Sugu na Jide ni wasanii wasioguswa, ukiwagusa umepotea kimoja, pitia hapa ushuhudie

Sugu na Jide ni wasanii wasioguswa, ukiwagusa umepotea kimoja, pitia hapa ushuhudie

Hili si kweli hata kidogo unless wewe umemjuwa Sugu wakati anaimba mambo ya feza na Jide, lakini kipindi anatembea na Cd yake mkononi yenye beat na anaomba kupewa nafasi ya kuperfom bila hata kupewa mia hukumjuwa.

Na kama ulikuwa hujui maisha ya mshkaji amesurubika mno na watu wa aina yake Mungu huwafuta machozi na kwa nini alifanikiwa kutoa albam alikuwa anatumia pesa anayopata kazini kwake BP kulipia studio Don bosco akipeleka master kwa wadosi anaambulia laki mbili tu.

Sugu mziki upo kwenye damu hawezi kuacha game maana mashabiki wake tupo wengi maana kwake mashabiki(fans) ndio swala la msingi kwake! Jamaa namkubali sana kwenye hustle zake za kitaa!! Hustle hustle hard! Cha msingi no turning back ni kusonga kwa mwendo wa farasi au kinyonga!
 
Aaah wapi!!! Jide toka enzi zileee....hata hili halihitaji ushahidi.

Nakubaliana na wewe Avemaria kuwa jide kawa maarufu kitambo! Je mifarakano na watu haijamsaidia? Na huyo Chid amepotezwa vipi na Jide? Mwana FA kapotezwa vipi? Mbona anatoa muziki mzuri? Mbona anapiga show? Mbona Clouds media wanafanya biashara vizuri kama zamani? Ni nani kapotezwa?
 
Last edited by a moderator:
Kuna track waliimba pamoja kati ya Jide na Chid unaitwa upo Juu,inaonekana baada ya ku-hit huo wimbo chid benz akaanza kuleta mapozi kwenye kushoot video mara ana-demand anunuliwe nguo mara apangiwe hotel mara alipwe kiasi kadhaa yani full complication kina Gadner na jide wakaona isiwe shida wakakata audio yake kwenye ile video wakaweka wacheza show basi video ikaruka hewani baada ya kupotezewa ndio akaanza bla bla nyingii na beef likawa juu.

Kwa hiyo baada ya kutokea beef ndio Chid akapotezwa? Kwa hiyo Jide ndio sababu ya Chid kutofanya vizuri kimziki miaka minne sasa?
 
Hili si kweli hata kidogo unless wewe umemjuwa Sugu wakati anaimba mambo ya feza na Jide, lakini kipindi anatembea na Cd yake mkononi yenye beat na anaomba kupewa nafasi ya kuperfom bila hata kupewa mia hukumjuwa.

Na kama ulikuwa hujui maisha ya mshkaji amesurubika mno na watu wa aina yake Mungu huwafuta machozi na kwa nini alifanikiwa kutoa albam alikuwa anatumia pesa anayopata kazini kwake BP kulipia studio Don bosco akipeleka master kwa wadosi anaambulia laki mbili tu.

Hayo yote nakubaliana na wewe kabisa!
Lakini ambacho kimewashinda ni kuonesha ni akina nani wali wagusa hao (Jide na Sugu) wakapotezwa?
Na walipotezwa vipi?
 
Aisee ayo maswali yako kama tupo mahakamani sasa... Hapa nafikiri wameongrlea. ishu za kijamii zaidi sio kisheria mpaka mtu alete ushahidi..

Maana Jide ni maarufu nadhani tangia Chidi yupo primary school sasa ayo ya baada ya kutongoza ikawaje mie nitakuwa nasema uhongo ila walishafanya wimbo pamoja unaitwa Mpo juu na video Chidi hakuwekwa.

Ni kama watu wa siasa wanavyosema ukitaka kupiga siasa zako bila kuharibu basi usimdiss Nyerere na kweli tunaona watu waliomgusa Nyerere walishindwa siasa. Sasa aya ni mambo ya. kijamii zaidi ayaitaji facts kama we unavyotaka. Na nadhani ndio wanachosema washikaji hapa.

Ni kweli mambo ya kijamii hayahitaji facts? Mi nafikiri mnatakiwa kumsaidia mtoa mada ni jinsi gani hao aliowataja wamepotezwa?
Clouds hadi Leo wanafanya biashara vizuri!
Mwana FA hadi Leo ana Fanya vyema na anapata show.

Labda nikuulize Jide ndio alikuwa sababu ya Chid kupotea kwenye ramani ya muziki?
 
Nimemuelewa mtoa maada unajua alio wataja kupotea hata kama hawajapotea kwa ukubwa lakini sio sawa na wasingetofautiana na hao watu unajua mziki ni biashara na kanuni ya biashara ni pamoja na kupata uzoefu kwa wazoefu na walio tajwa hapo kwenye mziki ndio haswa wazoefu kwahyo unapo kosana nao mziki wako utaenda lakini sio sawa na ungekua peace Nao. Kama huamini Leo ukiwa star kosana na dimond huwezi athilika sawa na ukikosana na jide,sugu, professor jay, ay, n.k nilimuekewa hivyo jamani kwa mziki Wa Ben pol hakuna dababu ya kutokua juu tena juuuuuuu zaidi.
 
Kwani nani kakwambia msanii hatakiwi kuwa mtu mzima? Unaonekana wee ni mtoto! Kuwa kwanza akili yako ijuwe mambo.

We unakua kama kizazi cha Mulugo mi nasema kua jide ni mtu mzima kakomaa ila anaficha umri wake,
Hujaelewa nini sasa hapo.
 
Emi kumbe wa 72 aisee kumbe kikubwa hivyo? Ila Jide atakuwa kwenye 78 hivi 72 hajafika uko.

Eminem mkongwe ila Jide hakosi miaka 40 hapo tumempunja, cheki sura ile.
Ila yeye hatakagi kukubali kua umri umeenda yeye ni mtu mzima sasa.
 
Kama jide kuwa na uso ulokomaa ni shida .....ina maana wewe hautokua???
Some people bhana, growing old is mandatory hata wewe muda ukifika shavu litakushuka tu na sura itakakamaa kwa sana.

We umetumwa nini??
Ishu kubwa hapa sio kukomaaa, ishu kubwa hapa ni yeye kua mtu mzima lakini kutokubali ukweli na kukataa miaka yake,
Ni kama yule miss tz wakati anapewa umiss mwaka 2006 alikua amenizidi umri lakini sasa hivi nashangaa eti mimi ndo nimemzidi umri
 
We unakua kama kizazi cha Mulugo mi nasema kua jide ni mtu mzima kakomaa ila anaficha umri wake,
Hujaelewa nini sasa hapo.

Tupe ushaidi ni kivipi Jide anaficha umri wake na wapi alitaja umri wake akaongopa na wewe tuthibitishie Jide kazaliwa mwaka gani? Otherwise JF si kijiwe cha wapiga porojo na majungu.
 
Nimeshangaa pia, hoja ya kitoto sana, unajua mtu akiishiwa maneno ataongea tu ilimradi

We taaira kweli nyie ndo wale wale umri umeenda afu hamjafanya chochote cha maana sasa mnaficha aibu kwa kudanganya miaka ili muonekane watoto.

Fainali uzeeni.
 
Tupe ushaidi ni kivipi Jide anaficha umri wake na wapi alitaja umri wake akaongopa na wewe tuthibitishie Jide kazaliwa mwaka gani? Otherwise JF si kijiwe cha wapiga porojo na majungu.

Nikupe ushahidi we ni mahakama,
Acha tabia za kimchele mchele viuno mbelembele.
 
Siku zote kujitambua ni silaa,hawajakubali kutumika leo wanafaida vya kwao.bye bye vibaraka
 
We unakua kama kizazi cha Mulugo mi nasema kua jide ni mtu mzima kakomaa ila anaficha umri wake,
Hujaelewa nini sasa hapo.
Nani kakwambia umri wake ni matangazo ya biashara? Na unataka umri wake wa nini? Ukishaujua ukusaidie nini? Nyie ndo wambea na wanafiki, badala ya kufikiria mambo ya maana unafikiria private information. Kwendreeaaah huko
 
Back
Top Bottom