Kuna ndugu yangu alihamia nyumba flani iko tegeta wazo, wakati anahamia kuna mtu jirani alimfuata akamwambia we dada hiyo nyumba watu hawakai mwenye nayo ni balaa.
Yeye kwakuwa alikuwa kalipa kodi akaona hawezi acha kodi yake.
Siku ya kwanza kalala fresh asubuhi mwenye nyumba kaja ni mama flani wa kipemba.
Na alipokuja akanikuta nimekuja salimia, akawa anamuuliza huyo ndugu yangu. Vipi umelala vizuri bila tatizo. Akajibiwa ndiyo. Akarudia bila tatizo kabisa, akajibiwa ndio.
Ndugu yangu hakutafakari yale maswali, ila mimi niliyatafakari sana.
Nikawa najiuliza huyu mama alitegemea apatwe tatizo au.
Aliendelea kukaa na wakahamia wengine, wakawa wapangaji watatu.
Kilichowakuta hawawezi kusahau.