Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

Ha ha haa.
Mie Sina la kusema .
Ila Putin aliulizwa kwa Nini mlikimbia Kiev akajibu hatukukimbia Bali tuliondoka kuheshimu makubaliano ya amani yaliyokua yakisimamamiwa na Ututuki.
Putin akamuuliza mwandishi au unataka turudi?

Basi majibu yote yalikua hapo.

Hata hivyo hivi kweli mtu msomi na mwenye akili timamu unaweza kusema Ukraine anashinda vita?
Au Urusi anashindwa vita?
 
Umesema Money Stores Value kuliko rasilimali kama chakula. lla ukweli wa hii kauli kwenye vitendo ni upi ? Kwamba, fedha inaweza kukaa na thamani kupita rasilimali kama dhahabu, hebu tuelezane mwamba.
Nilivyoisoma hii sentensi kule kwake nikarudia tena, na tena halafu nikawazaa🤔

Ivi mwamba yupo siriazi. Pesa ni kitu tumekubaliana tu kiwakilishe thamani ilihali chenyewe kama chenyewe hakina hiyo thamani. Sasa kitu cha makubaliano ndo kiwe madhubuti kuliko vitu vyenyewe😳. Akat tunaweza kuamua kutokubaliana, kutoiamini na hapohapo inageuka nothing.

Kidogo niseme wachumi nao wanafundishwa ujinga. Ila afadhali we mchumi mwenzake umelipoint out. Ngoja ntasoma majibu yake.

Asante kwa mada na majibu, tunajifunza sana page by page, comment by comment. Inafariji hata tu kuona kuna watu wanaofikiria sense. Big up👊
 
Mbona Ulaya na Marekani wananunua bado rasilimali muhimu kutoka Urusi na kuendelea kuwekeza nchini humo, kama ambavyo Uchina na India wanafanya. AU haya ninyi wataalamu wetu hamyaoni jamani, ???

Takwimu za UN zinasema kwamba, Urusi na Ukraine kwa pamoja ndiyo wauzaji wakubwa wa mazao ya chakula. Wanaendelea kusema kwamba asilimia 44% ya nafaka kutoka bahari nyeusi imeenda kwa wateja ambao ni mataifa makubwa ya Ulaya na Asia (High Income Countries).

Juzi Urusi katijoa kwenye The Black Sea Grain Deal, na angalia nini kimetokea. Takwimu za masoko ya dunia zinasema baada ya Urusi kujitoa tu kwenye huo makakati hapo majuzi, bei ya nafaka imepanda kwa asilimia 3% nzima ambayo ni sawa na senti 689.25 kwa kibaba kimoja (689.25 Per Bushel). Hii inamaanisha bei ya chakula itapanda sana na kuchochea mfumuko wa bei (Food Price Inflation) kule Ulaya na sehemu nyingine duniani.

Hapa hata upandishe riba juu (Hiking Interest Rates) kiasi gani ili kupambana na mfumuko wa bei, huwezi kufanikiwa. Njia rahisi ya kudhibiti mfumuko wa bei itakuwa ni kutafuta rasilimali, na siyo zenye uhaba na kuziingiza kwenye soko. Fedha zitapoteza thamani na nguvu ya manunuzi itaisha.

Hili nimemwambia ndugu yangu zitto junior , ila yeye anaamini kwamba huu utajiri wa vitu visivyoonekana (Imaginary/ Incorporeal wealth) ndiyo njia sahihi ya kupata taswira halisi ya uchumi wa nchi. Binafsi hili linanipa ukakasi, kwasababu tokea karne za 17 tulitumia vyote, (Utajiri unaoonekana na Utajiri usioonekana) kupima taswira ya utajiri na uchumi wa nchi.

Sasa narudia maswali yangu, tena;

Mosi, imekuwaje taifa ambalo ni asilimia 4% ya Uchumi wa dunia isababishe mfumuko mkubwa wa bei ya chakula kwenye soko la dunia hadi kuathiri nchi tajiri za G7 ambazo zinamiliki asilimia 37.7% ya uchumi wa dunia, ???

Pili, Je dunia na wachumi walikuwa sahihi kuacha kuangalia utajiri wa nchi kwa kurunzi ya Finance Economy peke yake bila kuzingatia Commodity Economy, ???
Boy,


Kwa nin west wanafata kibubusa sera za us ambazo zinapelekea chumi zao kutetereka kinomanoma
 
Kweli kabisa Mkuu Mwana Taaluma.
Ni tofauti kubwa sana kujua mambo Kwa ukamulifu na kujua mambo Kwa ujanjaujanja.
Hii ndio inawakumba Baadhi ya Pro USA.anaulizwa swali anatoa maelezo meeeengi nje ya mada ili aonekane anajua mambo.
Sasa bahati sio Yao tena, Wanakula spana za hatari. Kila sekta wanakutana na kichwa kimoja hatari sana kina watuliza.


Yaani hii special operation wajamaa walijipanga haswa.
 
Kwanini tangu mwaka 2022 imapungua thamani ya mzunguko (Dollar's Circulation Volume) kutoka asilimia 75% hadi 55%, jambo ambalo mara ya mwisho kutokea ni mwaka 2001. Hapa namaanisha mpaka sasa, dola ya Marekani inatumika kwa asilimia 55% duniani kote. Nini chanzo cha hali hii kutokea, ??
Contradictory!! Umesema Dollar ya Marekani ilichapishwa nyingi kuliko mahitaji Cha ajabu unasema circulation volume imepungua?

If at all it was surplus to requirements how on earth is the volume staggering? In fact low volume or velocity of currency in circulation requires more pumping of dollars in the economy to stimulate multiplier effects.

Can you please clarify your contradicting statements?
 
Nikawauliza hivi ni sahihi kusema kwamba taifa ni dhaifu kiuchumi kwa kuzingatia tu, uchumi wa kifedha, Finance Economy. Bila kuzingatia uwezo wa nchi kwenye uchumi wa bidhaa, Commodity Economy, ???
Tulikujibu tunapima ubora wa kiuchumi kupitia GDP or GNP, GNI, HDI n.k ambazo Zina encompass both commodity, finance and service sectors.

Sielewi kwanini una assumption kwamba capital markets ni uchumi hewa? AZAM inauza real commodities ila ikitaka wawekezaji inaenda pale DAE ku trade meaning watu wananunua hisa za Real products Sasa kivipi Tena inakua uchumi hewa?
Mfano kampuni ya Apple pekee ni almost sawa na GDP ya Afrika nzima Sasa kampuni kama hiyo ikiwa Ina trade hisa zake kwenye stock markets kivipi inakua "finance economy" ilihali inauza actual commodities kama simu, tablets, technology, cloud storage n.k??

Why do you assume Finance markets ni uchumi hewa ilihali kampuni Zinazouza hisa zinauza real products?
 
Sasa bahati sio Yao tena, Wanakula spana za hatari. Kila sekta wanakutana na kichwa kimoja hatari sana kina watuliza.


Yaani hii special operation wajamaa walijipanga haswa.
Ha ha haa.
Na Siri kubwa ya wapiga spana wa upande wa wajamaa katika mada hizi za haya yanayotokea ulimwenguni Leo hii ni "ukweli na haki TU".
Daima ukisema ukweli na ukitetea haki unakua unahoja za msingi.
Lakini zaidi ukiseam kweli unakua huru.hawa wanaopingana na ukweli huishi kwa hoja za kubabaisha babaiaha TU.
Na haya ndio yanayowapata pro NATO wengi humu.
 
Ha ha haa.
Na Siri kubwa ya wapiga spana wa upande wa wajamaa katika mada hizi za haya yanayotokea ulimwenguni Leo hii ni "ukweli na haki TU".
Daima ukisema ukweli na ukitetea haki unakua unahoja za msingi.
Lakini zaidi ukiseam kweli unakua huru.hawa wanaopingana na ukweli huishi kwa hoja za kubabaisha babaiaha TU.
Na haya ndio yanayowapata pro NATO wengi humu.
Natamani Sana kwenye mada hii ya uchumi angeonzeka mchumi daraja lakwanza, mwenye data na fact kaka yangu Chige bila kumsahau kaka yangu Mchambuzi ili wengine tuendelee kujifunza namna uchumi na siasa za kimataifa zilivyo katka uhalisia. Pia nitoe shukran Kwa ndugu yangu zitto junior michango yake nimizuri Sana hongera Sana mkuu, bila kumsahau mchumi na mwanasheria wetu wa mjadala huu The Boy Wonder . Lakini pia natamani kuona michango ya Kichuguu ingawa nimtu ambae Huwa simkubali katika maoni yake katika siasa za ndani na zile za kimataifa..
 
Natamani Sana kwenye mada hii ya uchumi angeonzeka mchumi daraja lakwanza, mwenye data na fact kaka yangu Chige bila kumsahau kaka yangu Mchambuzi ili wengine tuendelee kujifunza namna uchumi na siasa za kimataifa zilivyo katka uhalisia. Pia nitoe shukran Kwa ndugu yangu zitto junior michango yake nimizuri Sana hongera Sana mkuu, bila kumsahau mchumi na mwanasheria wetu wa mjadala huu The Boy Wonder . Lakini pia natamani kuona michango ya Kichuguu ingawa nimtu ambae Huwa simkubali katika maoni yake katika siasa za ndani na zile za kimataifa..
Uchumi wa Urusi hauko Imara kama watu wengi wanavyoaminishwa. Putin alikuwa ametunza akiba kubwa sana akijiandaa na vikwazo baada ya vile vya mwa 2014. Kwa sasa hivi Urusi inatumia zaidi akiba hiyo kuliko income mpya. Pamoja na kwamba Urusi ina raslimali nyingi sana mabazo ndiyo uti wa mgongo wa nchi hiyo; hawana industrial goods zaidi ya silaha. Mauzo yao nchi za nje yamekuwa ni ya hasara sana. Kwa mfano mauzo ya mafuta India na China yanakwenda kwa bei ya karibu na bure; wanalazimika kuuza mafuta mengi sana kupata kiasi wanachohitaji. Faida yote inakwenda India na China kwani wao ndio wanaouza products za mafuta hayo nje kwa faida.
 
Contradictory!! Umesema Dollar ya Marekani ilichapishwa nyingi kuliko mahitaji Cha ajabu unasema circulation volume imepungua?

If at all it was surplus to requirements how on earth is the volume staggering? In fact low volume or velocity of currency in circulation requires more pumping of dollars in the economy to stimulate multiplier effects.

Can you please clarify your contradicting statements?
Mchumi na hili nalo nikuelekeze tena, ilhali ulitakuwa uwe unalifahamu, ???

Mosi, Marekani ilivyopandisha riba juu (Hiking Interest Rates) imepelekea doka kuimarika kitendo ambacho kimesababisha madhara makubwa kwa masoko yanayokuwa (Emerging Markets), kwasababu nchi nyingi zilipunguza thamani ya fedha zao hadi kwa asilimia 10% hadi 20% dhidi ya dola ya Marekani ili kuweza kumudu kuingiza (Imports) bidhaa kutoka soko la kimataifa.

Maana yake sasa, fedha za nchi zikipungua thamani, nchi inapata mfumuko wa bei, unaopelekea nchi kutumia fedha nyingi za kununua bidhaa muhimu kama mafuta na chakula. UNCTAD wametoa takwimu na zinaonyesha nchi zinazoendelea (Deloping Economies) zimekumbwa na DOUBLE-BURDEN (High Flood Prices Vs Strong Dollar).

Pili, Dollar Liquidity Swap Lines hazipo kwa kila nchi duniani, ndiyo maana uhaba wa dola umekuwa mkubwa. Siyo kila nchi inaweza kwenda kuchukua dola inavyotaka. Mpaka sasa, July 2023, mataifa ambayo yamepewa Unlimited Liquidity Swap Provisions na Marekani ni (Canada, United Kingdom, European Union, Japan and Switzerland).

Anafuatiwa (Australia, Brazil, South-Korea, Mexico, Singapore na Sweden) ambao Liquidity Swap Line yao ni dola za kimarekani Bilioni 60. Baada ya hapo kuna ( Dernmark, Norway, Newzeland) ambao Liquidity Swap Line yao ni dola za kimarekani Bilioni 30.

NB: Welcome to global economics my friend.....
 
USA na West hawajawahi tarajia uchumi wa Urusi uanguke. Lengo lao kwenye sanctions ni kuilazimisha Urusi iwe na options kwenye harakati zake za expansionism. Ijue wakati inaendelea kufanya uvamizi itaendelea kupoteza mazingira ya kiuchumi na hao wanaoweka vikwazo, isiwe na uhuru wa kuvamia ikijisikia.
Kama West na US zingetaka kuiua kiuchumi Urusi basi zingeanzia kwenye machine tools na precision machinery ambako Urusi haijiweziView attachment 2698026View attachment 2698027
Importation ya mitambo muhimu ya uzalishaji ingesitishwa yote na Urusi wangeishia kutegemea black market au kutegemea machine tools za China ambazo huwa haizipendelei.

Kwanza Marekani inahusika kwenye kuisaidia Soviet Union kukua kiviwanda mwanzoni mwa utawala wao, Volgograd tractor plant ilijengwa na Wamarekani pale Soviet Union iko busy kukua kwenye kilimo. Walikuja kupishana na Marekani walivyoanza kujitutumua na kujishindanisha na Marekani. Na technology transfer wakawa wanaitumia kutengeneza silaha, mfano hiyo Volgograd plant ilitengeneza vifaru, infantry fighting vehicles na artillery.
Sasa nchi gani itakubali ikupe teknolojia uunde silaha alafu uitunishie misuli, wakaachana nayo.
Hata China wanamfanyia hivi Warusi na Wamarekani, unamuuzia licence ya helicopter kutoka Sikosrky ya Marekani yeye anatumia kutengeneza attack helicopter. Sasa unaamua kumpa teknolojia chache zisizo na dual use na sometimes unagoma kumuuzia baadhi ya vitu asiige.

Marekani iliwahi kuwashawishi Germany na Japan baada ya WW2 kustaariba na kuishi kama waungwana duniani wakati kwenye vita walipigana. Leo hizo ni nchi za tatu ya nne kiuchumi duniani, South Korea waliopambaniwa na Marekani ni nchi inazidi Urusi kiuchumi. Hizo nchi tatu ni almost hazina kitu kwenye rasilimali wala ukubwa wa ardhi kama Urusi. Kama Urusi wangekuwa serious na vitu vya msingi hizo nchi tatu hazikutakiwa ziikaribie kiuchumi.

Una rasilimali za kutosha madini mengi kuanzia aluminium, gold, bauxite, iron ore, copper, diamond hadi rare earth metals, gesi ni wa kwanza duniani, mafuta ya kutosha mpaka unaitwa OPEC wakati sio mwanachama, unalima ngano, una mbao, una ardhi kubwa sana wakati idadi ya watu milioni 144 ukitaka kutenga eneo kubwa la kilimo unaweza, una uvuvi. Bado unazidiwa na Italy kwa GDP. Sasa wewe upewe nini hapa duniani?

Urusi sio kwamba hawaipendi, ni yenyewe inalazimisha kujipanbanisha na kuishi kama karne ya 20. Marekani haina haja ya kupambana na Urusi, na inachofanya ni kilekile tena pungufu ya ambacho superpower yeyote kwa timeline yoyote hapa duniani huwa anafanya.
Russia ana eneo kubwa Ila eneo kubwa la ardhi na bahari sio potential Kwa sababu ya Hali ya hewa.
 
Tulikujibu tunapima ubora wa kiuchumi kupitia GDP or GNP, GNI, HDI n.k ambazo Zina encompass both commodity, finance and service sectors.

Sielewi kwanini una assumption kwamba capital markets ni uchumi hewa? AZAM inauza real commodities ila ikitaka wawekezaji inaenda pale DAE ku trade meaning watu wananunua hisa za Real products Sasa kivipi Tena inakua uchumi hewa?
Mfano kampuni ya Apple pekee ni almost sawa na GDP ya Afrika nzima Sasa kampuni kama hiyo ikiwa Ina trade hisa zake kwenye stock markets kivipi inakua "finance economy" ilihali inauza actual commodities kama simu, tablets, technology, cloud storage n.k??

Why do you assume Finance markets ni uchumi hewa ilihali kampuni Zinazouza hisa zinauza real products?
Ndugu Zitto Jr, nadhani mimi na wewe tunapishana pahala padogo mno. Hebu twende sawa:

Mosi, napozungumzia Commodity Economy, nazungumzia uchumi ambao unaendeshwa na bidhaa ambazo zimeshikilia au zinatumika kwenye uzalishaji (Base Material). Kiuchumi, vitu kama dhahabu, nafaka, makaa ya mawe na madini mbalimbali, huitwa Commodities. Hizo Iphones, Gucci zinazouzwa, kiuchumi siyo (Commodities/Base Materials) bali huitwa, Finished Products. Wachumi huita otofati uliopo baina ya Base Material na Finished Products kama, Product Differentiation.

Ukienda kule World Trade Organisation (WTO) na kupitia baadhi ya mikataba yake, hasahasa ile ya miaka ya 90's haya yamewekwa wazi kabisa, kwamba ipi kisheria inachukuliwa kama Commodity na ipi inachukuliwa Finished Product. Ila pia hata kanuni za masoko yao ni tofauti. The Economics of Commodities is totally different from the economics of Finished Products. Ukisoma biashara ya kimataifa (International Trade and Commerce) na kupitia hii mikataba mikubwa kama GATT na GATS utaona utofauti wake ni mkubwa mno.

Pili, unaposema kwamba kampuni la Apple linatengeneza Iphone inauza Commodities, hii kibiashara na kisheria haiko sawa. An Iphone is not a commodity but a finished product. Wewe mchumi unatakiwa ulifahamu hili vizuri kabisa. Ukishafahamu hili, basi utatambua kwamba kibiashara, International Standards require that commities be produced in a uniform way worldwide. Masharti ambayo mkulima wa mchele wa Marekani amewekewa ili auze mchele kwenye soko la dunia, ndiyo hayohayo mkulima wa mchele wa Mbalali amewekewa ili auze mchele kwenye soko la dunia. Hili kitaalamu linaitwa, Fungibility.

Masharti ambayo, APPLE amewekewa ili atengeneze na auze bidhaa yake, ni tofauti kabisa na masharti ambayo XIAOMI amewekewa ili atengeneze na auze bidhaa yake. Finished Products zinatofautiana viwango kwasababu mbalimbali, muhimu ni kama gharama za tafiti (Research and Development), gharama za soko la ajira (The Cost of Labour Markets) na gharama za haki miliki (Intellectual Property Rights). Haya hufanya bei za Finished Products ziwe tofauti.

Huu mchakato mzima wa kutengeneza bidhaa, kuipa thamani na kuiuza kwenye soko la hisa, ndiyo Finance Economy yenyewe. Hata kwenye soko la huduma huwa hivihivi. Kinachotofautisha baina Finance Economy, ni kwamba wahusika wanaweza kucheza na bei za masoko kwa kufanya mambo kama: Overvaluation of Product and Speculation. Hili halipo kwenye Commodity Markets, because commodities are usually sold at their marginal cost of production.


Tatu, kwenye Commodity Markets mara nyingine huwepo na bei ya pamoja ya soko la kimataifa (Benchmark Price). Kubwa zaidi masoko yao ni maalumu, na hayauzi kwenye soko la hisa. Ukienda kwenye masoko ya makubwa ya vito vya thamani kama London Bullion Market Association (LBMA) utakuta bei ya dhahabu iko sawa na masoko mengine duniani kote. AU kama kibaba kimoja (Bushel) cha ngano ni senti 600, basi ndiyo huwa hivyo sehemu nyingi. AU kama mafuta (Brent Crude Price) ni dola 60% kwa pipa basi sehemu nyingi itakuwa hivyo.

Ila huku kwingine, Iphone huwa na bei yake na Xiaomi huwa na bei yake, japo zote mbili ni simu. Hili huathiri hadi thamani zao za hisa.

Nne, kiuchumi bei za Commodities haziwaathiri wanunuaji na wauzaji(Buyers and Sellers), bali hata watumiaji (Consumers). Bei ya mafuta au chakula zikipanda, tunaumia wote duniani. Hata wale wazalishaji wa simu kama APPLE huathirika. Ila bei za Iphone au Xiaomi zikipanda, nani anaathirika, ilhali hata Iphone sijawahi kumiliki mimi, ???

Tano, kisheria kampuni kama APPLE linavyouza hisa kuna au kampuni jingine ambalo limeamua kufanya Initial Public Offering (IPO) kuna mambo ambayo yanazingatiwa. Mengi kati ya hayo mambo hutokana na makadirio au makisio. Mfano, mabenki yanavyoyasaidia makampuni kupanga bei za hisa kuna kitu kiitwacho, HERD INSTINCT hutumika kama mbinu ya kupanga bei za hisa. Hapa kampuni hufanya makasio ya jinsi watu kama wewe Zitto Jr na wengine mnaopenda jina la APPLE mtashoboka na kukimbilia kununua hisa.

Mimi niliyesoma Intellectual Property & Entertainment navyosema Imaginary Wealth niko sahihi kabisa kisheria. Ukweli ni kwamba Intellectual Property Law protects and rewards expressed novel ideas that cannot be easily or uniformly quantified. Nikupe mfano rahisi tu, mradi wa ndege za Marekani wa F-35 Lock-Heed Martins umegharimu Marekani zaidi ya dola Trilioni 1 kwenye kufanya tafiti (Research & Development). Kasome mikataba kama TRIPS 1995, haya yako wazi kabisa mzee.

Ndege moja inaizwa hadi dola milioni 9, na Sheria (Intellectual Property Law) inamruhusu mtafiti kupanga bei yake kufidia gharama zake za tafiti. Hili jambo zima huathiri hata bei za hisa na thamani ya kampuni. Kisheria ni kwamba bidhaa (Finished Product), inapokuwa sokoni gharama yake hutokana haki ambazo ni za kifedha na zisizo za kifedha (Moral & Economic Rights of producers)

NB 1: Nashukuru umeuliza hili swali ili tuwekane sawa hasa kwenye suala zima la Finance Economy vs Commodity Economy, tukizingatia mambo muhimu kama International Trade and Commerce.

NB 2: Nakubaliana kabisa na wewe kwamba bidhaa (Products) lazima ziwe zina bei yake ambayo kiuchumi ni mihimu mno. Hili ni muhimu sana kiuchumi. Vipimo vya GDP, PPP, NG ni muhimu. Japo hivi vipimo mara nyingi huangalia uchumi peke yake kwa taswira ya jumla, bila kuangalia kwa ukaribu utendaji wa mambo kama biashara ya kimataifa (The Inner Workings of International Trade & Commerce) yanavyoathiri uchumi wa mataifa kiujumla hasa kwenye Finance Economy vs Commodity Economy.

NB 3: Niliweke na hili sawa ili usije ukazuka mjadala mwingine tena huko mbele, Not every natural resource is a commodity.

 
Ungeanza kunijibu maswali yangu mwanzo kabisa na kitaalamu kama anavyofanya bwana zitto junior ningetoa majawabu ya kila swali ulilouliza. Ila bahati mbaya hujafanya hivyo zaidi ya kuzunguka mbuyu na kuchanganya mambo. Nadhani mimi na wewe tuishie hapa, niendelea kufanya mjadala na Zitto Jr ambaye ni mchumi aliyesomea.
Sasa kumbe ulitaka mjadala ujibiwe na wanauchumi waliosomea. Si ungeweka dokezo tangu mwanzo badala ya kuchoshana.
Na kilichofanya uulize maswali na unajua sio mchumi niliyesomea ni nini, mpaka pale nilipotaka unijibu ndio ukajua mimi sio mchumi
 
Sasa kumbe ulitaka mjadala ujibiwe na wanauchumi waliosomea. Si ungeweka dokezo tangu mwanzo badala ya kuchoshana.
Na kilichofanya uulize maswali na unajua sio mchumi niliyesomea ni nini, mpaka pale nilipotaka unijibu ndio ukajua mimi sio mchumi
Kwanini wewe ulikimbilia kujibu swali la kiuchumi ilhali unafahamu wewe siyo mchumi, ???
Tatizo ni kimbelembele au ujuaji tu mazee ???
 
Siku zote uchumi unaotokana na mikopo ni uchumi hewa si himilivu hasa ukipata tatizo la kijamii au kiuchumi. Kwa mfano ukienda benki kukopa ni kweli UNAKUWA na fedha mfukoni lakini siku mwenye fedha akizihitaji na ukawa unazo pungufu ya alizozikukopesha au ukawa umeshindwa kulipa mkopo Kwa kadri ya makubaliano atatanga mali ulizo nazo ili ziuzwe kufidia fedha zake. Kama ulikuwa na nyumba au shamba litauzwa na utabaki masikini kuliko kabla hujakopa. Gdp ya mkopo si ya kuringia. Russia ameshinda hii vita ya kiuchumi Kwa sababu alikuwa na vitu muhimu ambavyo kama nchi mukivikosa vinaleta taharuki kubwa nchini kimaisha na kiuchumi.

1.CHAKULA
Urusi ni mzalishaji mkubwa wa chakula na anategemewa na dunia nzima , Kwa hiyo wananchi wake hawakuona kupanda kwa bei ya chakula ila kupungua Kwa bei baada ya soko la nje kusuasua.

2.Mafuta
Baada ya baadhi ya nchi kususa kununua mafuta yake aliyateremsha
bei Kwa soko la ndani na nchi marafiki Kwa hiyo wananchi kupata nafuu ya maisha, pia kupata masoko mapya Kwa nchi marafiki.

3.
Gesi
Baada ya ulaya kususa kununua gesi yake na hujuma kufanyika kwenye mfumo wa kupereka gesi ulaya ,alihimalisha soko la ndani Kwa kuweka unafuu wa bei.
Hivyo ndivyo vitu muhimu vinavyogusa wengi hivyo kufanya wananchi wa kawaida kutokuona mfumuko wa bei unaoathiri maisha yao.

4.
ZANA ZA KIJESHI.
Vita inakomba Hera nyingi hasa za nje kama unategemea kila ZANA uiagize nje ya nchi kama ilivyokuwa kwetu wakati wa vita ya Kagera. Mtihani huu Urusi kaushinda Kwa kuwa na akiba kubwa ya siraha na uzalishaji unafanyika ndani ya nchi, Kwa hiyo alichofanya ni kuongeza tu uzalishaji wa siraha.

Mambo hayo hapo juu ndiyo yalifanya uchumi wa Russia usitetereke huku waliomwekea vikwazo na wenye uchumi wa madeni wakipata mdororo wa uchumi. Unajidai kula kuku Kwa fedha ya mkopo ha ha ha ....!
Chakula, gesi, mafuta na zana za kijeshi sio vipimo vya uchumi. Hapo Urusi inajitosheleza kwa soko la ndani ila inahitaji pia kuuza nje na kununua nje, mambo inayofanya.
Uwezo wa kiuchumi na ukuaji wake una vipimo vyake. Wanauchumi wangetaja vitu kama GDP, PPP, investments, exports, imports, government expenditure, public consumption na kadhalika.
 
Kwanini wewe ulikimbilia kujibu swali la kiuchumi ilhali unafahamu wewe siyo mchumi, ???
Tatizo ni kimbelembele au ujuaji tu mazee ???
Umeanza kuniquote wewe, sikuanza kukujibu mimi. Na nimekuwa tagged kwenye uzi wako. Na hujaweka dokezo kwamba unastahili kujibiwa na wasomi wa uchumi.
 
Umeanza kuniquote wewe, sikuanza kukujibu mimi. Na nimekuwa tagged kwenye uzi wako. Na hujaweka dokezo kwamba unastahili kujibiwa na wasomi wa uchumi.
Ndugu Armata, mambo yako bayana kwenye kichwa cha habari na uzi mzima, kwamba maarifa ya uchumi yanahitajika kwenye huu uzi. Mbona wengine walielewa vizuri tu!
 
Nimezungumza na baadhi ya wachumi humu ndani. Nikawauliza hivi ni sahihi kusema kwamba taifa ni dhaifu kiuchumi kwa kuzingatia tu, uchumi wa kifedha, Finance Economy. Bila kuzingatia uwezo wa nchi kwenye uchumi wa bidhaa, Commodity Economy, ???

Maana uchumi wa Urusi ni mdogo mno kuliko hata ule wa Italia, ila sasa madhara ya kumtenga Urusi kiuchumi na kidiplomasia yamekuwa makubwa mno na kuumiza pande zote. Hata Marekani, EU na G7 walisema kwamba wangeweka vikwazo ambavyo vingeangusha uchumi wa Urusi ndani ya wiki chache. Je, walikosea kuangalia ukubwa na nguvu zao kwenye jicho la, Finance Economy, peke yake, ???

Kimweri
 
Back
Top Bottom