Suma Lee atoa elimu nzito katika post yake ya msiba wa msanii Jebby

Suma Lee atoa elimu nzito katika post yake ya msiba wa msanii Jebby

Hayo mambo yoooote yameelezwa Kwenye vitabu, usifkiri kama ni maneno yametungwa au kifikiriwa, KUNA HABARI NZITO NDUGU YANGU BAADA YA KUFA, fanya mema, omba msamaha kwa mola wako NDUGU.
Pia yapaswa kuamini kile ambacho unakiamini, maana imani yako ndio hukuponya.
 
Mungu hashindwi kufanya kitu chochote, JIULIZE ww amekuletaje huku DUNIANI ashindwe kukufufua tena upya na kakuhukumu kulingana na wema au makosa yako???
Kufufuliwa na Mungu ni jambo rahisi sana kwake je ikiwa hujafika kaburibi ugarudishiwa roho labda uko porini tu itakuwaje ukipiga kelele maana utaamka, tumesoma hiv
 
Hata Yesu alivofufuka hakutuambia kifo kiko vipi, Nadhani aliona Haina Haja kutuambia. sasa sijui wanaotuambia wanaonaje hili swala.
 
Hayo mambo yoooote yameelezwa Kwenye vitabu, usifkiri kama ni maneno yametungwa au kifikiriwa, KUNA HABARI NZITO NDUGU YANGU BAADA YA KUFA, fanya mema, omba msamaha kwa mola wako NDUGU.
Kwenye vitabu gani? Mimi kwa imani yangu naamini kuna hukumu baada ya kifo, lakini siamini hizo 'procedures' alizosema hapo.
Ila kama kwenye imani yake wanaamini hivyo basi hamna shida.
 
Naona udini unatawala, nasisitiza Hakuna Dini itakayo mpeleka mtu kwa mwenyezi Mungu, bali matendo.Kuna wapagani wenye matendo mema Kama kusaidia wahitaji, hawanyooshei watu vidole. Hakuna watu wabaya Kama wanaojifanya kuijua dini, 98%unafiki mtupu
 
Naona udini unatawala, nasisitiza Hakuna Dini itakayo mpeleka mtu kwa mwenyezi Mungu, bali matendo.Kuna wapagani wenye matendo mema Kama kusaidia wahitaji, hawanyooshei watu vidole. Hakuna watu wabaya Kama wanaojifanya kuijua dini, 98%unafiki mtupu
Matendo bila Imani[emoji18] [emoji18]
 
je ikiwa umedondoka tu porini na hujafukiwa ukirudishiwa roho na kuamka vipi ukipiga kelele?? maana porini huzikwi utaoza had kuisha kabisa na kusalia mifupa.

Nadhani hii ni nadharia kifo ni siri nzito sana.
Mkuu porini ukirudishiwa ROHO na ukapiga kelele omba mungu SIMBA asiwe maeneo ya karibu,akikukuta itakua the END ,ukiona umerudishiwa roho porini we sepa kimya kimya yasije ya kakukuta makubwa zaidi
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Ujumbe murua sana huu,ukiupenda basi uzingatie na kutimiza uliyoshauriwa,ukiona haukufai basi uache,dini ni imani na matendo mema,halazimishwi mtu,binadamu tumepewa akili ya kutambua na kutafakari mambo.
 
INNA LILLAH WA INNA ILAIHI RAAJIUUN
[HASHTAG]#JEBBY[/HASHTAG]

UNAVYO JIHISI KIFO.
Mtu huwa hatambui kuwa amekufa pale anapokufa. Yeye hujihisi anaota anakufa, anajihisi analia, anaoshwa, anafungwa na anateremshwa kaburini. .

Bado anajihisi kuwa anaota anapofunikwa na mchanga. Kisha hulia kwa makelele na hakuna anae msikia.
Baadae kila mtu anapotawanyika na ameachwa pekee chini ya ardhi, Mungu huirudisha roho yake. Anafungua macho na kuamka kutoka "ndoto yake mbaya" .
Mwanzoni, hufurahi na kushukuru kuwa alikuwa anaota tu, na sasa ameamka kutoka usingizini. Kisha hujigusa mwili wake ambao utakuwa umefunikwa na kitambaa cheupe,na kwa mshangao hujiuliza "shati/gauni langu liko wapi?"
Kisha ana anza kujihisi "niko wapi?" "hii ni sehemu gani?" Mbona kuna harufu ya udongo kila mahali? Ni nini haswa ninacho kifanya hapa?
Hapo ndipo atakapo anza kugundua kuwa yuko chini ya ardhi na alicho kihisi haki kuwa ndoto!
Ndiyo, anagundua kuwa ni kweli yeye amekufa, na amezikwa. .

Anapiga kelele kadri anavyoweza kuwaita watu waliokuwa karibu nae ambao wangeweza kumuokoa:
"baba"
"mama"
"kaka"
"dada"
"rafiki"

Hakuna anaemjibu. Kisha anagundua kuwa Allah ndio tegemeo lake pekee. Akilia na kumuita huku akimuomba msamaha :
"Yaa Allaaaaah...
Yaa Allaaaaaah...
Nisamehe mimi
Yaa Allaaaaaah!!! .

Anaita akiwa na hofu kubwa,ambayo hakupata kuwa nayo alipokuwa hai . .

Kama alikuwa mtu mwema na mcha Mungu, malaika wawili wakiwa na uso ulio na furaha watamkalisha na kumliwazana kumhudumia vizuri. .

Kama alikuwa mtu mbaya na hakuwa mcha Mungu, malaika wawili watamwongozea hofu yake na kumpa mateso kufuatana na amali zake mbaya. .

Ewe Mola, nisamehe dhambi zangu, dhambi za baba yangu, mama yangu, mke/mume wangu na wanangu na jamaa zangu na marafiki. .

Ewe Allah, usiuchukue uhai wangu ila pale nitakapo kuwa tayari kukutana nawe.

Kaka na dada katika uislam,una chaguo mbili hapa:

#1.Uache ilimu hii hapa isomwe na hakuna kitakacho tokea.

#2.[HASHTAG]#TAg[/HASHTAG] Isambaze ilimu hii kwa marafiki zako,.na wote wengine.
In Sha Allah itakuwa na manufaa kwao, na wewe utafaidika.
Ameen.
NB😛ichani ni Suma lee akiwa na msanii mwenzake marehemu Jebby.View attachment 754546
Adhabu ya kaburi aijuaye maiti, yeye kajuaje..
 
lengo la Sumalee watu watende mema sio kwamba ukifa utahisi unaota mara utapiga kelele
 
Kwahyo maiti ikifufuka kaburini, halafu inakufa tena kwa kukosa hewa na chakula
 
Back
Top Bottom