Swali ambalo Hayati Mwalimu Nyerere aliulizwa na wazungu akajibu kisanii matokeo yake tunayaona sasa

Swali ambalo Hayati Mwalimu Nyerere aliulizwa na wazungu akajibu kisanii matokeo yake tunayaona sasa

Mto Songwe

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2023
Posts
6,683
Reaction score
14,060
SWALI: Nafikiri kuna kama matatizo mawili yanayoikabili Afrika, na hilo ni pengo kati ya mfumo wa kisiasa wa taifa la kisasa na kiwango cha hali ya juu cha ustadi wa kiteknolojia na kiuchumi kinachohitajika katika kutengeneza taifa. Na nafikiri watu wanapozungumzia uhuru kuja haraka sana hawamaanishi kabisa kuwa watu hawako tayari kujitawala. Wanajiuliza, je, wana baadhi ya ujuzi na vifaa muhimu kufanya vizuri tunapoondoka?

NYERERE: Jibu halisi ni kuwa swali hilo halihitajiki kuwepo kabisa na ikiwa umeingia ndani ya nyumba yangu na kuiba koti langu usiniulize kama niko tayari kwa ajili ya koti langu, hilo koti lilikuwa langu. Haukuwa na haki yoyote ya kuchukua kutoka kwangu. Ndiyo, lakini inachukua muda mrefu, inaweza kuchukua muda mrefu kwenda katika mahakama kuu na kukata rufaa na kupata yote haya hadi nipate koti langu tena lakini huna haki yoyote ya kuniuliza kama nilikuwa tayari kwa ajili ya koti langu. Mfumo wa ikiwa, kweli naweza kuonekana vizuri katika koti langu ninapolivaa ni tofauti. Naweza nisiwe na sura nzuri nikiwa nalo kama wewe ulivyo nalo, lakini ni langu....

=====

Wazungu hawa walimuuliza swali hili Nyerere lakini yeye akatoa majibu ya kisanii.

Matokeo ya hili swali tunayaona sasa baada ya miaka 60 kupitia katika mataifa yetu.

Hawa wazungu walikuwa sahihi sana kuulizia za hili swali bila shaka kuna kitu walikiona ambacho yeye Nyerere na wenzake kwa wakati huo hawakukiona.

Mfano mwengine uliohai ni Africa kusini mpira wanarudishiwa makabulu taratibu kwa aibu kubwa.

 
Wazungu hawa walimuuliza swali hili Nyerere lakini yeye akatoa majibu ya kisanii.

Matokeo ya hili swali tunayaona sasa baada ya miaka 60 kupitia katika mataifa yetu.

Hawa wazungu walikuwa sahihi sana kuulizia za hili swali bila shaka kuna kitu walikiona ambacho yeye Nyerere na wenzake kwa wakati huo hawakukiona.

Mfano mwengine uliohai ni Africa kusini mpira wanarudishiwa makabulu taratibu kwa aibu kubwa.
View attachment 3028474
Mtakatifu Nyerere
 
Wazungu hawa walimuuliza swali hili Nyerere lakini yeye akatoa majibu ya kisanii.

Matokeo ya hili swali tunayaona sasa baada ya miaka 60 kupitia katika mataifa yetu.

Hawa wazungu walikuwa sahihi sana kuulizia za hili swali bila shaka kuna kitu walikiona ambacho yeye Nyerere na wenzake kwa wakati huo hawakukiona.

Mfano mwengine uliohai ni Africa kusini mpira wanarudishiwa makabulu taratibu kwa aibu kubwa.
View attachment 3028474
Ulitaka ajibu vipi? Kwamba bado hatujakua tayari kujitawala? Wee ndio wale wamelewa kasumba ya wazungu. Kwani wenyewe unaamini walikua wanatutawala ili tupate uwezo wa kujitawala? Hakika watu ka wewe wanatia huruma kwa ujinga.
 
Nyerere alikua sahihi kwa jibu alilotoa , hata kama alituingiza kwenye mfumo wa ujamaa ! Ila watu wote waliopita kijiti walichoachiwa ndo wametufelisha mpaka hapa ! Hebu angalia kama CCM now yaan haina mvuto hata kidogo , raia tunapangiwa hata wakishindwa uchaguzi wanalazimisha !
Ni wezi , ni wazandiki na wanajipendekeza
 
Pengine hata Nyerere hakuwa ameelika vya kutosha kuwa raisi,
Àliijenga nchi kisiasa Zaidi Kuliko kuwajengea wananchi wake ujuzi sahihi wa Maarifa ya kiuchumi kwenye uvuvi, ufugaji, utalii, Biashara.

Alifanya kila kitu kisimamiwe na serikali ambaye Ndio raisi, kupitia Chama chake.

Hakutaka wananchi kumiliki uchumi, hata kumiliki gar Benz unaonekana kitu cha ajabu, sasa kulikuwa na maana Gani ya kupata Uhuru, wakati wananchi hawana na hawatakiwi kumiliki uchumi wa nchi Yao,

Yani ilifikia kipindi aliyesoma na àsie soma kuwa ni kitu kimoja
 
Back
Top Bottom