Suala la maji wanyonge hatuna pa kusemea

Suala la maji wanyonge hatuna pa kusemea

Nakadori

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
8,778
Reaction score
21,010
Hata nguvu ya kusalimia sina.

Mji mzima kila mtu analalamika maji hakuna.

Hatuogi, hatufui, hatupiki....maji yamekuwa kama madini.....mtaani hayapatikani, na watu wa magari wanaosambaza hawauzi tank moja la lita 1000 ni kuanzia lita 3000 tena kwa 120000 hizo lita 3000.

Hivi kweli sisi wanyonge wa nchi hii tutaishije? Ni kweli tuna raisi na viongozi wengine wanaojua matatizo yetu au ni kwamba wao wakishakaa kwenye viyoyozi ofisini na kwenye ma vieiti basi wanasahau kwamba kuna watu wanataabika huku mtaani?

Serikali imekosa utatuzi wa hili tatizo kweli? Week zaidi ya 3 maji hakuna bombani? Hata kwa kukosea tu wameshindwa kutupatia maji?

Mbona maisha yamekuwa magumu sana?

Ninaandika kwa uchungu mwingi sana.
 
Duh kweli kazi ipo. Mimi huko mara ya mwisho nimenunua ijumaa lita 2000 kwa 40000 ila jamaa akasema hali ikiendelea watapandisha maana wanakochukulia maji pale dawasa kuna bonge la foleni
 
Yani na kuandamana bado maji hayaanza tu kutoka!!!
 
Duh kweli kazi ipo. Mimi huko mara ya mwisho nimenunua ijumaa lita 2000 kwa 4000 ila jamaa akasema hali ikiendelea watapandisha maana wanakochukulia maji pale dawasa kuna bonge la foleni
Wananchi wanateseka sana...
I wish watu wa magari wangekuwa hata wanapaki mahali wanauza kwa ndoo watu wengi wangenunua tu
 
Wananchi wanateseka sana...
I wish watu wa magari wangekuwa hata wanapaki mahali wanauza kwa ndoo watu wengi wangenunua tu
Kweli kabisa mkuu watu wanahangaika na maji. Huku nimeambiwa dumu 700, gari kwa lita 1000 bado 20,000 kwa maji ya dawasa na 15000 kwa maji ya kisima.
 
Back
Top Bottom