Wakati huo Sugu amepanga chumba mbagala na ni mlinzi wa getini BP ajira ambayo alikuwa akipata kipato kizuri sana kutokana na mishemishe za wese,
Kabla ya kupata lidandasi aligunduwa hawezi kufika popote bila kujichanganya na watoto wa kishuwa upanga ndio akajichanganya Don Bosco na kupiga story na kwanza Unity na baadaye Sugu alijumuishwa kwenye kundi la Diplomatz na king Saigon na Balozi lakini yeye akiendelea na Solo project zake kabla xa kwenda kupiga box UK.
Na hapo ndipo ilipotokea hujuma kabla Clouds fm haijaanzishwa na Radio one walikifuta rasmi kipindi cha Rap cha kila ijumaa ambacho kilikuwa chini ya Mike Mhagama hii ilikuwa ni kabla ya mwaka 95 na ndio 2 proud katika mistari aliwachana redio one kwamba yeye alianza kurap kabla ya Fm na watu walimfahamu.
Jide nilianza kumsikia yeye na Ray C wakiwa watangazaji wa clouds na baadaye wakatoa single zao, hakuna mwanabongo fleva nchi wa kumfananisha na Sugu, huyu ni Die harder.
Kama unafuatilia Bongo hiphop kuna vichwa vya ukweli lakini vimeshindwa kukomaa na wamenyoosha mikono juu lakini ni Sugu peke yake aliweza kukomaa.
Angalia hard blasters, Kwanza Unity, LWP, Wateule, Source B, Unique Sisters, Skwiza na dada yake huu ni mfano wa vipaji vilivyopotezwa na mfumo wa muziki wa Bongo.