Suluhisho la Mfululuzo wa Matatizo ya Uwanja Wa Benjamin Mkapa: Ubinafsishwe kwa Sekta Binafsi

Suluhisho la Mfululuzo wa Matatizo ya Uwanja Wa Benjamin Mkapa: Ubinafsishwe kwa Sekta Binafsi

Stuxnet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2011
Posts
13,417
Reaction score
23,310
Ni miaka inakaribia 20 toka Uwanja wa Taifa maarufu kama Benjamin Mkapa Stadium, au Kwa Mkapa au Lupaso uzinduliwe, tumeshuhudia mfululizo wa matatizo mengi hususan makubwa kama yafuatayo;

1. Kuvunjwa kwa viti vya kukalia kutoka kwenye majukwa ya moja ya timu kubwa

2. Kuvunjika kwa milango na masinki ya vyoo kwenye sehemu za kujihifadhi

3. Kuchakaa kwa pitch ya kuchezea mpira kutokana na ukosefu wa maji

4. Watazamaji kuvunja geti na kuingia bila utaratibu

6. Kukatika kwa umeme wakati wa mechi za kimataifa ikiwa ni ni pamoja na tukio la kwenye mechi ya jana kati ya Yanga na Rivers ya Nigeria

Tukubaliane tu kuwa Waafrika hasa Watanzania hatujui thamani ya raslimali (sense of value) tuliyonayo ndiyo maana tunaharibu kwa makusudi au kwa ujinga tu (bad mindset)

Serikali duniani kote hasina ufanisi kwenye menejimenti ya taasisi kama hizi.

Nashauri Serikali IBINAFSISHE usimamizi wa uwanja huu kwa kupitia zabuni ya wazi. Serikali ibakie kukusanya maduhuri yake na kodi za kisheria.

Nawasilisha
Screenshot_20230501_103456_Google.jpg
 
Usiwaze hivyo. Pole kwa uchungu ndugu.

Hii inapaswa watendaji wawajibishwe tu aidha wanaohusika waondolewe au waachishwe kazi. Itategemea na uamuzi wa wahusika.
 
Nadhani mapato ya uwanja yabaki kwa ajili ya operation za uwanja, ukiondoa yale yanayoenda TRA na kwenye timu.

Mapato yote yaingue kwenye special fund, Kila mwisho wa msimu inafanyika ukarabati mkubwa.

Hata kama si fedha yote, basi angalau a percent.

CAF wanasema viti vibovu, nashauri viondolewe vyote, tununue quality itakayodumu 20-30 years.

Tubadili taa zote.
Vyumba vya wachezaji na maafisa vifanyiwe mabadiliko makubwa, vyoo vifanyiwe ukarabati, Kila sehemu, hata kama utachukua bilioni 5 au 10
 
Usiwaze hivyo. Pole kwa uchungu ndugu.

Hii inapaswa watendaji wawajibishwe tu aidha wanaohusika waondolewe au waachishwe kazi. Itategemea na uamuzi wa wahusika.
Kuwajibisha watendaji ni short term hata mimi naikubali hatua hiyo ambayo Serikali imechukua.

Lakini kuondokana na hizi micromanagement za uwanja, nakubaliana na mtoa mada kuwa uwanja wa Taifa ubinafsishwe tu. Sekta binafsi ipewe malengo ya mapato, utunzaji na uwekezaji na serikali.
 
Ni miaka inakaribia 20 toka Uwanja wa Taifa maarufu kama Benjamin Mkapa Stadium, au Kwa Mkapa au Lupaso uzinduliwe, tumeshuhudia mfululizo wa matatizo mengi hususan makubwa kama yafuatayo...
Hili nilishalipigia kelele toka mwanzo uwanja unazinduliwa. Sisi watz ni watu wa ovyoovyo.
 
Uwanja ulitembelewa na Balozi wa Urusi akiwa na Waziri Chana na waliahidi kusapoti katika uboreshaji wa uwanja na huduma. Au zilikuwa siasa za wakomonisiti wawili dhidi ya ujio wa Kamala Harris
 
Uwanja ulitembelewa na Balozi wa Urusi akiwa na Waziri Chana na waliahidi kusapoti katika uboreshaji wa wa uwanja na huduma. Au zilikuwa siasa za wakomonisiti wawili dhidi ya ujio wa Kamala Harris
Kuna vitu vyakuhitaji msaada wa nchi za nje lakini sio uwanja jamani!.
 
Kuwajibisha watendaji ni short term hata mimi naikubali hatua hiyo ambayo Serikali imechukua.

Lakini kuondokana na hizi micromanagement za uwanja, nakubaliana na mtoa mada kuwa uwanja wa Taifa ubinafsishwe tu. Sekta binafsi ipewe malengo ya mapato, utunzaji na uwekezaji na serikali.
Swali ni kipi tumebinafsisha kikafanya vizuri?
 
Hadi hapo kila kitu sasa kibinafsishwe, kuanzia halmashauri hadi wizara.
Kwa kuwa hazifanyi vizuri pia
 
Hili nilishalipigia kelele toka mwanzo uwanja unazinduliwa. Sisi watz ni watu wa ovyoovyo.
Ni kweli kabisa Watanzania hatuna ustaarabu na hatuwezi kujifunza kuthamini vitu. Hii hali iko hata kwenye mabasi ya MWENDOKASI. Angalia mabasi mle ndani yalivyo, angalia hata vituo vya Mwendokasi namna vimechakaa
 
Usiwaze hivyo. Pole kwa uchungu ndugu.

Hii inapaswa watendaji wawajibishwe tu aidha wanaohusika waondolewe au waachishwe kazi. Itategemea na uamuzi wa wahusika.
Kuwajibishwa ni moja ya adhabu lakini suala ni kwamba kwenye utendaji wa Serikali hakuna efficiency. Privatise management halafu serikali ikusanye kodi na commission tu au kodi
 
Hili nilishalipigia kelele toka mwanzo uwanja unazinduliwa. Sisi watz ni watu wa ovyoovyo.
Nakabaliana na wewe Watanzania hatuna maadili ya kusimamia raslimali zetu. Tumeliona kwenye mashirika ya umma yalivyokufa
 
Serikali imetangaza kuanza Ukarabati wa Uwanja wa Taifa "Uwanja wa Mkapa" kwa gharama ya Tshs. Bilioni 30. Uwanja huo haujakarabatiwa kwa miaka 16 tangu uzinduliwe

Marekebisho makubwa yamepangwa kufanyika ikiwemo kubadilisha viti vyote, kubadilisha mifumo ya Taa, Stadium TV Screen, Eneo la kukimbilia na kuweka Mabenchi ya Kisasa ya Wachezaji
 
Serikali imetangaza kuanza Ukarabati wa Uwanja wa Taifa "Uwanja wa Mkapa" kwa gharama ya Tshs. Bilioni 30. Uwanja huo haujakarabatiwa kwa miaka 16 tangu uzinduliwe

Marekebisho makubwa yamepangwa kufanyika ikiwemo kubadilisha viti vyote, kubadilisha mifumo ya Taa, Stadium TV Screen, Eneo la kukimbilia na kuweka Mabenchi ya Kisasa ya Wachezaji
Nashangaa kwa nini mpaka leo hatuwezi kuingia Mkapa Stadium kwa tiketi inayoonyesha seat namba yako na ukakaa kwenye seat hiyo.

Hata mimi naamini angepewa mwekezaji binfasi tungekaa level siti kama kwenye Shabiby ya kwenda Dodoma
 
Back
Top Bottom