Nimeuliza makusudi ili nipate ufafanuzi .
Kuna fungu lolote kutoka serikalini linatengwa na kuingizwa kwenye akaunti ya TFF ? Nakumbuka wakati wa FAT ya Muhidin Ndolanga , FIFA ilipiga Marufuku kwa serikali kuingilia masuala ya soka , sasa siku hizi FIFA wamebadili msimamo wao ?
Je hela zile ni za Umma ama ni mchango wa FIFA kwa TFF ?
.....................................................
UPDATES
FIFA yaingilia kati , ambapo imetuma ujumbe kuja kufuatilia sakata hilo , inatarajiwa Jumanne ijayo kutafanyika kikao kati ya wajumbe wa FIFA na viongozi wa TFF walionusurika .