Swali kwa CCM: Ikiwa "makosa" ya Membe, Makamba na Kinana yalihumhusu Magufuli, ilikuwa sahihi kwa Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Kamati iliyowaadhibu?

Swali kwa CCM: Ikiwa "makosa" ya Membe, Makamba na Kinana yalihumhusu Magufuli, ilikuwa sahihi kwa Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Kamati iliyowaadhibu?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Ninaamini CCM wanauelewa msemo kwamba kesi ya kima huwezi kupeleka kwa nyani. Hakutakuwa na haki katika hukumu.

Vivyohivyo, Watanzania wote wanaelewa kwamba tuhuma za CCM dhidi ya Membe, Makamba na Kinana kwa namna kubwa zilikuwa zinamhusu Magufuli.

Membe siku zote ameonwa kuwa mpinzani na tishio kwa uraisi wa Magufuli. Kinana na Makamba walisemwa kuwa waliongea mambo ambayo yalikuwa dhidi ya Magufuli.

Sasa kitu cha ajabu sana kilichotokea, eti kamati ya CCM iliyotoa adhabu dhidi ya Membe, Makamba na Kinana mwenyekiti wake akawa huyo huyo Magufuli!

Hivi tuseme kwamba katika CCM yote hakuwapo mtu mwenye busara kuona hili halikuwa sahihi? Sio suala la kesi ya kima kuipeleka kwa nyani?

Labda hilo mliliona, lakini ukweli ni kwamba mnamwogopa sana Magufuli na kuhofia kupoteza nafasi zenu kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuthubutu kupendekeza au kutoa wazo kwamba isingekuwa vema Magufuli kuwa mwenyekiti wa kamati itakayowaadhibu Membe, Makamba na Kinana kwa kuwa kesi dhidi yao zilimhusu.

Kwanza hebu tutafakari na kwenda mbali kidogo. Huu uamuzi wa kamati ya CCM iliyotoa adhabu ilikuwa ni uamzi wa kamati au uamuzi wa Magufuli? Katika namna ya staili ya utawala wa Magufuli na uoga kwa Magufuli wa viongozi walio chini yake, hivi kuna mtu anategemea mwanachama yeyote wa kamati hii angeweza kutoa mawazo mbadala ikiwa Magufuli alikuja kwenye kamati hii akiwa tayari ameamua uamuzi gani utatolewa?

Na zaidi, ni wazi Magufuli amekuwa akifanya kila jitihada ya kuwazimisha wanachama wote wa CCM waliojitokeza kugombea uraisi dhidi yake mwaka 2015, kuanzia kina Mwigulu, Mwandosya, January Makamba, Membe nk, pamoja na wale wenye kuonyesha dalili za kuangaza kisiasa zaidi yake kwa sasa.

CCM ngoja tuwaambie ukweli, aliyepewa adhabu hapa wala sio Membe, Makamba na Kinana, bali ni nyie CCM wenyewe! Na hadi sasa mkubali kwamba nyie sio tena CCM inayopaswa kuwa Chama Cha Mapinduzi, bali ni CCM inayopaswa kuwa Chama Cha Magufuli.
 
Mzee mkubwa ni namba 6 anazunguka uwanja mzima
tapatalk_1582907846764.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa ndipo palipo na utata.

Jaji au hakimu anahukumu kesi ya anayemtuhum yeye mwenyewe

Conflict of interest must be 100%

Na kisheria hii sio sawa kabisaa sijuwi ccm wanakwama wapi. Haki haijatendeka.
Hapa ndipo unapoona kwamba CCM ya awamu ya tano afadhali ibadili jina iitwe CHAMA CHA MAGUFULI, bado itabaki kuwa CCM.
 
Kikao kilichomfukuza Zitto Chadema Mwenyekiti alikuwa Mbowe ma Katibu alikuwa Dr Slaa ambao wote walikuwa Wagomvi wa Zitto kwa nafasi ya Uenyekiti na ugombea Urais.

Kikao kilichomvua Uanachama wa CUF Prof Lipumba Kiliongozwa na Mtatiro na Seif ambao walikuwa ndio Walalamikaji

Aliekuwa anagawa Fomu za kugombea Urais wa Znz kupitia CUF alikuwa Seif Sharif Hamad ambae pia ndie alikuwa Mgombea wa Milele.

Kikao kilichomfukuzisha Uanachama na hatimae Kufungwa Maisha kwa tuhuma za uongo za Uhaini Marehemu Bibi Titi Mohamed Mlalamikaji alikuwa Nyerere na Mwenyekiti alikuwa Nyerere 1968.

Kwny Siasa hayo ni ya kawaida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Judgement must be realistic, concurrent to the facts with all justice including natural in place.

In this case conflict of interest was not considered as one of the finest and a must in a cause of justices.

CCM majanga
 
Kikao kilichomfukuza Zitto Chadema Mwenyekiti alikuwa Mbowe ma Katibu alikuwa Dr Slaa ambao wote walikuwa Wagomvi wa Zitto kwa nafasi ya Uenyekiti na ugombea Urais

Kikao kilichomvua Uanachama wa CUF Prof Lipumba Kiliongozwa na Mtatiro na Seif ambao walikuwa ndio Walalamikaji

Kikao kilichomfukuzisha Uanachama na hatimae Kufungwa Maisha kwa Uhaini Marehemu Bibi Titi Mohamed Mlalamikaji alikuwa Nyerere na Mwenyekiti alikuwa Nyerere 1968

Kwny Siasa hayo ni ya kawaida

Sent using Jamii Forums mobile app

Daaa hujaelewa kabisa

Who is a complainant in this case?
 
Kikao kilichomfukuza Zitto Chadema Mwenyekiti alikuwa Mbowe ma Katibu alikuwa Dr Slaa ambao wote walikuwa Wagomvi wa Zitto kwa nafasi ya Uenyekiti na ugombea Urais

Kikao kilichomvua Uanachama wa CUF Prof Lipumba Kiliongozwa na Mtatiro na Seif ambao walikuwa ndio Walalamikaji

Kikao kilichomfukuzisha Uanachama na hatimae Kufungwa Maisha kwa Uhaini Marehemu Bibi Titi Mohamed Mlalamikaji alikuwa Nyerere na Mwenyekiti alikuwa Nyerere 1968

Kwny Siasa hayo ni ya kawaida

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama ni hivyo basi tuna tatizo kubwa katika siasa za Tanzania. Hata hivyo, matarajio yetu ni kwamba CCM ni chama kilichokomaa kuliko Chadema, CUF nk. Kama vyama vingine vinafanya upuuzi basi CCM ilipaswa kujipambanua kuonyesha wao wana busara zaidi.

Mkeo akitembea nje ya ndoa na Juma, wewe husawazishi kwa kutembea nje ya ndoa na Mwajuma!
 
2014 Membe alirimamishwa asifanye siasa kwa muda wa mwaka mmoja ikiwa kosa ni kuanza kampeni za urais kabla ya muda na mwenyekiti wa kikao hicho alikuwa Mh Jakaya Kikwete.
 
Kikao kilichomfukuza Zitto Chadema Mwenyekiti alikuwa Mbowe ma Katibu alikuwa Dr Slaa ambao wote walikuwa Wagomvi wa Zitto kwa nafasi ya Uenyekiti na ugombea Urais

Kikao kilichomvua Uanachama wa CUF Prof Lipumba Kiliongozwa na Mtatiro na Seif ambao walikuwa ndio Walalamikaji

Aliekuwa anagawa Fomu za kugombea Urais wa Znz kupitia CUF alikuwa Seif Sharif Hamad ambae pia ndie alikuwa Mgombea wa Milele

Kikao kilichomfukuzisha Uanachama na hatimae Kufungwa Maisha kwa tuhuma za uongo za Uhaini Marehemu Bibi Titi Mohamed Mlalamikaji alikuwa Nyerere na Mwenyekiti alikuwa Nyerere 1968

Kwny Siasa hayo ni ya kawaida

Sent using Jamii Forums mobile app
Two wrongs do not make it right!Au ndio ile mwanao mwizi,mbona wako naye mwizi!
 
2014 Membe alirimamishwa asifanye siasa kwa muda wa mwaka mmoja ikiwa kosa ni kuanza kampeni za urais kabla ya muda na mwenyekiti wa kikao hicho alikuwa Mh Jakaya Kikwete.
Sasa hapo Kikwete alikuwa na mgongano upi wa maslahi?Yeye Jakaya hakuwa anatarajia kugombea 2015 hivyo alikuwa mtu sahihi wa kuongoza kikao hicho!
Naona umeshindwa kuelewa mantiki kabisa!
 
CC ya CCM imebariki tuu maamuzi, the kangaroo court was ile Kamati ndio imeamua, CC ikabariki.
P
 
Makosa hayakuwa dhidi ya Magufuli, bali kukiuka miongozo, taratibu, na kanuni zinazofahamika.
 
Hapa ni kesi ya Nyani amepelekewa Nyani kutoa hukumu!
 
Kamwe usimshatakie mumeo kwa bamkwe kuwa ni kipanga.

Jr[emoji769]
 
2014 Membe alirimamishwa asifanye siasa kwa muda wa mwaka mmoja ikiwa kosa ni kuanza kampeni za urais kabla ya muda na mwenyekiti wa kikao hicho alikuwa Mh Jakaya Kikwete.
Hapo kikwete alikuwa na interest gani mpaka asiongoze yeye kikao?
 
Back
Top Bottom