Swali ambalo Hayati Mwalimu Nyerere aliulizwa na wazungu akajibu kisanii matokeo yake tunayaona sasa

Watu wengi wakiulizwa maswali kama hayo huwa hawajui ku reject the premise.

Kungekuwa na temptation ya kuonesha kuwa tumejiandaa, tutaweza. Nyerwre angeweza jusema tupo tuliosoma nje tutaongoza nabkusomesha wengine. Lakini hakusema hivyo.

Nyerere rejected the legitimacy of the question.

Ukiielewa hiyo falsafa, ni jambo dogo lakini la msingi sana.

Usipoielewa, ndiyo mpaka mwaka huu 2024 unaona watu wanajiuliza wanashindwa kuelewa. Wengine mpaka leo bado hawamuelewi Nyerere.

Ni falsafa kubwa iliyowapita wasioielewa, halafu ni ndogo sana kwa wanaoielewa.

Ni kama wewe unavyoweza kuona kusema sentensi ya Kiingereza ni kitu kidogo sana, kwa sababu unakijua. Lakini kwa asiyekijua, ni kitu kigumu.

Kuna siku nilikuwa nawaelezea watu, wengine supposedly wasoni kabisa, the logic of elimination method katika kupata majibu ya hesabu. Wale watu wengine walikuwa hawanielewi kabisa. Narudia kwa mfano wa jinsi unavyoweza kufanya elimination ku converge kwenye jibu kutafuta jibu la square root, wale watu wengine bado walikuwa hawanielewi.

Mpaka leo najiuliza, kwa nini watu wengine wanakuwa na shida sana kuelewa mantiki ndogo tu kwangu, halafu wengine wanaelewa kwa urahisi kabisa.
 
Kanyerere nako kalikua kasanii sometime ndio matokeo haya tunayashahudia kwenye ccm yake
Wewe unategemea wazungu wamwambie kuwa mpo tayari kwa uhuru? Yani mtu unayetaka kumpokonya rasilimali zako arudishe kirahisi. Nyerere alikuwa na akili nyingi na amelijibu vizuri kwelikweli. Hakuna siku ambayo tungekuwa tayari. Koti linatukaa vizuri halikai vizuzi ilikuwa ni lazima tulivae kwani ni letu.
 
Huyu Nyerere kaacha viwanda kibao tu, na mashirika ya kutosha. Hao waliokuja baadae ndiyo walikuwa wasanii.
 
walikuibia nini? Walimbaka nani? Waliletaje ugonjwa wa zinaa hapa Tanganyika? waliuletaje?
 
Unajua watanzania tulianza kuvaa viraka kipindi cha Nyerere?
Hivyo viraka vimeisha? Na rasilimali wakati huu zinachukuliwa kwa fujo tofauti na wakati huo kuna jipya. Kulikuwa na ginery kibao zinazalisha mafuta.
 
 
Kabisa ..swali lilikuwa la kushusha spirit ya Nationalism kabisa .
Huwezi uliza swali ka hilo kwa mpigania uhuru .

Mugabe angewatukana.
He he. Walijibiwa ipasavyo.
Huyu aliyeleta huu mjadala, ndio mtukanaji mkubwa hapa. Pamoja na aliouliza maswali awali.
 
Katika uongozi wake wote Mwalimu nyerere hajawahi kuwa na maamuzi yake mwenyewe binafsi bila kufanyiwa na wazungu, kuanzia kabla ya Uhuru mpaka alipokufa.

Sifahamu kwanini hilo linafichwa?

Nyerere katika masharti ya kupooewa uongozi ilikuwa ni lazima afanye kazi zake chini ya mzungu, akipenda sipende. Aliwekewa mwanamke wa kizungu aitwae Joan Wickens kwa muda wote wa uongozi wake, hakuna hotuba ya Nyerere ambayo huyto mwanamke hajaipitia na hakuna maamuzi yoyote ya Nyerere ambayo huyo mwanamke hajayapitia.

Hata alivyokuja Malkia wa Uingereza kuitembelea Tanzania alikuwa na maongezi ya wazi na yasiyo ya wazi na Joan Wickens.
 
Unamaanisha Nyerere alikua kibaraka wa wazungu sie alikua anatuzuga tu.
 
Unamaanisha Nyerere alikua kibaraka wa wazungu sie alikua anatuzuga tu.
Huo ndiyo ukweli, mtafute Joan Wickens na ujiulize kwanini alikuwa Ikulu kabla tu ya Uhuru mpaka kifo cha Nyerere?

Na huyo Joan Wickens ndiye aliifanya Tanzania iwe ma soshalisti. Kwa sababu wanazozijuwa wenyewe Waingereza, sisi tutakisia tu kwa sasa kutokana na mwenendo wa mambo ulivyokuwa.

Nyerere hajawahi kufanya maamuzi mazito bila kupata go ahead ya Joan Wickens.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…