Suala la Machinga, yafanyike haya

Suala la Machinga, yafanyike haya

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Kwanza kabisa napenda kupongeza serikali kwa maamuzi waliyoanza kuyafanya ya kuwaondoa Machinga katika maeneo ambayo hawatakiwi kuwepo Mf Barabarani na kwenye maeneno ya miji yenye shughuli za kiofisi n.k

Tulishauri hapa na tumeshauri hapa kwa miaka mingi sana namna ya kuhandle hili jambo na nashukuru sasa Serikali wameona kuna haja lianze kufanyiwa kazi.

Kwanza napenda kusema wazi Tatizo la mipango mibovu kwenye miji yetu, majiji yetu ikiwemo kuzagaa hovyo kwa machinga ni matokeo ya uvivu, uzembe , kukosa exposure na kutowajibika kwa kipindi kirefu sana Kwa watendaji wetu! Hii ni Kwa sababu suala la machinga lilitakiwa kuanza kufanyiwa kazi kwa kipindi kirefu sana na hata sasa hili kundi lingekuwa linafanya kazi katika maeneo yaliyopangwa vizuri na hata lingekuwa linalipa kodi Kama makundi mengine ya wafanyabiashara.

Napendekeza katika kuangalia mipango ya muda mfupi na mrefu! Suala la machinga lishughulikiwe Kama ifuatavyo

1. Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Watendaji Wao, waande kufanya vikao vya majadiliano na Machinga. Wawaeleze kuhusu umuhimu wa wao kuendelea kufanya biashara ila kwenye maeneo rasmi, yaliyopangwa vizuri na kuwekewa utaratibu mzuri. Vikao hivi Vifanywe kwenye maeneo halisi walipo Machinga/ Wafanyabiashara wadogo wadogo.

2. Wakuu wa Mikoa, Wilaya, waandae maeneo hayo rasmi yenye mzunguko mkubwa wa watu mf. Karibu na vituo vya mabasi au ofisi au masoko na wawape tenda hata vijana wetu wanaosoma chuo cha ardhi wadesign aina ya majengo/ vibanda ambayo vinatakiwa kujengwa kwenye maeneo hayo. Michoro hiyo ikishapitishwa, Uongozi wa Majiji na Miji husika ndo ujenge na kusimamia ujenzi wa hayo structures izo - Ziwe na standard moja zinazofanana na zijengwe kisasa.

Msisitizo uwekwe kwenye kujengwa structures izo kwenye standard za juu za ubora ambazo haziruhusu miji kuchafuka. Zikishajengwa then wafanyabiashara wadogo wadogo wapangiwe kufanya kazi kwenye maeneo hayo. Kwa utaratibu wa kuzingatia usafi na mpangilio bora.

3. Uwekwe muongozo wa Wafanyabiashara kufanya biashara kwenye maeneo hayo. Ziteuliwe kamati za Wafanyabiashara hao hao katika kusimamia iyo miongozo itakayogusa namna ya kufanya biashara, jinsi ya kuzingatia usafi na mpangilio. Endapo eneo husika litakiuka hiyo miongozo uwajibishwaji uanze kwa kamati husika. Kuwe pia na penalties katika kukiuka iyo miongozo ikiwemo fine na hata kuzuiwa kufanya biashara kwenye eneo hilo.

4. Endapo mfanyabiashara anahitaji kufanya biashara nje ya eneo lililopangwa na kutengwa Kwa ajiri ya yeye kufanya biashara, kuwe na Miongozo maalum ya namna mfanyabiashara huyo anatakiwa kufanya biashara yake kwenye eneo hilo, namna anavyotakiwa kujenga eneo lake la biashara na Pia wawekewe kodi maalum ya kulipia ili afanye biashara kwenye eneo hilo ambalo ni nje ya eneo lililotengwa kwa kufanyiwa biashara. Kiwango cha kodi ambacho mfanyabiashara hiyo anatakiwa kulipa katika kufanya biashara kwenye eneo hilo lazima kiwe juu zaidi kuliko kiwango anachotakiwa kulipia katika maeneo ambayo wenzake wametengewa kufanya biashara.

Mwisho napenda kumpongeza Mama Samia kwa kuruhusu hili lifanyike. Naomba tu haya mawazo yazingatiwe maana tutaweza kumaliza hili Tatizo la uchafuzi wa miji na kuharibika kwa majibu yetu kutokana na ufanyaji wa biashara holela usiozingatia mipango miji na ukusanyaji wa kodi.

Naomba kuwasilisha
 
Hizi ni bla bla za midomoni tu.

Sheria za uzururaji zipo.

Kila mtu anataka kufanya biashara popote, utaongeaje na mtu huyo.

Hataki kujenga frame wala kulipa kodi, hayo mazungumzo yatakuwa vipi.

This is a mass migration from rural areas to towns /cities.

Chukua hao vijana wote peleka JKT walime na wazalishe, hata wakiwa laki tano.
 
Hizi ni bla bla za midomoni tu.
Sheria za uzururaji zipo.
Kila mtu anataka kufanya biashara popote, utaongeaje na mtu huyo.
Hataki kujenga frame wala kulipa kodi, hayo mazungumzo yatakuwa vipi.
This is a mass migration from rural areas to towns /cities.
Chukua hao vijana wote peleka JKT walime na wazalishe, hata wakiwa laki tano.
Matumizi ya akili yana matokeo mazuri zaidi kuliko matumizi ya nguvu
 
Machinga leo wanaitwa uchafu takataka.

Kama JPM alikuwa anapata feelings nazosikia nikiwatazama wamachinga mitaa ya kariakoo, basi Mungu ampe pumziko jema yule mzee.

Kuna wanangu sijui wataenda kuishije mtu kamaliza chuo miaka 7 hana kazi kaamua kuwa mlengaji anaanza kuona mwanga mara paap anarudishwa kitaa...

Sijui kama watu wanaona kinachoenda kutokea....all in all maisha ni vita ngumu sana mtu asipojua size ya viatu vyako anaweza fanya lolote tu... poleni sana wanangu kwa sasa hamna chenu.
 
Machinga leo wanaitwa uchafu takataka.

Kama JPM alikuwa anapata feelings nazosikia nikiwatazama wamachinga mitaa ya kariakoo, basi Mungu ampe pumziko jema yule mzee.

Kuna wanangu sijui wataenda kuishije mtu kamaliza chuo miaka 7 hana kazi kaamua kuwa mlengaji anaanza kuona mwanga mara paap anarudishwa kitaa...

Sijui kama watu wanaona kinachoenda kutokea....all in all maisha ni vita ngumu sana mtu asipojua size ya viatu vyako anaweza fanya lolote tu... poleni sana wanangu kwa sasa hamna chenu.
Takataka ni kitu chochote ambacho kipo mahali kisipostahili kuwepo!

Kukosa ajira sio kibali cha kufanya biashara katikati ya barabara hadi watembea kwa miguu wanashindwa kupata maeneo ya kupita!

Kukosa ajira sio kibali cha kujenga vibanda hovyo bila mpangilio maalum hadi kwenye njia za magari au sehemu zilizohifadhiwa kwa shughuli maalum.

Ni lazima kuishi kwa utaratibu! Ambaye haishi kwa utaratibu ni mnyama tu asiye na akili!
 
Hapa Mama Samia anamsikiliza kama kweli mtu,kumbe nyoka mwenye Sumu mbaya,huyu ndo alikuwa anatoa siri za Ikulu,mpuuzi sana huyu
Nyoka kivipi?
Tunajua Chato gang hamumpendi Rais Samia Ila mkubali au mkatae huyo ndo Rais wenu na yupo vizuri tunamkubali!
 
JPM aliwapa jeuri ipi?

Unajua kwamba wamachinga nao ni raia wa nchi hii?

Kama hijui usiongee, JPM alitoa maelekezo sahihi kabisa hata SSH anajua


Tulia ww
 

Kwanza kabisa napenda kupongeza serikali kwa maamuzi waliyoanza kuyafanya ya kuwaondoa Machinga katika maeneo ambayo hawatakiwi kuwepo Mf Barabarani na kwenye maeneno ya miji yenye shughuli za kiofisi n.k


Tulishauri hapa na tumeshauri hapa kwa miaka mingi sana namna ya kuhandle hili jambo na nashukuru sasa Serikali wameona kuna haja lianze kufanyiwa kazi.

Kwanza napenda kusema wazi Tatizo la mipango mibovu kwenye miji yetu, majiji yetu ikiwemo kuzagaa hovyo kwa machinga ni matokeo ya uvivu, uzembe , kukosa exposure na kutowajibika kwa kipindi kirefu sana Kwa watendaji wetu! Hii ni Kwa sababu suala la machinga lilitakiwa kuanza kufanyiwa kazi kwa kipindi kirefu sana na hata sasa hili kundi lingekuwa linafanya kazi katika maeneo yaliyopangwa vizuri na hata lingekuwa linalipa kodi Kama makundi mengine ya wafanyabiashara.

Napendekeza katika kuangalia mipango ya muda mfupi na mrefu! Suala la machinga lishughulikiwe Kama ifuatavyo

1. Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Watendaji Wao, waande kufanya vikao vya majadiliano na Machinga. Wawaeleze kuhusu umuhimu wa wao kuendelea kufanya biashara ila kwenye maeneo rasmi, yaliyopangwa vizuri na kuwekewa utaratibu mzuri. Vikao hivi Vifanywe kwenye maeneo halisi walipo Machinga/ Wafanyabiashara wadogo wadogo.

2. Wakuu wa Mikoa, Wilaya, waandae maeneo hayo rasmi yenye mzunguko mkubwa wa watu mf. Karibu na vituo vya mabasi au ofisi au masoko na wawape tenda hata vijana wetu wanaosoma chuo cha ardhi wadesign aina ya majengo/ vibanda ambayo vinatakiwa kujengwa kwenye maeneo hayo. Michoro hiyo ikishapitishwa, Uongozi wa Majiji na Miji husika ndo ujenge na kusimamia ujenzi wa hayo structures izo - Ziwe na standard moja zinazofanana na zijengwe kisasa.

Msisitizo uwekwe kwenye kujengwa structures izo kwenye standard za juu za ubora ambazo haziruhusu miji kuchafuka. Zikishajengwa then wafanyabiashara wadogo wadogo wapangiwe kufanya kazi kwenye maeneo hayo. Kwa utaratibu wa kuzingatia usafi na mpangilio bora.

3. Uwekwe muongozo wa Wafanyabiashara kufanya biashara kwenye maeneo hayo. Ziteuliwe kamati za Wafanyabiashara hao hao katika kusimamia iyo miongozo itakayogusa namna ya kufanya biashara, jinsi ya kuzingatia usafi na mpangilio. Endapo eneo husika litakiuka hiyo miongozo uwajibishwaji uanze kwa kamati husika. Kuwe pia na penalties katika kukiuka iyo miongozo ikiwemo fine na hata kuzuiwa kufanya biashara kwenye eneo hilo.

4. Endapo mfanyabiashara anahitaji kufanya biashara nje ya eneo lililopangwa na kutengwa Kwa ajiri ya yeye kufanya biashara, kuwe na Miongozo maalum ya namna mfanyabiashara huyo anatakiwa kufanya biashara yake kwenye eneo hilo, namna anavyotakiwa kujenga eneo lake la biashara na Pia wawekewe kodi maalum ya kulipia ili afanye biashara kwenye eneo hilo ambalo ni nje ya eneo lililotengwa kwa kufanyiwa biashara. Kiwango cha kodi ambacho mfanyabiashara hiyo anatakiwa kulipa katika kufanya biashara kwenye eneo hilo lazima kiwe juu zaidi kuliko kiwango anachotakiwa kulipia katika maeneo ambayo wenzake wametengewa kufanya biashara.

Mwisho napenda kumpongeza Mama Samia kwa kuruhusu hili lifanyike. Naomba tu haya mawazo yazingatiwe maana tutaweza kumaliza hili Tatizo la uchafuzi wa miji na kuharibika kwa majibu yetu kutokana na ufanyaji wa biashara holela usiozingatia mipango miji na ukusanyaji wa kodi.

Naomba kuwasilisha
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwani Bibi ana chuki na watu wa Chato[emoji23][emoji23][emoji23],Mama hana akili,na huku mtaani hakubaliki kabisa,kwanza hakupigiwa kura
Kwani JPM alikua anakubarika? Au alikua analazimisha misifa ya kijinga tu....Mungu Fundi... Ata nyumbani kwako kuna utaratibu huwezi ruhusu watoto wako waweke Viatu kwenye Friji huo ni upumbavu tu...Leo machinga wanapanga nyanya Barabarani kwenye Rami hii uliiona wapi km ulikua sio usen.ge wa JPM? Wakuu WaMikoa baadhi walijaribu kuwatafutia maeneo ya kwenda wakawa hawataki na JPM akawa anawakaripia hao wakuu... Leo pita miji mikubwa yani wamepanga nyanya hadi kwenye Round about kitu ambacho ni ushamba na hatari kwa usalama... Nchi lazima iwe na utaratibu... Samia ndo Rais kwasasa uwe umempigia kura au lah ata JPM hakupendwa na wote
 
😂😂😂😂 kwani Bibi ana chuki na watu wa Chato😂😂😂,Mama hana akili,na huku mtaani hakubaliki kabisa,kwanza hakupigiwa kura

Unafikiri inasaidie kumtusi Rais wako


Wanadamu hawana jema
 
Back
Top Bottom