Swali kwa CCM: Ikiwa "makosa" ya Membe, Makamba na Kinana yalihumhusu Magufuli, ilikuwa sahihi kwa Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Kamati iliyowaadhibu?

Kamati ndio iliyowasilisha taarifa na CC ikabariki uamuzi wa kamati maana ndio ilyofanya kazi ya kuwasikiliza na kuja na maamuzi na kazi ya CC nikukubaliana na kamati ambayo ilipewa kazi na CC

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kawaida ni utamaduni au utaratibu
B-50
 
Kuna TACO na TAKO .... Lakini zote zinatamkwa tako... Sio mbaya mkiita CCM lakini ikiwa ni CHAMA CHA MAGUFULI itaendelea kubaki tu ni ccm......
Mkuu TACO na TAKO ni lugha mbili tofauti huwezi kulinganishaila hili la CCM Mapinduzi na Magufuli hawawezi kukwepa 🙂
 

Chama ni saccos binafsi mwenye saccos yake ndo kaamua iwe hivo
 
Huyo anapotosha; kesi ya Zito ilikua dhidi ya kula njama ya kumpindua mwenyekiti na kufanya hujuma dhidi ya chama.
Kesi ya Membe na wenzake ilikua dhidi ya Mh Magufuli, kwenye yale mazungumzo amna sehemu iliyozungumzwa ccm kama chama. Iwapo yale mazungumzo yangekua na nguvu wangeshtakiwa na serikali au na Magufuli mwenyewe.
Mbona wanachama wengi wa CCM wanatukana na kugombana na watu kila kukicha huku mtaani kwanini hawajastakiwa kwenye chama?
Ni mpuuzi tu ndo anaweza kuamini kua kile kilikua barua ya kuwaita kwa mashtaka yanayousiana na yale mazungumzo.
 
@blome-e kwaiyo ukitaka kila kikao kikao cha halmashaur kuu ya chama ikikaa kumjadili mkosaji katiba ya chama ibadilishwe kama **** kuna mjumbe anamaslah na mtu fulani anaejadiliwa? Ukumbuke katiba ya imetaja kama mwenyekiti
 
@blome-e kwaiyo ukitaka kila kikao kikao cha halmashaur kuu ya chama ikikaa kumjadili mkosaji katiba ya chama ibadilishwe kama **** kuna mjumbe anamaslah na mtu fulani anaejadiliwa? Ukumbuke katiba ya imetaja kama mwenyekiti
Huhitaji kuweka vitu kama hivyo kwenye katiba, hata common sense itatosha. Kwani mwanachama wa hiyo kamati akiwa ndio mtuhumiwa naye atabaki kwenye hichi kikao kama member wa kamati? Kwa hiyo kama kuna kipengele kinasema atapisha basi kinapaswa kutumika hata kwa mwenyekiti kupisha ili kikao kifanyike askiwa hayupo. Haijalishi kama yeyey sio mtuhumiwa bali suala ni kwambaanahusika moja kwa moja katika tuhuma zinazojadiliwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…