Suala la mzee Mwinyi kuzikiwa Zanzibar wala lisifanywe la kisiasa, pitieni hapa msome muelewe sababu

Suala la mzee Mwinyi kuzikiwa Zanzibar wala lisifanywe la kisiasa, pitieni hapa msome muelewe sababu

Mimi m'bara original mkuu. Kuwa na mawazo tofauti haimaanishi kuwa mtu sio m'bara. Maana hata Hussein Mwinyi kwao bara, lakini kaamua baba yake azikiwe Zanzibar.

Kuna watz wengi walitoka mikoani kuja Dar, na bado wakifariki wanazikiwa hapa hapa Dar sio mikoani kwao.
Kazaliwa bara ila kwao ni visiwani
 
Maswali nimekuuliza pale juu naona umeshindwa kujibu ili tujue mvivu kati yetu ni nani, naamini umepata jibu ukaamua kupotezea usijali kiutu uzima nimekuelewa, naona umerukia sehemu nyingine kama kawaida yako....

Unaposema: " hakuna sababu yoyote ya kumfanya Mwinyi asitake kuzikwa Zanzibar" kwani ulikuwa unaingia ndani ya kichwa chake kuona nini alichokuwa akifikiria wakati akiwa hai? huoni kama huu nao ni "uzushi" wako!, ajabu one minute unajidai hupendi uzushi, next unaleta uzushi wako!.

Unadai tena: "hakuna logical consistency yoyote.." unaweza vipi kuipata consistency kwa jambo lililoanza kuzungumzwa juzi baada ya kifo chake? Hujioni ulivyo mweupe hata usiyejua maana ya consistency!.

- Usilazimishe kuufunga mjadala because of your lazy mind - kusubiri ushahidi, wacha tunaofikirisha bongo zetu tuendelee kutafakari mbele tutaipata hiyo logical consistency yako.

Unaita tena sababu nazotoa ni "uzushi pure" sijui unatumia kipimo gani kudhani hivyo, narudia tena kama ni fikra zako, basi uko wrong, kwasababu wewe sio kipimo cha usahihi hapa duniani, kujua uzushi upi ni pure, na upi sio pure, hata kama unatumia "logic" yako, kwangu huo ni ujuaji wako tu.

Lastly, huo mfano uliotoa wa .... mimi kuwa sawa na kula nyama za watu, hapo ndio naona kabisa umechoka akili ndugu, pumzika, maana hata mambo unayozungumzia hayaendani tena na mada iliyoko mezani, umegeuka ndege anayerukia kila tawi la mti, bahati mbaya kwake miti yote huteleza!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Hoja yako yote imejengwa katika wosia wa Mwinyi ambao hujaweza kuthibitisha upo.

Ni hoja ya kizushi tu.
 
Ndugu hao vijana wanabisha mambo wasioyajua. Huyo anaekwambia kuzikwa kifamilia huko kijiji ni jambo la mila na desturi. Anajifanya hajui kuwa 70% ya watu waliotoka mikoani kuja kutafuta maisha Dar huzikwa hapa hapa Dar es salaam na sio mikoani kwao.

Mbona hajawahi kubisha au kushangazwa na hilo?
Haya mengine ni matatizo ya kisaikolojia tu.
 
Hayo ni maono yako mtoa mada,nakumbuka nilipokuwa nasoma kule st mathew mbagala kila week mzee mwenye nilikuwa namwona na king'ora chake anaenda mkuranga kwao...hii ya znzbr imenishangaza kidogo...yasemwayo yapo .....
 
Nikajua unajua kumbe unahisi. Hao unaowasema watoto wake ikiwa ni pamoja na Rais wa Zanzibar Dr. Mwinyi, aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mkuranga mbona hakutengwa kwa vile ni Mzanzibar? Mkuranga ndo kwao hayo mengine ya Mzee Ruksa kuzikwa Zanzibar ni ya kutafuta uhalali wa kisiasa wa Dr. Mwinyi.
Upo sahihi mkuu
 
Hayo ni maono yako mtoa mada,nakumbuka nilipokuwa nasoma kule st mathew mbagala kila week mzee mwenye nilikuwa namwona na king'ora chake anaenda mkuranga kwao...hii ya znzbr imenishangaza kidogo...yasemwayo yapo .....
Mkuranga ipo ndani ya JMT na Zanzibar pia ipo ndani ya JMT. Sasa hapo tatizo liko wapi?

Asilimia kubwa ya wakazi wa Dar walitokea mikoani, na wengi waliokufa wamezikiwa hapa hapa Dar, mbona hamshangai au kuuliza kuhusu hilo?
 
Kasema nani kwao na Mwinyi ni Mkuranga?
Kasema mwenyewe kipindi cha kuzindua kitabu cha maisha yake. Anasema alipelekwa katika kisiwa hicho kwa lengo la kusoma dini ya kiislam. Ndiomaana unaona kuna mjadala wa watu kushangaa kwanini azikiwe Zanzibar na sio kwao Mkuranga.

Miaka 1950 kushuka chini Zanzibar ndio ilikuwa kitovu cha mafunzo ya dini ya kiislam. Hivyo wazazi wengi waliopenda dini kutoka katika nchi mbali mbali waliwapeleka watoto wao wakasome dini katika kisiwa hicho.

Historia inasema hata Abeid Amani Karume alipekwa Zanzibar na wazazi wake kusomea dini. Abeid Amani Karume asili yake ni Malawi, kutoka kabila la wayao wa upande wa Malawi, maana kuna wamalawi wa upande wa Tanzania pia.
 
Uzikiwe popote pale ila matendo yako ndio yatakayokusaidia huko kaburini.

Allah amjaalie qauli thabit mzee wetu, amuingize katika pepo!
 
Hayo mambo yaliyojadiliwa kwenye familia ya Mwinyi kama kweli yalijadiliwa, ni siri yao.

Lakini kimsingi, siku zote mtoto lazima azikwe pale walipozikwa wazazi wake, huu ndio utamaduni wetu, unalazwa pale walipolazwa ndugu zako wengine.

Sasa leo Mwinyi badala ya kuzikwa Mkuranga anaenda kuzikwa Zanzibar, kisa alisoma huko, hebu tuambie, kwa uamuzi wenu huo, hivi hamuoni kama mmemtenga na ndugu zake wengine waliozikwa huku Bara?

Ndugu yake yupi tena atakaekwenda kuzikwa nae Zanzibar, kama ni Rais Dr. Mwinyi, hamuoni pia hawa wawili mtakuwa mmewatenga na ndugu zao wengine waliozikwa huku Bara?

Hapo ndipo unapopata picha kwamba, huu uamuzi wa kumzika Mzee Mwinyi Zanzibar, ni purely political motivated.

Ndio maana kwasababu hizo za kisiasa, watajikuta ni wao wawili pekee, baba mtu na mwanae [kama nae atataka kuzikwa huko, sababu wanasema anaogopa baba yake kuzikwa bara sababu naye ataonekana sio mzanzibar na maadui zake kisiasa, sijui akiondoka madarakani hiyo hofu itabaki au ataondoka nayo] kama itabaki, ndio wawili pekee watakaozikwa Zanzibar, huku ndugu zao wengine wote wakizikwa Bara.

I never thought kama siasa ina nguvu kiasi hiki, au ni uoga tu wa mwanasiasa mwenyewe anayeamua kuchukua maamuzi yatakayokwenda kinyume na mila na desturi zetu, kwa maslahi yake ya kisiasa, hiki kilichofanyika kwa Mzee Mwinyi, binafsi sijakipenda, tunatakiwa siku yetu ya mwisho sote tulazwe pale walipolazwa ndugu zetu kama nafasi ipo.

Na ndio maana pia, wengine wetu ambao hawana uwezo wa kusafirisha ndugu zao, hupeleka udongo wa pale alipozikwa ndugu yao nyumbani kwao uende kuzikwa huko, yote hii ni ili kuonesha umuhimu wa kumzika marehemu pale alipozaliwa, nashangaa na kusikitika kwanini wamemuondolea Mzee Mwinyi haki yake hii, ikiwa uwezo wa kumsafirisha na kumzika nyumbani kwao Mkuranga upo, sio fair.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Je sisi tulio zaliwa Tanganyika tukifa tunazikwa wapi maana saivi Tanganyika haipo Kuna Tanzania na Zanzibar. 😂😂 Muunganiko wa Tanganyika na Zanzibar umeleta Tanzania na Zanzibar kazi iendelee. Kuzikwa ni kuzikwa tu.
 
Akhsante sana ndugu Nguruvi3 .
Kongole kwa mchango bora sana.
Mjadala huu ufungwe sasa.
Huwezi kulitenga suala hili na siasa hasa siasa za Zanzibar
Kuzikwa popote siyo tatizo, hata Raza aliyeuchukia Muungano alizikwa Kisutu.

Unguja wangependa azikwe huko kwasababu ni mwana Mapinduzi na itaondoa hoja za Wapemba
Mwinyi alikubalika Zanzibar kwasababu ilikuwa timu ya Kombo Thabiti , watu wa Mapinduzi

Kwasiasa za ubaguzi, wapo wanaoamini Mwinyi na waliotoka Bara kama VP Seif Idd si Wazanzibar.

Rais Hussein Mwinyi anakutana na wakati mgumu sana akisemwa si ''Mzanzibar halisi'' , anapigwa vita hata ''Shangazi' amewahi kulisema.

Kwa kutambua hilo kwa maoni yangu Familia iliamua azikwe Zanzibar ili kujenga msingi wa vizazi vijavyo kwamba ni Wazanzibar! Siasa ipo ndani ya hili

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Kasema mwenyewe kipindi cha kuzindua kitabu cha maisha yake. Anasema alipelekwa katika kisiwa hicho kwa lengo la kusoma dini ya kiislam. Ndiomaana unaona kuna mjadala wa watu kushangaa kwanini azikiwe Zanzibar na sio kwao Mkuranga.

Miaka 1950 kushuka chini Zanzibar ndio ilikuwa kitovu cha mafunzo ya dini ya kiislam. Hivyo wazazi wengi waliopenda dini kutoka katika nchi mbali mbali waliwapeleka watoto wao wakasome dini katika kisiwa hicho.

Historia inasema hata Abeid Amani Karume alipekwa Zanzibar na wazazi wake kusomea dini. Abeid Amani Karume asili yake ni Malawi, kutoka kabila la wayao wa upande wa Malawi, maana kuna wamalawi wa upande wa Tanzania pia.
Alisema na kitabu kinasema alizaliwa Mkuranga- kuzaliwa hakuna mahusiano na kwao mtu ni wapi. Wapo watu wamezaliwa Kenya lakini kwao ni Tanzania kwa mazazi na sheria.
 
Alisema na kitabu kinasema alizaliwa Mkuranga- kuzaliwa hakuna mahusiano na kwao mtu ni wapi. Wapo watu wamezaliwa Kenya lakini kwao ni Tanzania kwa mazazi na sheria.
Kumbe unaandika kwa mifano ya mtu kuzaliwa Kenya. Mimi nilijua utakuja na uthibitisho wa kuonesha kuwa Mwinyi alizaliwa tu Mkuranga lakini wazazi wake ni wazanzibar.

Kama hauna vithibitisho vya kuonesha kuwa wazazi wake ni wazanzibar, basi hauna haki ya kunifanya mimi niamini ulichoandika.

Mimi nimethibitisha kwanza kupitia kuzaliwa, na pili kauli yake mwenyewe ya kupelekwa Zanzibar kusoma dini. Sasa na wewe thibitisha kwanza uzanzibar wake kupitia wazazi wake, na pili uniambie aliposema kuwa nilipelekwa nyumbani Zanzibar kusomea dini. Zaidi ya hapo utakuwa umeamua tu kubishana huku ukweli wa kile nilichoandika ukiwa unaujua moyoni mwako.
 
Sio familia yake ni yeye.kwa mfano uamuzi wa wewe kuzikwa Sehemu sio ya familia ni wako.
Lakini kumbuka uamuzi pia hubadilika. Ndomaana unaweza kusikia mtu anakwambia amebadili maamuzi yake.

Nikiwa na maana kwamba huenda kabla ya kukata roho watoto wake walikaa nae wakamshauri azikiwe Zanzibar na yeye akabadilisha uamuzi na kuridhia kile walichomshauri au kumuomba akubali.
 
Back
Top Bottom