Sugu baibai Mbeya Mjini? Ili Tulia aendelee na urais IPU anatakiwa asipoteze ubunge miaka mitatu

Sugu baibai Mbeya Mjini? Ili Tulia aendelee na urais IPU anatakiwa asipoteze ubunge miaka mitatu

Weka record vizuri mbunge aliyechaguliwa Kwa kura nyingi 2015 ni Gibson Olemaseyeki alikuwa MB wa ARUMERU Magharibi

Sugu_mbeya mjini 2015.png
 
Umesahau kwamba Yule Mbunge wa Shinyanga Steven Masele alikua Rais wa Bunge la Africa na alitemwa ubunge Mwaka 2015?
Watu mnasahau mapema sana
Alitemwa mwaka 2020, alikuwa ana shida zake na CCM. Mwaka 2019 Ndugai aliandika barua PAP kusitisha uwakilishi wake, wakamrudisha nyumbani na kumpeleka kamati ya maadili kwa utovu wa nidhamu..
 
Alitemwa mwaka 2020, alikuwa ana shida zake na CCM. Mwaka 2019 Ndugai aliandika barua PAP kusitisha uwakilishi wake, wakamrudisha nyumbani na kumpeleka kamati ya maadili kwa utovu wa nidhamu..
Yeah nimekumbuka 2020, Ndugai ni majukumu yake kuandika Barua PAP maana hiko cheo kinakoma pale ukiacha kuwa mbunge Maana utakuwa hubanwi na sheria zozote za Uwajibikaji.
 
Kuwa rais IPU, haikufanyi uwe na tiketi ya uhakika ya kubaki bungeni kwa kura za wananchi, matakwa ya IPU Sio matakwa ya watu wa Mbeya. Watu wa Mbeya wanataka kiongozi atakaye timiza haja za Wana Mbeya, na sio habari za IPU. IPU haitatui shida za wanambeya.
 
Jambo la pili spika hawezi kushindwa ubunge hasa spika wa bunge la Tanzania haijawai na haitaruhusiwa kutokea.Sina Mengi ni hayo TU.
Kwamba mtamsaidia kuiba kura kama mlivyofanya 2020, au?!
 
Kwamba mtamsaidia kuiba kura kama mlivyofanya 2020, au?!
Hakuna Spika wa Tanzania anaweza kushindwa ubunge kuanzia CCM ndani mpaka nje kipi ambacho hakieleweki, Biteko atashinda TU ubunge kama atagombea, Tulia atashinda TU kama atagombea, Samia atashinda kama atagombea.
 
Kuna tetesi mmoja atagombea popote atakapogombea mwenzake katika hayo majimbo mawili endapo yakigawanywa..
😀😀😀
Mgawanyo wa majimbo (kama upo) ufanyike 'sasa' ili kila mtu ajijue anaangukia wapi!
 
'The IPU Governing Council elects the IPU President for a term of three years. He or she must be a sitting Member of Parliament throughout the term of the presidency'

Leo Tulia Ackson amechaguliwa kuongoza umoja wa mabunge duniani kwa kipindi cha miaka mitatu. Moja ya sifa ya kuendelea kuwa rais wa umoja huo ni kubaki kuwa mbunge kwa kipindi chote cha muhula wake wa miaka mitatu.

Tanzania inatarajiwa kuingia kwenye uchaguzi mkuu miaka miwili ijayo, Tulia atakuwa amebakisha mwaka mmoja kwenye muhula wake wa Urais IPU. Ukiachana na uchaguzi wa 2020, Sugu amekuwa na rekodi nzuri ya matokeo Mbeya mjini huku mwaka 2015 akizoa kura nyingi mpaka kuwa mbunge wa kwanza aliyechaguliwa kwa namba kubwa ya kura Tanzania nzima.

Mwaka huu wa 2023 wawili hao wamekuwa wakirushiana vijembe kila mmoja akitamba kumgaraza mwenzake uchaguzi wa 2025 huku Dkt. Tulia akianza na Sugu kujibu mapigo.

Uchaguzi wa ubunge jimbo la Mbeya Mjini umetiwa ndimu na chumvi! Tusubiri 2025..


Pia, soma=> Dkt. Tulia Ackson ameshinda Urais wa IPU kwa kishindo, apata kura 172 kati ya 303
Sio mlungula kweli maana hawaaminiki
 
Kuwa rais IPU, haikufanyi uwe na tiketi ya uhakika ya kubaki bungeni kwa kura za wananchi, matakwa ya IPU Sio matakwa ya watu wa Mbeya. Watu wa Mbeya wanataka kiongozi atakaye timiza haja za Wana Mbeya, na sio habari za IPU. IPU haitatui shida za wanambeya.
CCM wataongeza nguvu kutetea kiti cha ubunge Mbeya mjini, rekodi huko nyuma zinaonesha CCM huwa wanashinda sehemu ambazo hamna mtu alitarajia watashinda..
 
Jimbo linagawanywa Mkuu. Tulia anapewa la kwake na Sugu naye anapewa la kwake. Hivi ndivyo tunavyoishi Watanzania na mihimili yetu.

Ova
Kwa pesa zipi za kugharamia??
 
Dkt. Tulia hawezi kumshinda Sugu labda Viongozi wa CCM kuanzia Rais, Makamu wake, Waziri Mkuu na viongozi wengi wapige kambi Mbeya kwa miezi mitatu wakimpigia kampeni hapo anaweza kumshinda Sugu vinginevyo hiyo ni ndoto ya alinacha. Mpiga kura hajui what is IPU na ina faida gani kwake.
 
Sugu hawezi kushinda Mbeya atakama Dr. Tulia asingekuwa Rais wa IPU
 
Mkuu, tuacheni kujidanganya. CCM bila vyombo vya ulinzi na usalama kwwnye box la kura hawatoki, na wao wanajua kabisa hili.

Mbeya Tulia hatoboi bila polisi na NEC.
 
Back
Top Bottom