Story Za Kuchati Za Darasani

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,743
Reaction score
25,564


SIKU YA KWANZA

Mimi: Oya inakuwaje? Mbona leo umechelewa hivyo?
Anita: Usafiri ulikuwa shida kweli yaani, nilisubiri gari mpaka nikakoma, yalikuwa yakipita tu.
Mimi: Pole sana, kwa hiyo inakuwaje leo?
Anita: Nakusikiliza wewe tu, ukiniambia nije kwenu, nakuja, ukiniambia tuonane sehemu yoyote, nakuja.
Mimi: Kweli jamani?
Anita: Huamini?
Mimi: Mmmh! Aya, nitakujulisha, nasubiri ticha atoke klasi kwanza ili nichaji simu, nitakucheki, namba yako si ileile?
Anita: Ndiyo! Ileile, sijabadilisha.
Mimi: Poa...ila naona ticha anazingua sana aiseee...
Anita: Hata mimi naona hivyohivyo...kwanza imekuwaje mpaka kuanza kuchati na mimi, kitambo.
Mimi: Basi tu, nimemisi kuchati na wewe jamani!
Anita: Mh! Aya!
Hizo zilikuwa chatting fulani nilikuwa nachati na mrembo wa darasa anayeitwa Anita. Hatukuwa tukitumia simu, meseji zetu hizo tulikuwa tukiandikiana kwa kutumia vikaratasi, yaani mimi naandika, nampa mshikaji wangu aliyekuwa pembeni, anampa Anita, halafu ananijibu tena.
Yaani tulikuwa kama watoto ila ndiyo hivyo mambo yalikuwa yakisonga. Umeme ulizingua, ulikatika halafu simu haikuwa na chaji, ticha yupo klasi, so kuwasiliana tukawa tunawasiliana kwa vimeseji tu, siyo mimi peke yangu, yaani hata madenti wengine ilikuwa hivyohivyo, kwa kifupi, tulizoea kufanya hivyo.
Anita alikuwa manzi fulani hivi, mtoto mzuri, mtoto wa haja, alijazia kweli huku nyuma, macho yake yalikuwa mazitoooo...kulikuwa na mademu wengi kwa klasi, ila Anita, alikuwa babโ€™kubwa. Wanaume hapo klasi walimtaka sana, ila walipomwambia, mtoto akajishembeduashembedua, akawapiga masela vya mbavu hivyo wakaachana naye.
Anita alikuwa biashara nzuri sana, klasi, tulikuwa na katabia kamoja hivi, yaani anakuja mtu, tunamwambia demu fulani huwezi kumchukua, akisema anaweza, tunawekeana dau halafu anakwenda, tunampa muda, kama wiki mbili hivi awe amefanikiwa. Dau linategemea, labda laki moja kwa laki moja, halafu mtu anakwenda.
Sasa watu walishaliwa sana hela zao kwa Anita, kila mtu aliyetaka kula hela, anakwambia nenda kamchukue Anita, anakupa wiki mbili, ukichemka, basi umeliwa. Kalikuwa kamchezo fโ€™lani amazing, na nilishawala watu hela zao, waliniambia niende nikamchukue Rachel, wakanipa wiki mbili, yaani wiki moja tu, nilikuwa naye chumbani, nikawala hela yao.
Hawakuishia hapo, kuna mdada aliitwa Fatuma, wakabisha kwamba siwezi kumchukua eti kwa sababu Cosmas alimshindwa, Eduardo alimshindwa, nikawaambia tuweke hela, tukaweka, nikawala kwani ndani ya siku nne, Fatuma akawa oyaoya.
Sasa kaupinzani kalikuwa kwa huyu Anita, watu walichemka sana, walimfuata kwa mikwara lakini hawakufanikiwa, ikawa ukitaka kuliwa hela yako, sema unamfuata Anita, lazima uliwe kwani alikuwa mgumu mno mpaka watu kuhisi kwamba labda mtoto alikuwa silidi.
Mimi: Ila tatizo lako unazingua sana....
Anita: Nani? Mimi? Akuu..wala sizingui.
Mimi: Kwa hiyo leo uhakika?
Anita: Wewe tu.
Unajua Anita alikuwa mzinguaji sana, kukubaliana naye lilikuwa jambo dogo lakini kwenye utekelezaji ndiyo ilikuwa shughuli. Omari aliwahi kumfuata, mtoto akalegea, akamrembulia macho sana jamaa, akajipa uhakika kwamba atakula mzigo na hela zetu, kilichotokea, wiki mbili zikakatika, hakuna kitu.
Mimi si ndiyo mbishi wao, nikaona mbona simpo tu, yaani Anita anishinde? Ana nini? Kama niliwahi kuwachukua wengine, yeye atanishindaje? Nikapiga moyo konde, nikaweka dau la shilingi laki mbili, watu watano wakajitokeza, nao wakaweka laki mbilimbili, nikaona poa, nikapewa wiki mbili niwe nimemaliza, nikasema sawa.
Tukachati sana kwa vikaratasi, baada ya ticha kutoka, nikachaji simu harakaharaka ili baadaye nianze kuchati naye kwenye simu.
Ngoja nikwambie kitu, watu hawakunielewa, nilikuwa mjanja sana, watu walipokuwa wakimfuata, walimfuata waziwazi ili kututisha tulioweka dau, sasa walipokuwa wakishindwa, tulijua mapema kwamba walishindwa ila kwangu, nilitaka kumfuata kimyakimya, yaani ukifuatilia, hujui kama mimi na yeye tuilikuwa tunachati.
Mimi: Leo una ratiba gani?
Anita: Saa ngapi?
Mimi: Mbili usiku.
Anita: Mmh! Nitakuwa home tu, kuna kitu?
Mimi: Ndiyo! Nataka nikupeleke sehemu fulani hivi!
Anita: Wapi?
Mimi: Surpriseeee...
Anita: Sawa.
Mbele yangu niliona mafanikio kwa kudhani kwamba kila kitu kingekwenda poa. Nikajiona Sharukh Khan kwamba hakukuwa na demu yeyote ambaye angenikataa, mtoto alikubali kutoka nami out...kuna nini tena!
Kumbuka hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kwanza kabisa, tulipotoka chuo, nikaelekea nyumbani, sikutaka kuchati naye sana, nikamuweka kiporo kwanza. Watu walikuwa wakisikilizia tu, walisubiri siku 14 ziishe ili wachukue hela zao, si unajua Anita ndiye alikuwa mgumu wa darasa.
Ilipofika saa moja na nusu usiku, nikamcheki kwa simu, kwanza ikaita weeee, alipokuja kuipokea, swali la kwanza kuniuliza, eti โ€œWewe nani?โ€
Mimi: Unasemaje?
Anita: Naongea na nani?
Mimi: Jamani Anita...kweli namba yangu haukuwa nayo, uliifuata au unanifanyia kusudi tu?
Anita: Wewe nani?
Mimi: Naitwa Chilo.
Anita: Hahaha! Kumbe wewe..niambie sasa.
Mimi: Poa! Upo wapi?
Anita: Nipo nyumbani! Kuna nini?
Mimi: Kwani tulizungumza nini chuoni kwenye vikaratasi?
Anita: Nimesahau, hebu nikumbushe.
Sikiliza mshikaji wangu, Anita hakusahau, kwanza alijua anazungumza na nani ila alishajua kwamba namtaka hivyo akahakikisha kwamba ananisumbua na mwisho wa siku nisipate kitu kama ilivyokuwa kwa wana wengine.
Kumpata halikuwa tatizo, nilitaka kumfanyia mambo ambayo hakutegemea ili mwisho wa siku achukuliwe kiulaini kabisa, nilichokifanya ni kuwaandaa washikaji zangu wa kitaa, kama wanne hivi na mademu wawili, hao walikuwa kwa kazi maalumu ambayo ingenifanya nimchukue Anita.
Mimi: Nataka nije nikutoe out bwana...
Anita: Oooh..kumbeeee...naomba tufanye siku nyingine, leo nimechoka.
Mimi: Kuchoka si tatizo Anita, huku huji kukimbia wala kufanya kazi, nitakufuata kwa usafiri wangu, hivyo hautochoka kihivyo...make me happy bhanaa....
Anita: Chilo! Try to understand!
Mimi: Sawa.
Kulikuwa na kaugumu ila kila nilipokumbuka milioni moja iliyowekwa mezani, nilipagawa na kujitolea kwa nguvu zote. Siku hiyo, mshindi alikuwa yeye, nikakubaliana naye, hivyo nikaendelea kufanya yangu huku moyo ukiwa unauma kweli, wakati mwingine nilijuta kwa nini niliweka laki mbili zangu mezani.
Washikaji wakawa wananipigia simu na kuniuliza, ilikuwaje? Nimefanikisha? Nitamuweza? Sikutaka kuwajibu, mi nikatulia zangu na hata simu sikutaka kupokea, nikaona jibu zuri kuwajibu ni kuniona nikiwa nimemchukua huyu mtoto na kuendelea na watoto wengine ambao walinipa.

Je, nini kitaendelea?
 
CLASS CHATTING - 02

SIKU YA PILI
Mimi: Umeshatoka?
Anita: Ndiyo!
Mimi: Upo wapi kwa sasa?
Anita: Nipo kituoni. Nipitie basi!
Mimi: Huko kwenu?
Anita: Ndiyo! Kwani mbali?
Mimi: Yaap! Mbali, siwezi kukupitia, au kukurudisha muda wa kutoka.
Anita: Sawa bhana!
Hizo zilikuwa meseji za asubuhiasubuhi, nilikuwa nimeamka, mtu wa kwanza kumtafuta alikuwa yeye. Aliniambia niende kumchukua kituoni lakini nikakaza kwa sababu kuu moja kwamba sikutakiwa kuonekana laini japokuwa nilikuwa namtaka sana.
Nilipojiandaa, nikatoka zangu, nikapanda usafiri na kisha kuelekea chuo kama kawaida. Nilipofika, washikaji wakataka kufahamu, siku ya kwanza ilikuwaje? Nilifanikiwa? Maendeleo yalionyesha uhai au ndiyo hivyo yalianza kufa? Sikutaka kuwajibu zaidi ya kuwauliza, kwani wiki mbili tayari?
Kama kawaida yangu, nilipomuona Anita katulia, nikaanza kumchombeza kwa meseji.
Mimi: We Anita vibaya hivyo....Umependezaaaaa...kama naniiiiii...
Anita: Hahaha...Kama nani?
Mimi: Mlimbwende fulani hivi...miguu mizuri, kifua kizuri, sura ya kitoto, nguo zimekukaa sana, nampongeza aliyekuchagulia, anajua sana....
Anita: Hahah! Hakuna hata aliyenichagulia, nimejichagulia mimi mwenyewe...
Mimi: Mmh! Basi wewe balaa....inawezekana ukawa na nyota ya uanamitindo halafu hujijui...safi sana, napenda mwanamke smati kama wewe.
Anita: Unavyonipamba....au unataka nisahau kama ulinikatalia kunifuata kituoni?
Mimi: Hakuna bhana...niliogopa kukuchelewesha...
Anita: Au ndiyo ulikuwa unalipiza?
Mimi: Kulipiza nini?
Anita: Kuhusu jana kukataa kutoka out nawe.
Mimi: Ooh! My God! Kumbe jana nilikwambia tutoke out? Nilishasahau kabisa, unajua mambo mengi bwana mrembo...ila na wewe ulinikera...tumekubaliana, halafu ukazingua...hahaha
Anita: Hahah! Kawaida tu.
Mimi: Kwa hiyo?
Anita: Kuhusu?
Mimi: SI ile ya jana tunaenda leo!
Anita: Kwani bado tu jamani.
Mimi: Ndiyo! Tunaweza kwenda hata leo!
Anita: Mmh!
Mimi: Kwani unajua vyakula vya jana vimechacha, kwa taarifa yako leo vimepikwa vingine bhanaa...fanya hivyo!
Hiyo ilikuwa siku ya pili, mambo bado hayakuwa mepesi hata kidogo, mbele yangu nilikaona kamlima fulani hivi, kukapanda kalihitaji sana moyo, hivyo nikaendelea mapambano kwa kuamini kwamba kabla ya siku 14 ningekuwa nimemaliza kila kitu.
Tatizo la Anita lilikuwa moja, yaani anaingia, halafu anatoka....anaingia, halafu anatoka, yaani alikuwa haelewekieleweki kabisa. Sikutaka kujali sana. Ticha alipozama klasi, tulitumia muda wetu kuchati, yaani siku ya pili hiyo lakini tayari ilionekana kuwa kama mwezi kwa jinsi tulivyokuwa beneti katika simu zetu.
Muda wa kutoka, akanifuata na kuniambia nimpeleke nyumbani kwao, kama kawaida yangu, nikamkazia.
Mimi: Siendi sasa hivi...kama vipi subiri.
Anita: Jamani Chilo naomba unisaidie, nawahi mwenzako, nipelekeeeee...
Mimi: Haiwezekani Anita...yaani nitoke hapa chuo kwa ajili yako? Yaani kukupeleka tu? Acha masihara bwana, kama vipi lipia hela ya mafuta.
Anita: Yaani wewe wa kuniambia hivyo mimi?
Mimi: Kwani nimekutukana, wala sijakutukana sasa unamaindi nini?
Washikaji waliokuwa pembeni wakabaki wakishangaa, wao ndiyo walioniwekea dau kwamba nisingeweza kumchukua mtoto Anita sasa zile jeuri nilizokuwa nikimletea, iliwashangaza kwamba kwa nini nilifanya vile? Je sikuwa na mpango au, kumbe pembeni nilikuwa na mawazo yangu, tena mipango mikakati ya kumchukua kiulaini kabisa.
Anita akaondoka mahali hapo, alionekana kukasirika lakini kwangu sikuonekana kujali. Anita mwenyewe si ndiyo alijifanya mtu wa mapozi, hivyo na mimi nilijifanya kuwa na mapozi lakini ndani kabisa nilikuwa na mipango yangu.
Rajabu: Chilo, mbona umefanya hivyo?
Mimi: Kufanyaje?
Rajabu: Yaani mtoto umempa makavu, au hutaki hela?
Mimi: Huwa sipendi kuona demu akiniletea pozi, ni wa kawaida sana, sasa iweje aniletee vipozi vya kijinga, aende zake.
Hassani: Basi tuchukue kabisa hela manake umeshaharibu.
Mimi: Mchukue hela ya nini tena? Si bado siku 14 hazijakwisha?
Rajabu: Kwa hiyo una uhakika utampata?
Mimi: Nahisi...ngoja tusubiri!
Siku hiyo wala sikutaka kuzungumza sana, katika suala zito kama hilo nilitakiwa kuwa mpole kabisa, sikuwaambia mipango niliyokuwa nayo kwa kuamini kwamba siku ambayo wangekuja kuiona, wangenipigia saluti kwa kusema kwamba nilikuwa nuksi kwa watoto wa kike.
Wakati nikiwa kwenye mazungumzo na washikaji huku Anita akiwa ameondoka, ghafla nikasikia meseji ikiingia kwenye simu yangu, nilipoichukua na kuangalia jina la mtumaji, alikuwa Anita.
Anita: Hivi kweli umenifanyia hivi?
Fasta nikajibu.
Mimi: Nimekufanyaje?
Anita: Umenishushua mbele ya marafiki zako!
Mimi: Anita! Unazingua sana, una utoto mwingi, hebu kua bwana.
Anita: Unamaanisha nini?
Mimi: Ukue tu.
Hilo ndilo jibu nililompa, sikutaka kuchati naye sana, sikutegemea kumtumia tena ujumbe, kumbuka kwamba kila kitu nilichokuwa nikikifanya ni kumsogeza karibu na mwisho wa siku niweze kungโ€™oa mchuma, basi hakuridhika bwana, huyo akanitwangia.
Anita: Unanichanganya sana...
Mimi: Na nini?
Anita: Kwa nini unasema sijakua?
Mimi: Unajiona mkubwa?
Anita: Ndiyo!
Mimi: Una miaka mingapi?
Anita: 20.
Mimi: Ndiyo maana nasema kua, acha utoto Anita...
Nilikuwa namuweka kwenye maswali mengi, sikutaka ajue nilichokuwa namaanisha, ile napiga naye stori kwenye simu, akaanza kuingia mkenge kwa kuniambia kwamba ilikuwa ni lazima nionane naye, nizungumze naye, YEEEESS....
Anita: Nataka nikuone saa mbili.
Mimi: Sitokuwa na nafasi, nitakuwa nacheki habari, si unajua Magufuli kateua baraza lake la mawaziri.
Anita: Basi saa tatu...
Mimi: Haitowezekana, baada ya habari, nitakula kisha nitambonji...
Anita: Sawa, naona unanifanyia makusudi...
Anta: Unaona nakufanyia makusudi, ila ukweli sikufanyii makusudi, wewe ndiye unazingua..
Anita: Nimezingua na nini?
Mimi: Tutazungumza siku nyingine.
Nilichokigundua ni kwamba Anita hakuwa msichana wa kuwekwa presha sana, anapofanya kitu na kumkosoa ilikuwa ni lazima akwambie umtafute. Hilo, wanaume wengi hawakulifahamu, wao walimnyenyekea na wengine hata kumpa makavu hawakuweza kwa sababu alikuwa mrembo, eti ndiyo maana wengi walimuonea noma.
Kwangu, si nikajifanya mimi starling, sikutaka kumnyenyekea msichana, kwanza kufanya hivyo kwangu ni kama dhambi, huwa ninakuwa gaidi fulani hivi, ukimaindi, haina noma, wewe sepa mimi wala sijali.
Aliningโ€™angโ€™aniza nionane naye, nikamkazia, akaona duuh! Mambo yamekuwa si mambo, akaanza kunichombeza kwa vineno vyake ili mradi niwe dhaifu na kumwambia poa tuonane, ila kwangu akagonga mwamba, ilishindikana kabisa.
Usiku, sikumcheki, alinitumia meseji, nikawa doro, sikujibu chochote kile, yeye si alijiona mrembo, wanaume kumshobokea akajua wote tupo hivyohivyo, sasa kwangu akagonga mwamba. Mwisho wa siku akanitumia meseji hii...
Anita: Umelala?
Mimi: Ndiyo! Tena naota sasa hivi...
Anita: Hahah! Acha utani bhana....
Mimi: Anita unanisumbua, nimekwambia nimelala na ninaota, husikii...
Anita: Naomba unisamehe kwa kukusumbua...
Hiyo ya mwisho wala sikuijibu, nikachuna japokuwa kimoyo nacho kilikuwa kinauma kindanindani kwa sababu, kama ningekubali kwa haraka, basi ilikuwa ni lazima ningโ€™oe mchuchu fasta, nilambe halafu nisepe na mpunga, ila kufanya hivyo bila kumsumbua isingekuwa poa kivile, kwanza asote ndiyo mwisho wa siku nimalize yangu.
Alipoona nimekaa kimya, alichokifanya ni kunitumia meseji huku akinidedicate Wimbo wa Sorry wa Justin Bieber, pamoja na hayo, nikachuna tuliiiiiiiiii.....

Je, nini kitaendelea?
 
Wapi stori jamani, lete nyunyuzi mkuu.

T[emoji769]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ