Sukuma Gang is Real: Waanza kumtisha Rais Samia, wamtumia Msukuma kudai mkoa wa Chato kinguvu

Sukuma Gang is Real: Waanza kumtisha Rais Samia, wamtumia Msukuma kudai mkoa wa Chato kinguvu

Kwani kuna shida gani chato ikiwa mkoa? Mbona mnapenda kukuza mambo kijinga yaonekane yanamaana sana? Mnaacha kuoambania mindege inayotua huko Loliondo mnapambana Chato usiwe mkoa!
Kutaka Chato kuwa mkoa ni mawazo ya kijima
 
Chato haina ardhi kwa hiyo wilaya iko angani?Russia na china huwezi kuzifananisha na Tanzania, hakuna uwiano. Kwanini usitolee mfano wa nchi za afrika mashariki na kati?kwa hali yoyote ile mm naunga mkono chato kuwa mkoa kwa maslahi mapana ya wananchi wanafuata huduma mbali(makao makuu ya mikoa).
Kwanini usiombe huduma kusogezwa kama ziko mbali badala ya kuomba upumbavu?
 
Hili kundi sio la kufikirika lipo na litamtesa sana mama Samia.

Nipo kanda ya Ziwa kiukweli mama yangu Samia huku watu hawakupendi kwa sababu mbili.

Watu wa huku wana mfumo dume hawaamini kama mwanamke anaweza kuwa Rais.

Pili ni wivu tu na roho mbaya,wanaona kama wewe unafaidi matunda ya mwenazake bure

Hawaamini kama utaendeleza miradi ya mwendazake aliyoianzisha kanda ya ziwa.

Kuna mikoa kama Geita hususan wilaya ya Chato imerudi nyuma kimaendeleo,enzi za mwendazake ikulu ilihamia Chato,mzunguko wa hela ukawa mkubwa,sasa hotel za Chato ni makazi ya popo, mji umepooza dorooo.

Sasa wameamua kumtikisa Rais wetu mpendwa mama Samia kwa kudai mkoa wa Chato,katika hili wanamtumia Dk Msukuma kumtisha mama.

Chato haina ardhi wala hadhi vya kuwa mkoa, huo ndio ukweli,mama simamia haki.nadhani ifike muda sasa mambo ya kutengeneza mikoa mipya ywfike tamati.

China USA na Russia ni kubwa ila hawana ujinga huu,kikubwa serikali ipeleke huduma bora kwa wananchi basi kwa kuzisogeza karibu.

Mwisho Sukuma Gang waambiwe kuwa mama yetu Samia yuko pale kitini kwa sababu ya katiba,na waambiwe kuwa Hayati Magufuli aliitwa na Bwana Mbinguni kwa mapenzi yake,
Tutulie tujenge nchi
,waache nongwa.
Mbona mama aliagiza wahusika watazame vigezo kama chato inakidhi kuwa mkoa.sasa kama vigezo havikupatikana kosa la mama liko wapi?Na wanamtisha nani?
 
Back
Top Bottom