Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
21,113
Reaction score
65,124
Tokea mwaka 1944, baada ya kutengeneza mfumo wa Bretton-Woods hakuna taifa ambalo limewahi kuwa na uchumi mkubwa kama Marekani. Kufika mwaka 1945, Marekani ilikuwa inamiliki nusu nzima ya uchumi wa dunia. Fedha ya Marekani ikishikiliwa na dhahabu (Gold-Backed) ilikuwa ndiyo inatumiwa kwa kiwango kikubwa kwenye biashara zote za kimataifa.

Mwaka 1957, baada ya Raisi Gamal Abdel Nasser wa Misri kutaifisha mfereji wa Suez, Uingereza, Ufaransa na Israel waliunda mkakati wa kuvamia Misri ili kumtoa Nasser. Mkakati huu ulikufa kibudu baada ya Raisi wa Marekani General Dwight Eisenhower kuwachimba mkwara mzito Waingereza kwamba wangeacha kununua hati-fungani (Sovereign Bonds) za Uingereza na nyingine wangeziuza, jambo ambalo lingeangusha uchumi wa Uingereza.

Kiufupi, baada ya hili kutokea Raisi wa Ufaransa General Charles De Gaulle alilalamika na kusema kwamba "The dollar gives America an exorbitant privilege in international financial system". Akimaanisha kwamba dola inampa Marekani nguvu iliyomithirika kwenye uchumi wa dunia dhidi ya mataifa mengine. Kiufupi Marekani akikutoa kwenye mfumo wake wa kifedha, lazima uumie.

Wataalamu wanatumia vipimo (Metrics) kama GDP na PPP kupima uchumi wa dunia. Ukitumia kipimo cha GDP, nadhani Marekani ndiyo taifa lenye uchumi mkubwa zaidi duniani likifuatiwa na Uchina. Uchumi wa Marekani peke yake ni asilimia 24% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Kiufupi ni kwamba, all financial roads lead to America.

Marekani hayuko peke yake, anashirikiana na wenzake wa kule Ulaya (European Union) na wenzake wa chama cha mabwanyenye wa dunia almaarufu kama G7. Ukichanganya uchumi wa Marekani, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani, Italia, Canada na Japan, ambao ndiyo nchi tajiri zaidi duniani unapata asilimia 30.7% ya uchumi wa dunia (Global GDP).

Kiuhalisia, haya mataifa saba ndiyo yanayoendesha uchumi wa dunia kupitia mifumo waliyoitengeneza baada ya mwaka 1945. Viwanda vikubwa duniani ni vyao, masoko makubwa ya hisa ni yao, mabenki makubwa duniani ni yao, wao ndiyo wanaongoza katika kuzikopesha fedha nchi nyingine na wao ndiyo wanaongoza kwa kuuza huduma zaidi hapa duniani.

Maswali yangu ya kiuchumi ni haya yafuatayo:
Mosi, kwanini Urusi ambayo ni asilimia 4% tu ya uchumi wa dunia (Share in Global GDP) bado haijaanguka baada ya mataifa makubwa yanayomilikia asilimia 30.7% ya uchumiwa dunia kuwawekea vikwazo vikali ?

Pili, kwanini makampuni ya Urusi ya nishati ndiyo yameongoza duniani kwa kuuza zaidi nishati, ilhali yamewekewa vikwazi baada vikali ? Takwimu zilizotolewa na Marekani yenyewe zinasema kiujumla mashirika ya nishati ya Urusi yameuza zaidi na kupata faida kipindi hiki cha vita na vikwazo kuliko kipindi kingine chochote. Tatizo liko wapi hapa ?

Tatu, Je, tutegemee kwamba kuna siku hivi vikwazo vitafanya kazi na vitauangusha uchumi wa Urusi kama ambavyo Raisi Biden alisema mwaka 2022 kabla ya uvamizi kuanza ? Alisema kwamba uchumi wa Urusi ungeanguka ndani ya wiki chache tu, sasa ni mwaka na zaidi. Mataifa ya Magharibi yamefanikiwa au tuendelee kusubiri ?
 
Nitajibu swali lako kama ifuatavyo:

Uchumi wa Russia haujateteleka kwa sababu zifuatazo

1. Russia ni Superpower Halisi: unavyodeal na nchi kubwa kama Russia inakupasa uwe na Plan B au C. West walishindwa kutambua Stage alokuwa amefikia Russia ilikua ni stage kubwa sana. Sababu Russia alizifanya nchi za ulaya kuwa dependent kwake kwenye suala la Nishati na ili kuwakamata zaidi alijenga pipes “strems” za kusuply gas na mafuta kwa cheap price.

2. Nature of economic system: Russia ni socialist state hivo major means of production ziko under the government. Zile sector zinazobeba uchumi wa nchi bhasi kuna mkono wa Serikali. Ndomana unaona hizi Gazprom na Rosatam bado ziliendelea kufanya vizuri licha ya vikwazo.

3. Strong leadership

4. Russia ni moja ya nchi ambazo zinajitegemea kiuchumi hawa jamaa karibu 90% wanajitegemea ni asilimia ndogo sana ambazo wana import.

5. Russia wana intelejensia hatari sana ambayo inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa (FSB).

6. Russia is Rich in natural resource ($75 trillion approximately)
 
Nitajibu swali lako kama ifuatavyo:

Uchumi wa Russia haujateteleka kwa sababu zifuatazo

1. Russia ni Superpower Halisi : unavyodeal na nchi kubwa kama Russia inakupasa uwe na Plan B au C. West walishindwa kutambua Stage alokuwa amefikia Russia ilikua ni stage kubwa sana. Sababu Russia alizifanya nchi za ulaya kuwa dependent kwake kwenye suala la Nishati na ili kuwakamata zaidi alijenga pipes “strems” za kusuply gas na mafuta kwa cheap price.
Nakusoma mkuu, lakini hapa nataka nieleweshwe zaidi. Unataka kusema kwamba bila nishati kutoka Urusi, uchumi wa nchi za Ulaya hauwezi kwenda mbele ? Kwanini Ulaya wasitumie nishati mbadala (Renewables) kama umeme wa jua, makaa ya mawe, nyuklia na upepo ?
2. Nature of economic system: Russia ni socialist state hivo major means of production ziko under the government. Zile sector zinazobeba uchumi wa nchi bhasi kuna mkono wa Serikali. Ndomana unaona hizi Gazprom na Rosatam bado ziliendelea kufanya vizuri licha ya vikwazo.
Kama ni mfumo wa kijamaa, kwanini Urusi ya kisovieti (USSR) ilianguka na kufilisika ilhali kila kitu kilikuwa kinamilikiwa na serikali ya kikomunisti ?

4. Russia ni moja ya nchi ambazo zinajitegemea kiuchumi hawa jamaa karibu 90% wanajitegemea ni asilimia ndogo sana ambazo wana import.
Benki Kuu ya Urusi ilitoa tamko mwaka 2021 kwamba asilimia 65% ya viwanda vya uzalishaji inategemea teknolojia na bidhaa kutoka nje. Hebu fanya tafiti zaidi naweza kuwa nakosea. Swali langu hapa, ni hili kama utegemezi wa bidhaa za nje ni asilimia 65% kwanini mpaka sasa uzalishaji wa Urusi haijaanguka ?

6. Russia is Rich in natural resource ($75 trillion approximately)
Nadhani hii inaweza ikawa moja ya sababu kubwa. Japo naendelea kusubiri nondo za wadau, watufundishe zaidi.
 
Kwa vile hii mada inahusu uchumi mim sitoweza kuchangia kwa koment bali nitadondosha laik kwa Kila mchangiaj


Kuna dogo anajiita Malcom Lumumba jamaa noma kwa mijadala ya aina hii ila tangu special operation ing'oe nanga hachangii kabisaaaaaaa mijadala ya kisiasa sasa sijui nae kaenda front kuongezea nguvu au kaamua kususa tu
 
Nitajibu swali lako kama ifuatavyo:

Uchumi wa Russia haujateteleka kwa sababu zifuatazo

1. Russia ni Superpower Halisi: unavyodeal na nchi kubwa kama Russia inakupasa uwe na Plan B au C. West walishindwa kutambua Stage alokuwa amefikia Russia ilikua ni stage kubwa sana. Sababu Russia alizifanya nchi za ulaya kuwa dependent kwake kwenye suala la Nishati na ili kuwakamata zaidi alijenga pipes “strems” za kusuply gas na mafuta kwa cheap price.

2. Nature of economic system: Russia ni socialist state hivo major means of production ziko under the government. Zile sector zinazobeba uchumi wa nchi bhasi kuna mkono wa Serikali. Ndomana unaona hizi Gazprom na Rosatam bado ziliendelea kufanya vizuri licha ya vikwazo.

3. Strong leadership

4. Russia ni moja ya nchi ambazo zinajitegemea kiuchumi hawa jamaa karibu 90% wanajitegemea ni asilimia ndogo sana ambazo wana import.

5. Russia wana intelejensia hatari sana ambayo inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa (FSB).

6. Russia is Rich in natural resource ($75 trillion approximately)
Umepapasa papasa tu hili jibu lako hujajibu kisayansi ya Uchumi au wewe ndio Waziri wetu wa Fefha nini??
 
Nakusoma mkuu, lakini hapa nataka nieleweshwe zaidi. Unataka kusema kwamba bila nishati kutoka Urusi, uchumi wa nchi za Ulaya hauwezi kwenda mbele ? Kwanini Ulaya wasitumie nishati mbadala (Renewables) kama umeme wa jua, makaa ya mawe, nyuklia na upepo ?


Kama ni mfumo wa kijamaa, kwanini Urusi ya kisovieti (USSR) ilianguka na kufilisika ilhali kila kitu kilikuwa kinamilikiwa na serikali ya kikomunisti ?


Benki Kuu ya Urusi ilitoa tamko mwaka 2021 kwamba asilimia 65% ya viwanda vya uzalishaji inategemea teknolojia na bidhaa kutoka nje. Hebu fanya tafiti zaidi naweza kuwa nakosea. Swali langu hapa, ni hili kama utegemezi wa bidhaa za nje ni asilimia 65% kwanini mpaka sasa uzalishaji wa Urusi haijaanguka ?


Nadhani hii inaweza ikawa moja ya sababu kubwa. Japo naendelea kusubiri nondo za wadau, watufundishe zaidi.
Ndio mana nimesema huyu jamaa hakujibu maswali yeye alizama kwenye pori analolijua yeye basi
 
Probably you aren’t paying much attention on economic trends ya russia and, there are changes on russia economy post sanctions.

The fact economy haija crash abruptly instead it’s declining slowly it’s difficult kwa non-economists ku notice the stumbling situation.

Qn1.
G7 waneweka vikwazo (kwa baadhi ya commodity tu na sio zote. Due to diversified economy ya russia (gas, petrol, mbolea, rare earth metals, etc) inanfanya awe na uwanja mpana wa wateja na sio west tu. So demands ya commodities bado ipo kutoka mataifa mengine. Also domestic consumer ya watu 145mil ni market tosha kuweza kustabilize uchumi. Pia kuna issue ya interest rate kwenye forex kuboost local currency isishuke zaidi.

Kuhusu makampuni ya russia kuongoza mauzo mbona hilo niswala rahisi sana

Qn2.
Business inategemea na control variables ili uwin market. So amid sanctions Russia alinusa kuanguka wa ruble alichofanya ni ku play na price ya petrol na gas. Unaposhusha price ya bidhaa una attract large market. Lowering commodity price psychologically triggers market flocking. Hii inapelekea bulk sells for fear that yanaweza kupanda bei. So majumuzi ni makubwa. Kutoka India na China, Africa.

Mfano: unapoizuia Mbeya isiuze mchele DSM kwa wateja 8milion. Mbeya inashusha bei ya mchele, mikoa mingine inaenda mbeya kujumua mchele kwa bei ya chini lakini kilo nyingi sababu wajumizi watafikiri mbeleni bei itapanda. Population ya mikoa mingine ni zaidi ya 50 milion by simple mathematics mbeya itapata faida kuliko ingeuza DSM.

Qn3.
Uchumi wa Russia utakua ngumu kuanguka labda kushuka hasa Unapokua na disposal ya natural resources (petrol, gas, metals, mbolea) you’re safe. Russia currently yuko scarce na technologies especially electronics chips. Hii itapelekea kukosa technology advancement kwenye mashine muhimu za uzalishaji hasa tractors, farm drones, ndege, magari, industries na automation kwa ujumla na itakua expensive kwelikweli maana soko lao kuu la electronics lilikua west .

Pia west wakiendelea na kutafuta alternative ya kupata nishati (gas au renewable) basi itakua shida kwa Russia maana competition ya market itakua hot. Especially US aki rump up production, Venezuela, canada, Norway, and other places

Ruble against $ currently .
86B467A7-5521-4564-80A7-AFB7C26F8D37.jpeg
 
Tokea mwaka 1944, baada ya kutengeneza mfumo wa Bretton-Woods hakuna taifa ambalo limewahi kuwa na uchumi mkubwa kama Marekani. Kufika mwaka 1945, Marekani ilikuwa inamiliki nusu nzima ya uchumi wa dunia. Fedha ya Marekani ikishikiliwa na dhahabu (Gold-Backed) ilikuwa ndiyo inatumiwa kwa kiwango kikubwa kwenye biashara zote za kimataifa.

Mwaka 1957, baada ya Raisi Gamal Abdel Nasser wa Misri kutaifisha mfereji wa Suez, Uingereza, Ufaransa na Israel waliunda mkakati wa kuvamia Misri ili kumtoa Nasser. Mkakati huu ulikufa kibudu baada ya Raisi wa Marekani General Dwight Eisenhower kuwachimba mkwara mzito Waingereza kwamba wangeacha kununua hati-fungani (Sovereign Bonds) za Uingereza na nyingine wangeziuza, jambo ambalo lingeangusha uchumi wa Uingereza.

Kiufupi, baada ya hili kutokea Raisi wa Ufaransa General Charles De Gaulle alilalamika na kusema kwamba "The dollar gives America an exorbitant privilege in international financial system". Akimaanisha kwamba dola inampa Marekani nguvu iliyomithirika kwenye uchumi wa dunia dhidi ya mataifa mengine. Kiufupi Marekani akikutoa kwenye mfumo wake wa kifedha, lazima uumie.

Wataalamu wanatumia vipimo (Metrics) kama GDP na PPP kupima uchumi wa dunia. Ukitumia kipimo cha GDP, nadhani Marekani ndiyo taifa lenye uchumi mkubwa zaidi duniani likifuatiwa na Uchina. Uchumi wa Marekani peke yake ni asilimia 24% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Kiufupi ni kwamba, all financial roads lead to America.

Marekani hayuko peke yake, anashirikiana na wenzake wa kule Ulaya (European Union) na wenzake wa chama cha mabwanyenye wa dunia almaarufu kama G7. Ukichanganya uchumi wa Marekani, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani, Italia, Canada na Japan, ambao ndiyo nchi tajiri zaidi duniani unapata asilimia 30.7% ya uchumi wa dunia (Global GDP).

Kiuhalisia, haya mataifa saba ndiyo yanayoendesha uchumi wa dunia kupitia mifumo waliyoitengeneza baada ya mwaka 1945. Viwanda vikubwa duniani ni vyao, masoko makubwa ya hisa ni yao, mabenki makubwa duniani ni yao, wao ndiyo wanaongoza katika kuzikopesha fedha nchi nyingine na wao ndiyo wanaongoza kwa kuuza huduma zaidi hapa duniani.

Maswali yangu ya kiuchumi ni haya yafuatayo:
Mosi, kwanini Urusi ambayo ni asilimia 4% tu ya uchumi wa dunia (Share in Global GDP) bado haijaanguka baada ya mataifa makubwa yanayomilikia asilimia 30.7% ya uchumiwa dunia kuwawekea vikwazo vikali ?

Pili, kwanini makampuni ya Urusi ya nishati ndiyo yameongoza duniani kwa kuuza zaidi nishati, ilhali yamewekewa vikwazi baada vikali ? Takwimu zilizotolewa na Marekani yenyewe zinasema kiujumla mashirika ya nishati ya Urusi yameuza zaidi na kupata faida kipindi hiki cha vita na vikwazo kuliko kipindi kingine chochote. Tatizo liko wapi hapa ?

Tatu, Je, tutegemee kwamba kuna siku hivi vikwazo vitafanya kazi na vitauangusha uchumi wa Urusi kama ambavyo Raisi Biden alisema mwaka 2022 kabla ya uvamizi kuanza ? Alisema kwamba uchumi wa Urusi ungeanguka ndani ya wiki chache tu, sasa ni mwaka na zaidi. Mataifa ya Magharibi yamefanikiwa au tuendelee kusubiri ?
Si Marekan hiyo hiyo ilisema Iraq ina nyuklia na mkaamini , leo mnatumia tena takwim zake kusifia wapinzan wake , Marekan huyu huyu alisema Sadam anaeza lipua dunia nzima ila ni kwel alikuwa na uwezo huo ? Marekan hutumia sifa kumfanya adui alale pia wengine wamwogope kwa kujihami dhidi yake
 
Nakusoma mkuu, lakini hapa nataka nieleweshwe zaidi. Unataka kusema kwamba bila nishati kutoka Urusi, uchumi wa nchi za Ulaya hauwezi kwenda mbele ? Kwanini Ulaya wasitumie nishati mbadala (Renewables) kama umeme wa jua, makaa ya mawe, nyuklia na upepo ?


Kama ni mfumo wa kijamaa, kwanini Urusi ya kisovieti (USSR) ilianguka na kufilisika ilhali kila kitu kilikuwa kinamilikiwa na serikali ya kikomunisti ?


Benki Kuu ya Urusi ilitoa tamko mwaka 2021 kwamba asilimia 65% ya viwanda vya uzalishaji inategemea teknolojia na bidhaa kutoka nje. Hebu fanya tafiti zaidi naweza kuwa nakosea. Swali langu hapa, ni hili kama utegemezi wa bidhaa za nje ni asilimia 65% kwanini mpaka sasa uzalishaji wa Urusi haijaanguka ?


Nadhani hii inaweza ikawa moja ya sababu kubwa. Japo naendelea kusubiri nondo za wadau, watufundishe zaidi.
unaweza ukawa na resources nying lakin ili kuzitumia unagundua ni gharama mno bora uagize

socialist economy ni closed system haiingiliwi ovyo meanwhile open market ndo haya yanayotusibu "wawekezaji tena wa nje " wakiwa wakubwa watakuendesha tu .
 
Nakusoma mkuu, lakini hapa nataka nieleweshwe zaidi. Unataka kusema kwamba bila nishati kutoka Urusi, uchumi wa nchi za Ulaya hauwezi kwenda mbele ? Kwanini Ulaya wasitumie nishati mbadala (Renewables) kama umeme wa jua, makaa ya mawe, nyuklia na upepo ?


Kama ni mfumo wa kijamaa, kwanini Urusi ya kisovieti (USSR) ilianguka na kufilisika ilhali kila kitu kilikuwa kinamilikiwa na serikali ya kikomunisti ?


Benki Kuu ya Urusi ilitoa tamko mwaka 2021 kwamba asilimia 65% ya viwanda vya uzalishaji inategemea teknolojia na bidhaa kutoka nje. Hebu fanya tafiti zaidi naweza kuwa nakosea. Swali langu hapa, ni hili kama utegemezi wa bidhaa za nje ni asilimia 65% kwanini mpaka sasa uzalishaji wa Urusi haijaanguka ?


Nadhani hii inaweza ikawa moja ya sababu kubwa. Japo naendelea kusubiri nondo za wadau, watufundishe zaidi.
wenzetu intellejensia zao zipo active sio ktk maswala ya kisiasa ko ni michezo ya watu walio komaa kiakili. unamzubaisha adui ili asikutilie maanani sana huku ukisukuma kete yako vema hujawah cheza checkers kete 12 . moja yaweza ikawa culture,nyingine dini, lakin zote zinaenda mbele kutafuta ushindi
 
Nakusoma mkuu, lakini hapa nataka nieleweshwe zaidi. Unataka kusema kwamba bila nishati kutoka Urusi, uchumi wa nchi za Ulaya hauwezi kwenda mbele ? Kwanini Ulaya wasitumie nishati mbadala (Renewables) kama umeme wa jua, makaa ya mawe, nyuklia na upepo ?


Kama ni mfumo wa kijamaa, kwanini Urusi ya kisovieti (USSR) ilianguka na kufilisika ilhali kila kitu kilikuwa kinamilikiwa na serikali ya kikomunisti ?


Benki Kuu ya Urusi ilitoa tamko mwaka 2021 kwamba asilimia 65% ya viwanda vya uzalishaji inategemea teknolojia na bidhaa kutoka nje. Hebu fanya tafiti zaidi naweza kuwa nakosea. Swali langu hapa, ni hili kama utegemezi wa bidhaa za nje ni asilimia 65% kwanini mpaka sasa uzalishaji wa Urusi haijaanguka ?


Nadhani hii inaweza ikawa moja ya sababu kubwa. Japo naendelea kusubiri nondo za wadau, watufundishe zaidi.
katika dunia ya sasa ili uwe na kauli au huru mbinu pekee ni kujiweza(kujitegemea) hata ktk maisha yetu ya kawaida ya familia c tunayona
 
Si Marekan hiyo hiyo ilisema Iraq ina nyuklia na mkaamini , leo mnatumia tena takwim zake kusifia wapinzan wake , Marekan huyu huyu alisema Sadam anaeza lipua dunia nzima ila ni kwel alikuwa na uwezo huo ? Marekan hutumia sifa kumfanya adui alale pia wengine wamwogope kwa kujihami dhidi yake
political propaganda taifa flan linapotaka kuvamia taifa jingine mambo huwa hivyo sababu hata za uongo hutumika.
Waafrica sisi tupo ndani ya box kila tawala inapambania ndoto zake warumi wao wapo wanachase ndoto yao,warusi,waingereza,wafaransa ndio maana unakuta vyuma vinaumana pale mmoja akigundua anaingiliwa kimaslah
 
Probably you aren’t paying much attention on economic trends ya russia and, there are changes on russia economy post sanctions.

The fact economy haija crash abruptly instead it’s declining slowly it’s difficult kwa non-economists ku notice the stumbling situation.
Nauliza hivi kwasababu mabadiliko hayako kwenye uchumi wa Urusi peke yake. Hadi kule Ulaya kuna mabadiliko makubwa tu. Shirika la fedha duniani (IMF) limetangaza kwamba mataifa mengi ya Ulaya yameingia kwenye mdororo wa Uchumi (Recession) kutokana na mfumuko mkubwa wa bei. Ujarumani, taifa lenye uchumi mkubwa barani Ulaya limeingia kwenye mdororo mkubwa.

Marekani nako hali imekuwa mbaya kiuchumi. Mfumuko wa bei (High-Inflation) umepelekea hati-fungani (Bonds) kushuka thamani na kupelekea taasisi nyingi za kifedha kama mabenki kufilisika, kushindwa kutoa huduma na kulipa madeni yake. Inasemekana mpaka sasa mabenki zaidi ya 2,315 yako mufilisi (Insolvent).

IMF wamesema taifa ambalo linategemewa kukua sana kiuchumi kwa mwaka huu na miaka ijayo ni India ambapo uchumi wake unategemea kukua kwa asilimia 6.4% hadi 7%. Hili limechangiwa kwa sehemu kubwa na ununuzi wa nishati ya bei ndogo kutoka Urusi ambapo, inasemekana mwaka jana peke yake India imekomboa zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 5. Hizi ni fedha nyingi sana kwenye ununuzi wa mafuta.

Swali langu ni rahisi sana, Urusi ni asilimia 4% ya uchumi wa dunia, mataifa ya G7 ni asilimia 30.7%, tulitegemea vikwazo vilete madhara zaidi kwa Urusi. Kwanini madhara yanatokea kwa pande zote ?

Qn1.
G7 waneweka vikwazo (kwa baadhi ya commodity tu na sio zote. Due to diversified economy ya russia (gas, petrol, mbolea, rare earth metals, etc) inanfanya awe na uwanja mpana wa wateja na sio west tu. So demands ya commodities bado ipo kutoka mataifa mengine. Also domestic consumer ya watu 145mil ni market tosha kuweza kustabilize uchumi. Pia kuna issue ya interest rate kwenye forex kuboost local currency isishuke zaidi.

Kuhusu makampuni ya russia kuongoza mauzo mbona hilo niswala rahisi sana
Kama nimekuelewa vizuri, unachomaanisha hapa ni kwamba mataifa ya Magharibi yanaendeshwa na FINANCE ECONOMY (Capital Markets & Services) huku taifa la Urusi linaendeshwa na COMMODITY ECONOMY (Raw materials are a source of Russia's hard currency). Maana kilichoiwezesha benki kuu ya Urusi kuinua fedha ya Urusi (Ruble) ni kuiunganisha na biashara za rasilimali kama mafuta, nafaka, gesi, mbolea na madini muhimu.

Hivyo hapa tusema kwamba, yale tuliyofundishwa tukiwa chuo kwamba FINANCE ECONOMY ndiyo kila kitu, inabidi tuyatazame upya kwasababu hata COMMODITY ECONOMY inasehemu pana kwenye maendeleo ya nchi. Je, wataalamu wa Magharibi walikosea kuiangalia Urusi katika jicho la FINANCE ECONOMY ?

Qn2.
Business inategemea na control variables ili uwin market. So amid sanctions Russia alinusa kuanguka wa ruble alichofanya ni ku play na price ya petrol na gas. Unaposhusha price ya bidhaa una attract large market. Lowering commodity price psychologically triggers market flocking. Hii inapelekea bulk sells for fear that yanaweza kupanda bei. So majumuzi ni makubwa. Kutoka India na China, Africa.
Nakubaliana na wewe. Urusi akishirikiana na OPEC wameweza kutengeneza mazingira ambayo yamepeleka dunia kugawanyika katika pande mbili. Upande wa Magharibi wanauziwa nishati kwa gharama kubwa, jambo linalochangia mfumuko mkubwa wa bei (Energy Inflation). Hili linaathiri uzalishaji. Upande wa Mashariki wananunua nishati kwa bei ndogo mno, jambo ambalo linawapunguzia gharama za uzalishaji.

OPEC+ wamefanya makubaliano kupunguza uzalishaji wa gesi na mafuta, na maajabu yanaanza pale ambapo hadi nchi kama Saudi Arabia inanunua gesi na mafuta ya bei ndogo kutoka Urusi ili kufidia uhaba (To cover deficit). Hili linawafanya Saudi Arabia kupata utajiri mkubwa kutokona na bei ya gesi na mafuta kupanda.

Je, ni sahihi kusema mataifa yasiyo na rasilimali ni matajiri kwa kuangalia tu vitu kama masoko ya hisa, huduma na uzalishaji wa viwanda ?

Qn3.
Uchumi wa Russia utakua ngumu kuanguka labda kushuka hasa Unapokua na disposal ya natural resources (petrol, gas, metals, mbolea) you’re safe. Russia currently yuko scarce na technologies especially electronics chips. Hii itapelekea kukosa technology advancement kwenye mashine muhimu za uzalishaji hasa tractors, farm drones, ndege, magari, industries na automation kwa ujumla na itakua expensive kwelikweli maana soko lao kuu la electronics lilikua west .
Nakubaliana na wewe, hili litamgharimu sana Mrusi hasa kwenye uzalishaji na ukuaji wa viwanda. Akitaka kutumie teknolojia zake atatumia gharama kubwa sana na muda mrefu mpaka kuyafikia mataifa ya Magharibi. Japo naomba kuuliza, kama Urusi ataacha kabisa kununua teknolojia ya Magharibi unadhani hayo makampuni hayatakosa mabilioni ya fedha kutoka Urusi ?

Wataalamu wanasema kwamba mashirika mengi ya Magharibi yanapata faida sana Urusi. Mfano Nestle la Uswisi, peke yake walipata faida zaidi ya dola za Kimarekani Bilioni 1 kwenye soko la Urusi kwa mwaka 2022 peke yake. British Petroleum (BP) walikuwa wanamiliki zaidi ya asilimia 19.75% kwenye shirika la Rosneft wakivuna mabilioni ya faida. Metro la Ujerumani linahudumia wateja 2.5 nchini Urusi. Unadhani ikiendelea hivi makampuni ya Magharibi yanyewe pia hayatapoteza soko ?

Upande mwingine kuhusu Chips, Urusi na Ukraine ndiyo wanaoongoza kwa kuuza madini muhimu kama Palladium ambayo yanatumika katika uzalishaji nchini Marekani. Inasemekana asiliamia 35% ya Palladium ya Marekani inatoka Urusi. Hapa kuna kupata mbadala wa Urusi ndani ya usiku mmoja tu ?

Pia west wakiendelea na kutafuta alternative ya kupata nishati (gas au renewable) basi itakua shida kwa Russia maana competition ya market itakua hot. Especially US aki rump up production, Venezuela, canada, Norway, and other places
Nakubaliana na wewe, lakini kwa gharama ipi ? Mfano rahisi tu. Ulaya wananunua gesi kutoka Marekani kwa gharama kubwa mara mbili kuliko ile ya Urusi. Hapo inabidi uzingatia kwamba wananua LNG ambazo zinakuja na meli. Pia kuna gharama za bima ya majini (Maritime Insurance),na muda wa usafirishaji. Ukizingatia haya utafahamu siyo rahisi kama inavyosemwa.

Uchumi wa viwanda wa Ujerumani una thamani ya dola za Kimarekani Trilioni 1 na zaidi, lakini unaendeshwa na nishati ya Urusi yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 30 hadi 60. Hili ndilo linawafanya waweze kuzalisha na kuwa na nguvu ya viwanda (Cheap Energy). Sasa wakianza kununua gesi Venezuela, Marekani, Canada, Norway unadhani itakuwa gharama ndogo ?
 
Total value of Russian fossil fuel imports by countries since Russia-Ukraine war:

China 🇨🇳: $66.6 billion
Germany 🇩🇪: $26.1 b
Turkey🇹🇷: $25.9 b
India🇮🇳: $24.1 b
Netherlands🇳🇱: 18.0 b
Italy🇮🇹: $14.8 b
Poland🇵🇱: $12.1 b
France🇫🇷: $9.5 b
Belgium🇧🇪: $9.2 b
Hungary🇭🇺: $8.6 b
 
Back
Top Bottom