Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele ‘Maslahi ya Taifa’?

Swali la Morality: Je, ni lazima kuusema kila ukweli unaousikia au tutangulize mbele ‘Maslahi ya Taifa’?

Sasa unauliza "sababugani"i katika muktadha upi? Kumbuka hapa tunaongelea deni katika general context.Hakuna case in point,tunayoirejea kwa mjibu Wa mada hii.
Na mimi nauliza katika muktadha wa general context.

Umesema si madeni yote yanatakiwa kulipwa.

In general, deni gani halitakiwi kulipwa na kwa sababu gani?
 
Kaka yangu Paskali, naweza kukupa somo jipya litakalo kusaidia katika maisha yako yaliosalia hapa duniani.

Kamwe hakuna ukweli unaobomoa, maana ukweli ndio asili ya Mungu mwenyewe kwa hiyo unaposema ukweli mahali popote umeufurahisha moyo wa Mungu. Kiroho, Kimwili, na kisaikolojia usiposema ukweli umejiumiza mwenyewe.

Labda jambo ambalo ungesema katika kusema ukweli lazima hekima itumike. Nitamani ni kuwekee mfano mmoja wa kusema ukweli kwa hekima.

Mfalme Daudi alimtamani mke wa mwanajeshi wake, kwa hiyo akamfanyia hila kuhakikisha anauawa vitani, Mungu hakupendezwa na jambo hilo, kwa hiyo alimtuma nabii Nathan kumwambia Daudi uovu wake. Nabii alimwambia Daudi kuwa kuna mtu mmoja tajiri ametembelewa na wageni, ila amechukua kondoo wa maskini akawachinjia wageni wake.

Mfalme Daudi alihamaki na kusema kwamba huyo tajiri lazima auawe, nabii akamwambia Daudi kuwa mtu huyo niwewe Daudi alilia sana na kutubu. Ukweli kwa njia ya hekima, ila ukweli unatakiwa usemwe kila wakati

Excellent Vivianet!!!
 
Na mimi nauliza katika muktadha wa general context.

Umesema si madeni yote yanatakiwa kulipwa.

In general, deni gani halitakiwi kulipwa na kwa sababu gani?

Hilo swali lako linatosha kuiangusha Serikali nzima. Hawawezi kukujibu AW.

But again I'm gobsmacked just how could we be so dumb as a people? Hivi hayo wanayoyaita "maadili ya uongozi" ni kitu gani hasa? Je si wino mweusi kwenye karatasi ambao hauna chembe ya uhusiano na uhalisia wa maisha tunayoishi????
 
Na mimi nauliza katika muktadha wa general context.

Umesema si madeni yote yanatakiwa kulipwa.

In general, deni gani halitakiwi kulipwa na kwa sababu gani?

Mifano iko mingi: umenikopesha pesa.Kumbe pesa yenyewe uliiba mahali na au chanzo chake ni biashara ya madawa ya kulevya.Katika mazingira kama hayo, ikigundulika kuwa chanzo chake sio halali,deni hilo huwezi kuwa na nguvu ya kisheria au ya kimaadili kulidai.

Mfano Wa pili: katika kunikopesha ulitumia ulaghai wa namna Fulani.Nimekuomba uninunulie Lori la mwaka 2016 kwa mkopo.Wewe ukanikopesha Lori la mwaka 2010.Lori likapata ajali na kuharibika vibaya kwa sababu ya kushindwa kupanda mlima.Nikigundua kuwa ulinikopesha lori tofauti na maombi yangu mkopo huo sitaulipa na nitakudai fidia tena kwa sababu malengo yangu hayakutimia na umenipotezea muda.

Mifano mingine unaweza kuongezea.Nafikiria sasa una picha kamili.
 
Pascal Mayalla
images(1).jpg
 
Mifano iko mingi: umenikopesha pesa.Kumbe pesa yenyewe uliiba mahali na au chanzo chake ni biashara ya madawa ya kulevya.Katika mazingira kama hayo, ikigundulika kuwa chanzo chake sio halali,deni hilo huwezi kuwa na nguvu ya kisheria au ya kimaadili kulidai.

Mfano Wa pili: katika kunikopesha ulitumia ulaghai wa namna Fulani.Nimekuomba uninunulie Lori la mwaka 2016 kwa mkopo.Wewe ukanikopesha Lori la mwaka 2010.Lori likapata ajali na kuharibika vibaya kwa sababu ya kushindwa kupanda mlima.Nikigundua kuwa ulinikopesha lori tofauti na maombi yangu mkopo huo sitaulipa na nitakudai fidia tena kwa sababu malengo yangu hayakutimia na umenipotezea muda.

Mifano mingine unaweza kuongezea.Nafikiria sasa una picha kamili.
Mifano yako yote haina uhusiano na habari ya uhalisi iliyopo.

Habari iliyopo imeshaenda mahakamani, mahakama ikaamua serikali ilipe, serikali ikakata rufaa, serikali ikashindwa rufaa.

Unataka kutumia mfano usiohusika kuhalalisha deni lisilipwe?
 
Hilo swali lako linatosha kuiangusha Serikali nzima. Hawawezi kukujibu AW.

But again I'm gobsmacked just how could we be so dumb as a people? Hivi hayo wanayoyaita "maadili ya uongozi" ni kitu gani hasa? Je si wino mweusi kwenye karatasi ambao hauna chembe ya uhusiano na uhalisia wa maisha tunayoishi????
Huwezi kuwa na maadili ya viongozi katika nchi ambayo rais wake anayependwa na watu wengi anaita mawaziri wake aliowateua mwenyewe wapumbavu.

Kimaadili kakosea sana kuwaita wasaidizi wake wapumbavu hadharani, hata kwenye faragha kuna lugha ya kutumia.

Si tu anaonekana hana maadili, bali anatuambia kwamba yeye aliyewateua hao wapumbavu kuwa mawaziri ni mpumbavu zaidi, kwa sababu ni mpumbavu zaidi tu anayeweza kumteua mpumbavu kuwa waziri.
 
Mifano yako yote haina uhusiano na habari ya uhalisi iliyopo.

Habari iliyopo imeshaenda mahakamani, mahakama ikaamua serikali ilipe, serikali ikakata rufaa, serikali ikashindwa rufaa.

Unataka kutumia mfano usiohusika kuhalalisha deni lisilipwe?

Ahaaa mkuu,mbona hivi? Mbona tunajenga hoja "kijadi"? Ulisema tunajadili kulipa au kutolipa deni katika General context.Tukakubaliana hivyo.Nimekupa mifano.Sasa umeruka kimanga na unaniletea issue ya deni la Stirling! Una lenga kunichokonoa nikupe ninachokijua kuhusu suala hilo au nini dhamira yako.Basi tuishie hapo.
 
Ahaaa mkuu,mbona hivi? Mbona tunajenga hoja "kijadi"? Ulisema tunajadili kulipa au kutolipa deni katika General context.Tukakubaliana hivyo.Nimekupa mifano.Sasa umeruka kimanga na unaniletea issue ya deni la Stirling! Una lenga kunichokonoa nikupe ninachokijua kuhusu suala hilo au nini dhamira yako.Basi tuishie hapo.

Ujuzi unahusiana na kutoka kwenye la jumla na kwenda kwenye hususan.

Mfano wako wa jumla hauhusiani na habari hususan.

Sijalenga kukuchokonoa unipe unachokijua kwa sababu sina hakika unajua chochote cha maana.

Usiseme "tuishie hapo" baada ya kutoa mfano usio linganifu katika maada, sema umetoa mfano usio linganifu na hujakidhi hoja za kujibu swali hususan.

Sent from my Kimulimuli
 
Tuamue kama tunasema kweli au tunasema uongo. hakuna kweli na uongo at the same time, hapo huingia unafiki nakadhalika..... Kama tunaamua kuwa wakweli kwenye kuwasema wenzetu basi tuwe wakweli pale tunaposemwa sisi pia....
 
Tuamue kama tunasema kweli au tunasema uongo. hakuna kweli na uongo at the same time, hapo huingia unafiki nakadhalika..... Kama tunaamua kuwa wakweli kwenye kuwasema wenzetu basi tuwe wakweli pale tunaposemwa sisi pia....
Ukweli ni nini na utajuaje huu ni ukweli si uongo? Kwa misingi ipi? Na hiyo misingi imewekwaje? Na unajuaje kwamba assumption za hiyo misingi ni za kweli?

Nikisema pembetatu zote zina nyuzi 180 nitakuwa nasema kweli au si kweli?

Sent from my Kimulimuli
 
Ukweli ni nini na utajuaje huu ni ukweli si uongo? Kwa misingi ipi? Na hiyo misingi imewekwaje? Na unajuaje kwamba assumption za hiyo misingi ni za kweli?

Nikisema pembetatu zote zina nyuzi 180 nitakuwa nasema kweli au si kweli?

Sent from my Kimulimuli
===
Njia sahihi yakuthibitisha ukweli ni kusubstantiate claim yako kwa justifiable evidence... kama ni jambo la maslahi ya nchi swala la kuficha ukweli haliwezi kuamuliwa na mtu mmoja... kwa mfano kama tunashiriki kukemea wezi wa madini then report za madini na mikataba yake lazima ziwe available kwetu wote... la sivyo usiri ni alama ya kufichwa ukweli....
 
===
Njia sahihi yakuthibitisha ukweli ni kusubstantiate claim yako kwa justifiable evidence... kama ni jambo la maslahi ya nchi swala la kuficha ukweli haliwezi kuamuliwa na mtu mmoja... kwa mfano kama tunashiriki kukemea wezi wa madini then report za madini na mikataba yake lazima ziwe available kwetu wote... la sivyo usiri ni alama ya kufichwa ukweli....
1.Serikali ya Tanzania wezi wengi na hawana interest na ukweli.

2. Tunapoongelea ukweli ni muhimu tuweke context, framework, acceptable margin of error etc.

Hata ukisema "parallel lines hazikutani" bila ku specify per number 2 above, utakuwa hujasema kweli.

Sent from my Kimulimuli
 
1.Serikali ya Tanzania wezi wengi na hawana interest na ukweli.

2. Tunapoongelea ukweli ni muhimu tuweke context, framework, acceptable margin of error etc.

Hata ukisema "parallel lines hazikutani" bila ku specify per number 2 above, utakuwa hujasema kweli.

Sent from my Kimulimuli
Binafsi siwezi kusema serikali ya Tanzania ni wezi na hawana interest na ukweli.... nadhani tunaweza ku-scale tatizo katika different dimensions. Serikali ni nani na wanatoka wapi hao wasimamizi wa serikali?... if serikali ni waongo vipi wanaodanganywa wakitambua ukweli bado hawaonekani kukereka? Labda ni tatizo la culture zaidi from primary settings za jamii....
 
Paskali, kulingana na kauli za kaka yakoni kuwa "msemakweli ni mpenzi wa Mungu"
Jee weweau nani hapendi kuwa mpenzi wa Mungu? ajabu ni kuwa huo ukweli una jambo la ajabu sana. Ukisema "mfalme yuko uchii!" hata kama hajavaa, wewe ni mkosaji, unapaswa kusema joho la mfalme limempendezalakini halionekani!
 
Binafsi siwezi kusema serikali ya Tanzania ni wezi na hawana interest na ukweli.... nadhani tunaweza ku-scale tatizo katika different dimensions. Serikali ni nani na wanatoka wapi hao wasimamizi wa serikali?... if serikali ni waongo vipi wanaodanganywa wakitambua ukweli bado hawaonekani kukereka? Labda ni tatizo la culture zaidi from primary settings za jamii....

By serikali I mean viongozi wakuu wa kitaifa wa serikali na support network yao.

Ikiwa jamii ya Tanzania ina utamaduni wa kuachia machifu wao wafanye wanavyotaka, na utamaduni huo kwa haki unaachia wizi na unyonyaji wa kimangimeza, na utamaduni huo ndio unaoendelea mpaka leo hata kama tunajidanganya kwamba tuna sheria, demokrasia, bunge etc, hilo linafanya viongozi wanaouziana nyumba za serikali kwa bei ya kutupa halafu serikali ikaishiwa na nyumba kuwa si wezi?

Hilo linafanya viongozi wanaochukua mikopo mifuko ya jamii bila kuilipa kuwa si wezi?

Kwa sababu tuna utamaduni wa kuruhusu viongozi kukwapua wanavyotaka, wakikwapua si wezi?
 
Back
Top Bottom