Swali la mjinga: Mwenye mamlaka ya kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya ni nani?

Swali la mjinga: Mwenye mamlaka ya kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya ni nani?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Swali la kijinga toka kwa mjinga. Kama hujui maana ya ujinga na mjinga, unaweza kunicheka kwa kuona au kudhani najitukana mwenyewe.

Lakini ukweli wa mambo ni kwamba ujinga si tusi. Binadamu wote wana ujinga.

Hakuna mtu ajuaye kila kitu.

Sasa basi, leo ngoja niulize.

Katika Tanzania yetu hii, ni nani mwenye mamlaka ya kuamua kuanzishwa mchakato wa kupata katiba mpya?

Ni wananchi wenyewe?

Ni wananchi kupitia wabunge?

Au ni Rais ambaye kwa Tanzania ni Mungu mtu aliye juu ya kila kitu, ikiwemo katiba yenyewe?

Nauliza hivyo kwa sababu sasa hivi Rais Samia anapewa shinikizo la kuanzisha tena mchakato wa katiba mpya.

Sasa mimi sielewi na sijui. Yeye Samia [rais] ndiye mwenye hayo mamlaka?

Kama yeye ndiye, hayo mamlaka yanatoka wapi?

Yameandikwa kwenye katiba? Sheria?

Au tunadhani tu kuwa yeye ndiye mwenye hayo mamlaka kwa sababu yeye ni Rais lakini kiukweli hayo mamlaka hana?

Kwa nini mchakato wa kupata katiba mpya ni mpaka yeye aridhie ilhali yeye ni mtumishi wa wananchi ambao ndiyo wenye nchi?

Wajuzi na wajuvi, naomba mnifute huu ujinga nilionao. Tafadhalini sana 🙏.
 
Kwa kuwà Rais anatokana na wananchi na kwakuwa pia yeye ni sehemu ya bunge ambalo pia linatokana na wananchi kwa maana demokrasia ya uwakilishi na kwakuwa yeye ndiye mwenye bajeti kama mhimili unakusanya pesa Kwa kuwa katiba ili iundwe huhitaji bajeti ni ukweli kuwa yeye mheshimiwa Rais anayonafasi kubwa ya kuanzisha mchakato wa katiba kuliko hao wajinga uliowataja hapo juu.

USSR
 
Kwa kuwà Rais anatokana na wananchi na kwakuwa pia yeye ni sehemu ya bunge ambalo pia linatokana na wananchi kwa maana demokrasia ya uwakilishi na kwakuwa yeye ndiye mwenye bajeti kama mhimili unakusanya pesa Kwa kuwa katiba ili iundwe huhitaji bajeti ni ukweli kuwa yeye mheshimiwa Rais anayonafasi kubwa ya kuanzisha mchakato wa katiba kuliko hao wajinga uliowataja hapo juu.

USSR
Yeye ndiye mwenye bajeti? Hizo hela kwani ni za kwake au ni za wananchi na wahisani?
 
Mwenye mamlaka au anayetakiwa kuwa na mamlaka?

Kwa msingi wa sheria na katiba au kwa msingi wa maisha ya kiuhalisia ya Watanzania?
 
Mwenye mamlaka au anayetakiwa kuwa na mamlaka?

Kwa msingi wa sheria na katiba au kwa msingi wa maisha ya kiuhalisia ya Watanzania?
Nazungumzia sasa hivi: mwenye mamlaka hayo ni nani?
 
Nazungumzia sasa hivi: mwenye mamlaka hayo ni nani?
Kwa msingi wa katiba na sheria au kwa msingi wa uhalisia wa maisha ya Watanzania?

Watanzania hatuishi kwa kufuata sheria na katiba kwa hivyo kuna majibu ya msingi wa kufuata sheria na katiba, na majibu ya uhalisia wa maisha ya Watanzania.

Sasa unalenga wapi hapo?
 
Mabadiliko ya Katiba yanatakiwa yaanzie kwa wananchi,lakini kwa Tanzania Rais ni kila kitu ,yeye anateua Jaji mkuu, anateua Spika wa bunge(Mwenyekiti wa kamati kuu ya CCM inayopitisha jina la Spika), anateua Mwenyekiti na makamishna wa time ya uchaguzi,yeye anaweza kufunga watu,yeye anaweza kuua,yeye anaweza kubambikia mtu kesi...Kila kitu anaweza kufanya na kuamua na ndiyo maana mchakato wa Katiba mpya anaombwa yeye.
 
Yeye ndiye mwenye bajeti? Hizo hela kwani ni za kwake au ni za wananchi na wahisani?
Haya maswali mbona hamkumuuliza hayati wakati ananunua ndege na kujenga uwanja chato bila idhini?
MUACHENI MAMA AFUNGUE NCHI SI NDIO TULIVYOKUBALIANA AU?
 
Leo na wewe muumini wa Chato unatoa neno kuhusu katiba mpya? Kipindi Cha JPM uliipinga kwa nguvu zote, ukawa unataka ndege, madaraja....reli na lami
 
Kwa kuwà Rais anatokana na wananchi na kwakuwa pia yeye ni sehemu ya bunge ambalo pia linatokana na wananchi kwa maana demokrasia ya uwakilishi na kwakuwa yeye ndiye mwenye bajeti kama mhimili unakusanya pesa Kwa kuwa katiba ili iundwe huhitaji bajeti ni ukweli kuwa yeye mheshimiwa Rais anayonafasi kubwa ya kuanzisha mchakato wa katiba kuliko hao wajinga uliowataja hapo juu.

USSR
Tatizo lako la kuabudu magufuli litakutokea puani
 
Kwa msingi wa katiba na sheria au kwa msingi wa uhalisia wa maisha ya Watanzania?

Watanzania hatuishi kwa kufuata sheria na katiba kwa hivyo kuna majibu ya msingi wa kufuata sheria na katiba, na majibu ya uhalisia wa maisha ya Watanzania.

Sasa unalenga wapi hapo?
Nazungumzia aliye na mamlaka hayo kisheria.

Sizungumzii kufanya mambo kienyeji enyeji na kwa mazoea na uoga.

Nazungumzia utaratibu ulio rasmi.

Ni nani mwenye hayo mamlaka? Ni Rais?

Kama ni Rais, hayo mamlaka yanatoka wapi? Kwenye sheria ipi? Sura ipi ya katiba?
 
Haya maswali mbona hamkumuuliza hayati wakati ananunua ndege na kujenga uwanja chato bila idhini?
MUACHENI MAMA AFUNGUE NCHI SI NDIO TULIVYOKUBALIANA AU?
Kwa hiyo kama hatukuuliza ndo tusiulize?

What kinda fcuked up logic is that?

Dunderhead.
 
Tatizo lako la kuabudu magufuli litakutokea puani
Wewe ni mpumbavu nani kamtaja Magufuli hapa mnamuogopa mtu aliyekufa , kila siku mnamtukana mnadhani wananchi waliwatuma kutatua kero zao au kumnanga Magufuli

USSR
 
Nazungumzia aliye na mamlaka hayo kisheria.

Sizungumzii kufanya mambo kienyeji enyeji na kwa mazoea na uoga.

Nazungumzia utaratibu ulio rasmi.

Ni nani mwenye hayo mamlaka? Ni Rais?

Kama ni Rais, hayo mamlaka yanatoka wapi? Kwenye sheria ipi? Sura ipi ya katiba?
Mamlaka ya mwisho yanatoka kwa wananchi, ukisoma falsafa ya social contract utaona hilo limeandikwa kuanzia Hobbes, Locke, Rousseau, de Tocqueville mpaka Fukuyama, Mazrui na Nyerere.

Au hata kwa kutumia mantiki tu.

Mjakazi aliyewekwa kuwatumikia watu hatakiwi kuwa na nguvu kuliko watu waliomuweka.

Hii ni Jamhuri, si Ufalme usio na wigo.
 
Mamlaka ya mwisho yanatoka kwa wananchi, ukisoma falsafa ya social contract utaona hilo limeandikwa kuanzia Hobbes, Locke, Rousseau, de Tocqueville mpaka Fukuyama, Mazrui na Nyerere.

Au hata kwa kutumia mantiki tu.

Mjakazi aliyewekwa kuwatumikia watu hatakiwi kuwa na nguvu kuliko watu waliomuweka.
Kinyume chake kama hataki hiyo ni DICTATOR
 
Wewe ni mpumbavu nani kamtaja Magufuli hapa mnamuogopa mtu aliyekufa , kila siku mnamtukana mnadhani wananchi waliwatuma kutatua kero zao au kumnanga Magufuli

USSR
Wewe ni lijinga la mwisho, huwezi kuabudu mwanadamu mwenzako. Uliabudu Raisi wa awamu ya tano ukafikiri ndiye aliyeumba hii Dunia. Kwasasa unachuki ya kijinga dhidi ya Rais alioko madarakani
 
Mamlaka ya mwisho yanatoka kwa wananchi, ukisoma falsafa ya social contract utaona hilo limeandikwa kuanzia Hobbes, Locke, Rousseau de Tocqueville mpaka Fukuyama, Mazrui na Nyerere.

Au hata kwa kutumia logic tu.

Mjakazi aliyewekwa kuwatumikia watu hatakiwi kuwa na nguvu kuliko watu waliomuweka.
See, that’s the problem with us Tanzanians.

We are complete pussies. Too docile.

We are scared to take the bull by the horns and do what’s in our best interest.

Kipindi cha Magufuli tulikaa kimya kabisa kuhusu katiba.

Sasa hivi tunabembeleza tupate hisani ya Samia.

Ndo maana CCM wanatuchezea sana.
 
Back
Top Bottom