Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
MAELEZO KUHUSIANA NA HUDUMA YA MAJISAFI KWA KATA ZA MTAMAA NA UNYIANGA NA MANISPAA YA SINGIDA KWA UJUMLA
Kata za Unyianga na Mtamaa ni mojawapo ya maeneo ambayo yana uhitaji wa kusogezewa huduma ya majisafi katika Manispaa ya Singida na Serikali inatambua hilo na imeshachukuwa hatua stahiki.
Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na: Katika kipindi cha muda mfupi, Serikali inatekeleza mradi wa maji wa Visima 900 ambapo Manispaa ya Singida ina visima vitano na kisima kimoja kinachimbwa Unyianga na cha pili kinachimbwa Mtamaa na kazi inaendelea.
Aidha, katika mradi wa majisafi wa Miji 28 ambapo kwa Manispaa ya Singida unagharimu kiasi cha shilingi bilioni 42, tayari Mkandarasi yupo site na tayari ameshachimba visima Mtamaa B ambapo visima viwili vina uwezo wa kuzalisha maji wastani wa lita 35,000 na 45,000 kwa saa.
Vilevile mradi huo utajenga matenki matano ya maji ambapo tenki mojawapo linajengwa Unyianga baada ya vyanzo kukamilishwa.
Mradi wa majisafi wa Miji 28 kwa Manispaa ya Singida unajumuisha kazi za uchimbaji visima kwa lengo la kuongeza uzalishaji maji kwa siku wa sasa kutoka lita milioni 10.5 hadi kufikia lita milioni 28 kwa siku, ulazaji wa mabomba kwa urefu wa kilomita 55 na ujenzi wa matenki matano ambapo kata za Mtamaa na Unyianga zinanufaika na mradi huu mkubwa na wa kihistoria kwa Manispaa ya Singida.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano - SUWASA
24 Desemba 2024
Pia soma ~ Wananchi wa Unyianga Singida na shida ya maji
Kata za Unyianga na Mtamaa ni mojawapo ya maeneo ambayo yana uhitaji wa kusogezewa huduma ya majisafi katika Manispaa ya Singida na Serikali inatambua hilo na imeshachukuwa hatua stahiki.
Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na: Katika kipindi cha muda mfupi, Serikali inatekeleza mradi wa maji wa Visima 900 ambapo Manispaa ya Singida ina visima vitano na kisima kimoja kinachimbwa Unyianga na cha pili kinachimbwa Mtamaa na kazi inaendelea.
Vilevile mradi huo utajenga matenki matano ya maji ambapo tenki mojawapo linajengwa Unyianga baada ya vyanzo kukamilishwa.
Mradi wa majisafi wa Miji 28 kwa Manispaa ya Singida unajumuisha kazi za uchimbaji visima kwa lengo la kuongeza uzalishaji maji kwa siku wa sasa kutoka lita milioni 10.5 hadi kufikia lita milioni 28 kwa siku, ulazaji wa mabomba kwa urefu wa kilomita 55 na ujenzi wa matenki matano ambapo kata za Mtamaa na Unyianga zinanufaika na mradi huu mkubwa na wa kihistoria kwa Manispaa ya Singida.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano - SUWASA
24 Desemba 2024
Pia soma ~ Wananchi wa Unyianga Singida na shida ya maji