Suala la uraia pacha alilosema Malamula litapatiwa ufumbuzi kamba ya mwisho mwa 2021 ni lipi hasa, au tulidanganywa kama siku zote?

Suala la uraia pacha alilosema Malamula litapatiwa ufumbuzi kamba ya mwisho mwa 2021 ni lipi hasa, au tulidanganywa kama siku zote?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Nina tatizo la waandishi wa habari wa Tanzania - huwa hawajui kufuatilia mambo, na mara nyingi wanaishi kwa ajii ya siku iliyopo tu.
  • Kuna wakati kurugenzi ya Habari ilitangaza kwamba Chancellor wa Germany Angela Melkel kaongea na Magufuli kujenga kiwanda cha mbolea mwaka 2022. Hakuna aliyefuatilia suala hili limeishia wapi
  • Kuna wakati tulisikia Mkurugenzi mmoja amemuua muumini wa Sabato kwa risasi, hakuna anaefuatilia suala hilo limeishia wapi
  • Ahadi za SGR, ahadi za kutokatika umeme, ahadi za umeme wa Stiegla, ahadi za hiki na kile, bure!
Ahadi nyingi sana zinatolewa, matukio mengi yanatokea, lakini hakuna mwandishi anaerudi kuuliza jambo fulani tueleze limefikia wapi, kitu ambacho kinafanya wanasiasa na watendaji wa serikali kuona kwamba Watanzania wanadanganyika kirahisi sana - kila jambo linapita na upeopo na wanasahau.

Sasa turudi kwa Waziri wetu wa Mambo ya Nje Mulamula; Mwezi August mwaka huu 2021 aliongea na waandishi wa habari kwamba kuna mwelekeo mpya kuhusu suala la uraia pacha, na kwamba kabla ya mwisho wa 2021 litakuwa limepatiwa ufumbuzi. Hivi ni waandish wangapi wamerudi kwa Malamula na kuomba mrejesho wa ahadi yake?

Je tutamlaumu Raisi Mkapa pale alipowaponda waandishi wa habari wa Tanzania?

Refer: Mwelekeo mpya kwa uraia pacha

Saturday August 07 2021​

Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amesema Serikali inalifanyia kazi suala la uraia pacha na kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha, litakuwa limepatiwa ufumbuzi.
 
Uraia pacha wa nini? Kama unaipenda Marwkani kaishi huko achana na Bongo. Kama bado unaitaka Bongo kafanye kazi Marekani urudi kuzikwa Bongo, full stop.

Nchi nyingi kubwa hawaruhusu huo uraia pacha sembuse Choka mbaya Tanzania.

Tanzania ina matatizo mengi ya kushughulikia sio uraia pacha.

 
Tatizo hatuna waandishi wa habari bali makanjanja tu ambao hawana labda hata nauli ya kwenda na kurudi kila siku kutafuta habari au kufanya mahojiano au kumuuliza waziri au Katibu Mkuu wa Wizara

Usitegemee ukaona mwandishi akiomba mjadala na waziri kila Jambo linapotokea
Huwa ni siku hiyo hiyo na likipita basi wanasubiri tukio lingine
 
Kwa mfano Elon musk ana uraia wa nchi tatu- marekan, Canada na south africa. Sijui Africa kusin kama inanufaika na uraia wa huyo tajiri wa dunia
 
Kwa mfano Elon musk ana uraia wa nchi tatu- marekan, Canada na south africa. Sijui Africa kusin kama inanufaika na uraia wa huyo tajiri wa dunia
Yes SA inanufaika mno maana ni raia wake means kodi nyingi inakusanywa kutoka kwa tycoon huyo uliyemtaja.
 
Kwa mfano Elon musk ana uraia wa nchi tatu- marekan, Canada na south africa. Sijui Africa kusin kama inanufaika na uraia wa huyo tajiri wa dunia
Umeshasema tajiri wa dunia, mengineyo hihitaji akili kubwa kufikiri
 
Tatizo hatuna waandishi wa habari bali makanjanja tu ambao hawana labda hata nauli ya kwenda na kurudi kila siku kutafuta habari au kufanya mahojiano au kumuuliza waziri au Katibu Mkuu wa Wizara

Usitegemee ukaona mwandishi akiomba mjadala na waziri kila Jambo linapotokea
Huwa ni siku hiyo hiyo na likipita basi wanasubiri tukio lingine
Waandishi wetu wengi huwa wanasubiri press conference, lakini akili ya kutafuta habari na kuwa investigative hawana kabisa!
 
Nchi kubwa unazijua ama unabwabwaja tu? Kama hauna uwezo wa kupata uraia pacha acha wenye uwezo wa kupata wapate. Wee inakuumiza nini?
Uraia pacha wa nini? Kama unaipenda Marwkani kaishi huko achana na Bongo. Kama bado unaitaka Bongo kafanye kazi Marekani urudi kuzikwa Bongo, full stop.

Nchi nyingi kubwa hawaruhusu huo uraia pacha sembuse Choka mbaya Tanzania.

Tanzania ina matatizo mengi ya kushughulikia sio uraia pacha.

 
  • Thanks
Reactions: Tui
Nchi kubwa unazijua ama unabwabwaja tu? Kama hauna uwezo wa kupata uraia pacha acha wenye uwezo wa kupata wapate. Wee inakuumiza nini?
Mie nilishagundua siku nyingi kwamba kuna watanzania wana wivu wa ajabu sana, wa kutotaka watu wengine wapate fursa! Utakuta mtu kama huyu anabisha tu kwa kuwa anajua hata afanye nini hatapata uraia pacha, kwa hiyo anaona ni afadhali wote tuishi kama mashetani - sawa tu na yule shetani mkubwa, mentality moja!
 
Ukitaka kujua Waswahili ni mashetani, eti wana methali inasema, "kifo cha wengi ni harusi"!! Yaani inaonyesha jinsi roho mbaya ilivyo kwenye DNA zetu.
Mie nilishagundua siku nyingi kwamba kuna watanzania wana wivu wa ajabu sana, wa kutotaka watu wengine wapate fursa! Utakuta mtu kama huyu anabisha tu kwa kuwa anajua hata afanye nini hatapata uraia pacha, kwa hiyo anaona ni afadhali wote tuishi kama mashetani - sawa tu na yule shetani mkubwa, mentality moja!
 
Ukitaka kujua Waswahili ni mashetani, eti wana methali inasema, "kifo cha wengi ni harusi"!! Yaani inaonyesha jinsi roho mbaya ilivyo kwenye DNA zetu.
Eti tusote wote hapahapa Bongo sio mnaenda huko mnarudi kututambia la Lamborghini zenu! Mentality ya ajabu sana.
 
Tatizo hatuna waandishi wa habari bali makanjanja tu ambao hawana labda hata nauli ya kwenda na kurudi kila siku kutafuta habari au kufanya mahojiano au kumuuliza waziri au Katibu Mkuu wa Wizara

Usitegemee ukaona mwandishi akiomba mjadala na waziri kila Jambo linapotokea
Huwa ni siku hiyo hiyo na likipita basi wanasubiri tukio lingine
Labda Pascal Mayalla anaweza kuhoji. Nimewahi kusoma makala yake moja ya “kwa maslahi ya Taifa”, ambapo alizungumzia suala hili la diaspora.

Lakini umesema ukweli waandishi wetu wengi makannjanja.
 
Back
Top Bottom