Suluhisho la Kudumu la Kero Zote za Muungano, na Dawa ya Kutibu Sumu ya Ubaguzi wa Utanganyika na Uzanzibari ni Kuwa na Serikali Moja ya JMT?

Yes upigiwe kura, kabla ya kura maza na watu wake warudi kwao
Hakuna ugomvi hapa
Watu wa Nchi hizi ni ndugu moja, kinachotafutwa ni kuziondoa tu zile zinazoitwa kero za Muungano ambazo ni pamoja na muundo wa Muungano 👁
Tanzania ni Muungano wa Nchi mbili Tanganyika na Zanzibar 👁

Hakuna ugomvi hapa 👁😇🤠
 
Kwanini tujiulize maswali wakati tuna majibu.
 
"Muungano tutaulinda kwa gharama yoyote"! Mnaosema mtaulinda kwa gharama yoyote ni wachache ambao hamuitaki katiba! Na kutoitaka katiba ndiko kunakowafanya akina Mwinyi kuwa marais bila kuwa raia wa nchi husika! Tunaishi kwa kitumia dola badala ya katiba!
 
Mmmh. 👁😳😷
 
Ila Mzee unajitutumua sana....kutetea kitu Cha hovyo..ambacho kamati zote zilizoundwa ziliukataa..... Tume ya Nyalali ,Kasanga, Warioba ...hata wazanzibar wenyewe hawaitaki ..ila umeshikana nao tu ....Wakukumbuke aseeee....... Kama ni endorsements wakupe mapema kama teuzi pia wakupe Ili angalau upunguze kutujazia server. Mungu akubariki akili zako zile tulizo kufahamu nazo zikurudie.
 
kweli na kweli tupu!
 
Suluhisho ni serikali tatu,serikali moja Zanzibar hawaikubali hata kwa mtutu.
Ikishindikana Muungano uvunjike kila nchi irudi kama zamani wala tusidanganyike na utabiri uchwara wa mtu fulani aliyekuwa na lengo la kuabudiwa milele,Watanganyika na Wazanzibar tusiwe waabudu mzimu tukaogopa kufanya maamuzi tunayoona yanafaa kwa sasa.
 
Wakati ule watu wa pande zote mbili hawakuulizwa wanatakaje ,
Sasa ni muhimu watu wa hizo pande mbili wakaulizwa wanataka Muungano wa aina gani 👁😇
Sasa hivi sehemu kubwa ya watu wa upande mmoja (Zanzibar) wanaishi, kuendeleza maisha kisiasa na kiuchumi sehemu ya pili, hata kupata nafasi za uongozi hadi ile ya juu kabisa katika utawala.
Katika hali kama hiyo, kuulizana unatakiwa muungano wa aina gani ni kuzua migogoro na kupoteza muda, serikali moja inawezekana hata kesho asubuhi kukiwa na utashi wa kisiasa.
 
Wazo la kuwa na Serikali moja lilikuwa ni wazo la Karume lakini Nyerere ali
Your browser is not able to play this audio.

likataa!
Nadhani hapo ndipo Nyerere alipokosea!
 
Huu muungano una miaka 60 tumeshindwa kuwa na serekali Moja, Leo ndio mnalazimisha tuwe na serekali 1 wakati kizazi hiki hakiutaki huo muungano? Wanzanzibar ni dhahiri hawautaki muungano na huko mbeleni tutakuja kuingia kwenye uhasama usio na sababu. Huu muungano ni koti la kuuzima, na hapa lilipo limeshatubana, ni wakati wa kuvua.
 
Paskali,unavyong'ang'ania kwamba watu hawana elimu ya uraia,unakosea.Kuna uwezekano wewe ndiye umepewa elimu hiyo lakini haijajihifadhi sehemu njema kichwani mwako.Kwa ufupi haujaelewa kitu.Bado una safari ndefu ya kulishwa kwa nguvu kuhusu demokrasia na uhuru wa maoni.Naishia hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…