewekewa mavideo na mavideo huku viongozi na matumbo yao makubwa wakisifu na kuimba.

Hata ukisoma habari yenyewe unapata shida kuamini. Maana kinachoitwa ni "kuanza mradi kwa kasi" ni kupelekwa mitambo eneo la mradi.
 
Hizi mbwembwe za Arab contractors ni porojo tu mbona kama ingelikuwa kuna ukweli tungewekewa mavideo na mavideo huku viongozi na matumbo yao makubwa wakisifu na kuimba.

Mkuu ni kweli mashaka yako na wengi wetu pia, maana hata mradi wa SGR reli mavideo video kibao na waandishi bila kuwasahau ma-celebrity wanaoneshwa live ktk TV wakiwa eneo la SGR reli kujionea ilipofikia lakini mradi huu wa Stiegler's Gorge ni usiri mwingi na eneo lenye limekuwa kama eneo nyeti la Area 51 Nevada USA.

Wananchi walipa kodi na walipa madeni ya Taifa ya mikopo kufanikisha mradi unaotajwa wana haki ya kujua nini kinaendelea labda baada ya kusoma maoni yetu hapa ofisi maalum ya mahusiano kwa umma mradi wa Umeme Bonde la Rufiji itakuwa kila wakati ikirusha mapicha picha na video kuona huu mradi mkubwa wa umeme Bonde la Rufiji (Stiegler's Gorge) unaendelea vipi.

Mfano habari motomoto za kipande cha SGR reli sehemu ya Vingunguti Kiembe Mbuzi Dar-es-Salaam, Tanzania


Source: TRC RELI TV
 
Mbona mambo moto moto kumbe karibia unaanza kutumika .Maana hiyo picha inaonyesha aslimia kama 98%
 
Kazi ya kujenga kingo za mto contractor anasema atatumia miezi 12 employer anamwambia tumia miezi 9, contractor akasema as you wish sir! Matokeo yake contractor akalipua lipua kazi ili akimbizane na mda wa miezi 9 badala ya 12.
 
Kama maendeleo ni moto, umeme waweza kuwa cheche”-me
 
Back
Top Bottom