Story gani katika kitabu cha dini yako unafikiri ni hadithi ya ngano tu?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Ngano ni hadithi fupi inayosimuliwa kwa kusudi la burudani na pia mafundisho. Ni mambo ambayo hayajawahi kutokea kuhalisia. Ukitafakari kwa kina utagundua sehemu kubwa ya dini nyingi zimejengwa katika msingi huu.

Story gani ujawahi kuiamini kama ni ya kweli na halisi katika kitabu cha dini yako?
 
Story ya Ester, bahati bukuku alitusimulia kupitia wimbo wake wa waraka,
Yaani kuanzia Wimbo unaanza unaweza kwenda sokoni kununua dagaa, unarudi unapika, unamalizia kusonga ugali ndio utasikia wimbo umefikia "ooh Ester aah kwa mahombi huku akisindikizwa na mioyo ya wayaudi" .


Du hapo tulipigwa.
 
Kwamba Mungu aliumba dunia na kila kilichomo (sawa) kisha akaumba mwanaume na kuumba mwanamke kwa kumtoa ubavu mmoja mwanaume (sawa).

Kisha hao wawili (Adam na Eva/Hawa) wakazaa watoto wawili (Kaini na Abeli) - (sawa).

Kisha Abeli akawa mfugaji na Kaini akawa mkulima (sawa). Lakini Mungu alipendezwa zaidi na sadaka za Abeli kuliko za Kaini (sawa). Kaini akamuua kaka yake kwa wivu (sawa).

Mungu akampa adhabu Kaini kwa kumfukuza bustanini awe anatanga tanga huku na huko duniani (sawa).

Kaini akamwambia Mungu kuwa akitangatanga watu atakaokutana nao watamuua (shida inaanza kuja hapa). Mungu akamwekea alama usoni ili walimwengu wasimuue (shida inaendelea). Kaini akaenda huko nchi ya Nodi mashariki mwa Eden.

Kisha kaini akalala na mkewe akamzaa mtoto aitwae Henoki. (Sio sawa).

Reference: Soma kitabu cha Mwanzo 4:1-17.

Hii story haija balance kabisa hasa hapo mwishoni. Kama Mungu aliumba Adam na Hawa na wakazaa watoto wawili tu ina maana duniani palikuwa na watu wanne tu. Je hao watu aliokuwa akiwaogopa Kaini ni akina nani? Je huyo mwanamke alielala na Kaini na kuzaa nae mtoto alitoka wapi?

Wataalamu hebu naomba mtusaidie hapa.
 
Daah
 
Kuna sura na mstari kwenye kitabu cha yohana mtakatifu, unasema kama biblia ingeandika kila kitu basi isingetosha wala kujaa, hivo naamini pia kuna watu waliokuwepo ambao hawakuongelewa ktk kipengele hicho cha Kain, huenda ikawa pia ni wale jamii ya wanefili ambao kwenye mwanzo wanatajwa tu lkn hawakuonglewa kwa undani sana
 

Swali Lina kuja awa nao wali kuwa na Mungu wao au ?
 
Kuna yule baharia alitaka kusababisha wenzake wafe kwa meli wakamtupa baharini akamezwa na samaki siku 3 halafu akatemwa kule alipotakiwa kwenda ambapo alikuwa hataki na aliagizwa na Mungu..🀣🀣

Haikutosha vipi kwa mose ati alitawanya bahari waisraeli wakapita!.. nilipopenda zaidi ati shetani alienda mbinguni kuongea na Mungu ili amjaribu yule msela aliepewa mapunye mwili mzima,utajiri wake ukapotea,familia yake ikafa! How can it be wengine wafe kisa kujaribiwa kwa mtu mmoja!!πŸ˜€

Vipi kuhusu Israel ati alipigana na malaika usiku kucha mwisho wa siku malaika akaamua amtengue nyonga yakobo..🀣 jamani kama ni kupima uwezo Mungu si anajua uwezo wa kila mtu Sasa vipi kutumiana malaika waje tupigane nao ngwara..??πŸ˜‚

Tuachane na yote ati Adam na Eva walipokula tunda Mungu alipokuja akaanza kuwauliza ati nani kawaambia wapo uchi baada ya kula tunda!.. wakati huohuo tunaambiwa Mungu anayajua yote mwanzo Hadi mwisho sasa alikasirika nini na wakati alikuwa anajua kila kitu!
Alimuumba shetani huku akijua ya kuwa atakuja msaliti..🀣 what a movie..??
 
Hahahhhhh
 

We jamaa mbingu utaishia kuisoma JF πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Vita vyetu siyo vya damu na nyama ilihali adui yangu anakuja kwa bunduki, binduki panga, mikuki na mishale aiseeeee.


Ok, nalikujua tangu tumboni mwa mama yako, mwanza hadi mwisho. Kwa hiyo sasa tumesha hukumiwa kabisa kabisa maana alishajua Mimi Machepele ntakuwa zangu mbinguni.

#NITARUDI
 
Vitabu vya dini ukitumia logic, HUTOBOI. Maana kuna vingine havimake sense kabisa. Kufika mbinguni kazi sana.

Kuna muda unasoma unaona kabisa hii chai sasa, hasa yule mwamba aliyemezwa na samaki siku 3. Kwamba alikuwa tumboni amekaa tu. Sijui anapumuaje huko tumboni.

Mungu kama unatusikia tusamehe tu baadhi yetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…