MALCOM LUMUMBA
JF-Expert Member
- Jul 26, 2012
- 21,113
- 65,124
- Thread starter
- #281
Nashukuru kwa maswali, kiongozi wa mjadala!
Nitajibu swali la kwanza kama ifuatavyo:
Hizo ripoti za IMF za hivi karibuni kuhusiana na uchumi wa Urusi zimezua mjadala mkubwa miongoni mwa wataalamu, wachumi bila kusahau wanahabari duniani. Media maarufu ikiwemo Reuters ilitoka na article yenye kichwa cha habari: The IMF's outlook on Russia is too rosy to be true. Ndio maana katika mchango wangu uliopita, nilizungumza kuhusu hali ya kuaminika kwa taarifa zilizopo kwa sababu nimeona hizi takwimu za IMF zikitumika humu kujengea hoja kwamba "vikwazo havifanyi kazi".
The IMF's outlook on Russia is too rosy to be true:
![]()
Breakingviews - The IMF’s outlook on Russia is too rosy to be true
The IMF recently estimated that Russia's economy will avoid a recession in 2023 and expand after a year of shrinking. This forecast looks too positive, columnist Pierre Briançon writes.www.reuters.com
Ili kujibu swali lako la kwanza, nitanukuu vyanzo mbalimbali ili kuonesha jinsi ambavyo takwimu hizo zimeleta shida na kuzua upinzani mkubwa katika uwanja wa uchumi.
Tafiti mbalimbali za kiuchumi zikiwemo ambazo nimezileta hapa katika post iliyopita zinapingana kwa kiasi kikubwa na utabiri wa IMF. Miongoni mwa wakosoaji wakubwa wa makisio ya uchumi yaliyotolewa na IMF kuhusu maendeleo ya uchumi wa Urusi ni Professor Jeffrey Sonnenfeld wa Yale University nchini Marekani.
Miongoni mwa maandiko yake kuhusu hilo, akishirikiana na wachumi wengine kama vile Stephen Samuel Roach, mhadhiri mkuu [Yale School of Management] ambaye pia aliwahi kufanya kazi Morgan Stanley kama chief economist, unaweza kulipata kwenye website ya gazeti la Fortune lenye kichwa cha habari: How the IMF naively parroted Putin's fake statistics–and botched its economic forecast for Russia.
Article hiyohiyo imechapishwa pia kwenye website ya Yale School of Management (Yale Insights) yenye title: With 'Zero Visibility' into the Russian Economy, the IMF is Parroting Putin's Line.
Links hizi hapa:
![]()
How the IMF naively parroted Putin’s fake statistics–and botched its economic forecast for Russia
The IMF simply does not have the data it needs to independently calculate Russia’s GDP by any accepted method.fortune.com
![]()
With ‘Zero Visibility’ into the Russian Economy, the IMF is Parroting Putin’s Line
Rather than admitting ignorance, write Yale’s Jeffrey Sonnenfeld, Stephen Roach, and Steven Tian, the IMF is accepting the Kremlin’s statistics—and fueling pessimism about the impact of sanctions.insights.som.yale.edu
Ili kurahisisha mambo, hivi hapa chini ni vipande vichache vya andiko hilo:
View attachment 2711451
Article imeendelea kwa kusema;
View attachment 2711453
Hoja kubwa ya Jeffrey Sonnenfeld na wenzake ni kuwa, kwa sasa IMF haina taarifa za kutosha kuhusiana na uchumi wa Urusi ili kuwawezesha wataalamu wake kukokotoa na kutoa makadirio yenye kuridhisha kitaalamu, huku kukiwa na ushahidi wa wazi kabisa wa wataalamu wa IMF sanjari na mashirika mengine kunyimwa taarifa muhimu za kiuchumi na serikali ya Urusi mara baada ya uvamizi wake.
Katika hiyo article, kuna mahali wameambatanisha link yenye nyaraka ambayo ndani yake kuna kauli kutoka IMF kwenda kwa Sonnenfeld na timu yake (Yale University) kuhusiana na takwimu zilizotolewa na shirika lao. Katika hiyo statement, IMF inakiri kuwepo kwa sintofahamu kubwa (massive uncertainty) kuhusiana na mustakabali wa uchumi wa urusi hali ambayo inapelekea kuwepo kwa utata mwingi kwenye issue ya kutoa makisio.
Nimechukua kipande (screenshot) cha hiyo statement kutoka katika hiyo nyaraka yenye takwimu na makisio ya uchumi wa Urusi. Inasema;
"We agree that there is massive uncertainty surrounding the future of the Russian economy, and hence doing a forecast could be seen as a "fool's errand"."
Wametumia msemo "fool's errand" wakikubali kwamba kitendo cha kufanya utabiri wa kiuchumi kuhusu Urusi katika mazingira ya sasa kinaweza kutafsiriwa kama kazi ya kijinga isiyo na tija. Statement hiyo vilevile inasapoti kile nilichokisema kuhusu Data Integrity na uhaba wa upatikanaji wa taarifa za kutosha.
Screenshot:
View attachment 2711449
Nyaraka nzima iko katika muundo wa PPTX:
![]()
IMF Russia Slide Deck.pptx | Powered by Box
yale.app.box.com
Mkosoaji mwingine ni huyu anayefahamika kama Agathe Demarais ambaye ni mchumi, pia ni mtaalamu wa vikwazo vya kiuchumi kutoka kitengo cha utafiti wa masuala ya kiuchumi duniani (Economist Intelligence Unit) chini ya The Economist Group [media company]. Moja ya maandiko yake utalipata kwenye website ya Foreign Policy lenye title ambayo iko straightforward: Don't Trust Russia's Numbers (Moscow has made economic statistics a central part of its information war). Yeye amejikita zaidi kuelezea nguzo kuu za kile anachokiita "Russia's disinformation" kuhusiana na mwenendo wa uchumi wake.
Link:
![]()
Don’t Trust Russia’s Numbers
Moscow has made economic statistics a central part of its information war.foreignpolicy.com
Demarais anasema kwamba;
The latest controversy surrounds the state of the Russian economy and what Western media and others have been reporting to their audiences. Read anything about the war in Ukraine these days, and you'll probably find a mention that the Russian economy contracted by about 2 percent in 2022—a low decline that suggests little more than a mild recession. That number has entered the policy debate: For some, the low figure is proof that the Russian economy is resilient and sanctions do not work. Others use the same figure to argue that sanctions are starting to bite and Western countries should double down. These opposing arguments have one thing in common: They rely on a largely meaningless number.
Ukiendelea kumsoma huyo mchumi, anataja sababu kadhaa zilizochangia kuonesha huo upungufu mdogo ulioripotiwa tofauti na ilivyotarajiwa baada ya uvamizi wa Urusi mwaka 2022.
Even if Russia's reported GDP decline were truthful, it is clear that three factors artificially boosted the Russian growth number in 2022. First, the economic growth figure has been fueled by Russia's turbocharged production of military gear. Producing tanks and missiles does not improve living standards, however, and this part of Russian GDP will quickly be destroyed on the battlefield. Second, Russia's export earnings jumped in 2022 because of the war-induced spike in energy prices. And third, Western embargos on technology and other goods as well as sinking Russian consumer demand led to a plunge in imports, which dropped by almost 10 percent during 2022, according to Russia's official data.
Mwisho wa kunukuu!
Kwa kifupi, hoja yake kubwa ni kuwa, Urusi imekuwa ikichezea takwimu za uchumi wake kama sehemu ya disinformation war dhidi ya nchi za magharibi ili kujibu ama kukabiliana na hoja au tuhuma kwamba uchumi wa Urusi umedorora kutokana na vikwazo. Hivyo, taarifa hafifu za kiuchumi zinazotolewa na Urusi hazikidhi vigezo au sifa za kuweza kuaminika kutoa makisio yanayoweza kukubalika kiuchumi.
Swali la pili:
Current account surplus, kwa lugha rahisi ni hali ya kiuchumi ambapo thamani ya bidhaa na huduma zinazozalishwa kupelekwa nje (exports) zinazidi thamani ya bidhaa na huduma zinazoingia nchini (imports).
Kwa kifupi kuhusiana na rekodi ya current account surplus ya Urusi mwaka 2022:
Kushuka kwa thamani ya imports kumechagizwa na uamuzi wa makampuni mengi ya nchi za magharibi kujiondoa na kuondoa biashara zao nchini Urusi kutokana na vikwazo. Kilichoongeza thamani ya exports ni mapato ya mafuta na gesi kutokana na kuongezeka kwa bei ya nishati kulikochochewa na vita inayoendelea. Hiyo ni kabla ya bidhaa hizo hususani mafuta kuwekewa vikwazo.
Tafuta takwimu za hivi karibuni; current account surplus imepungua kutokana na kushuka kwa mapato yatokanayo na mafuta na gesi. Again, narudia, Urusi imesitisha utoaji wa taarifa muhimu za kiuchumi, zikiwemo data zake za capital outflow mwaka huu.
Kuhusu swali la tatu:
Uchumi wa Urusi hauko kwenye soft landing bali ulishaingia kwenye recession kwa mujibu wa data zilizotolewa mara ya mwisho na Urusi yenyewe. Hakuna mjadala kuhusu uchumi wa Urusi kuwa kwenye recession ama kinyume chake kwa sababu kwa mujibu wa wachumi wa pande zote, Urusi iko kwenye recession. Mabishano yako kwenye kiwango cha recession ilichonacho Urusi.
Kwa mujibu wa takwimu rasmi za GDP za mwaka 2022 zilizotolewa na Urusi, uzalishaji ulianguka kwa asilimia takribani 4.1 na 4 katika robo mbili mfululizo (3&4) ukilinganisha na kipindi kama hicho mwaka mmoja uliopita. Maana yake ni kwamba Urusi ilikuwa kwenye technical recession katika vipindi hivyo viwili mwaka jana. Takwimu rasmi za robo ya nne hazikutolewa hadharani.
Mwaka huu, Urusi ilitoa ripoti ndogo kwamba uzalishaji ulianguka kwa asilimia 1.9 katika robo ya kwanza ya mwaka ukilinganisha na kipindi kama hicho mwaka 2022; ripoti ambayo bado inaonesha recession pamoja na kwamba wachumi kadhaa wamekataa kuziamini hizo taarifa. Hata ripoti mbalimbali za mashirika na taasisi nyinginezo [independent] zinasema kwamba uchumi wa Urusi bado uko kwenye contraction mwaka huu.
Asante!
Ndugu mhandisi,
Niseme tu, tangu nianze huu mjadala wewe umeonesha kwamba ni mtu makini sana. Unafuatilia mambo, unasoma kwelikweli na una uelewa wa haraka. Katika hili nakupa nyota zako kibao. Hivi ndivyo mijadala ya wasomi inatakiwa kuwa. Sasa naomba nirudi kwenye mada, na ntajikita kwenye suala muhimu sana la kiuchumi, hasahasa tunapozungumzia DATA INTEGRITY:
Umesema hatuwezi kupata taswira sahihi ya uchumi wa Urusi kwasababu serikali imeficha takwimu muhimu. Ukaleta na mifano ya kutosha ili kuwekea mashaka takwimu za shirika la fedha duniani (IMF) kuhusu uchumi wa Urusi kukua. Hivyo basi, kama hakuna takwimu sahihi na za kutosha, hatuwezi kuwa na taswira sahihi. Mimi hapa maswali yangu ni machache tu:
Mosi, wewe unasoma historia ya maendeleo ya dunia na uchumi wake tangu kipindi cha dola la Mrumi (The Roma Empire) hadi kufika leo hii. Katika kusoma kwetu, huwa tunapewa hadi takwimu za idadi ya watu na uchumi wa nchi za kale kama Rumi. Mfano, halisi wanahistoria kutoka CAMBRIDGE UNIVERSITY wanasema kwamba kipindi cha Kaisari Trajan (Emperor Trajan) dola la Rumi, lilikuwa ni asilimia 20% hadi 26% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Hizi takwimu za uchumi za miaka zaidi ya 2000 iliyopita wachumi na wanahistoria wanazitoa wapi, ilhali Warumi wenyewe hawakuwapa, ???
Je, tutakuwa sahihi kusema kwamba takwimu hizi zina walakini (The Lack Integrity) kwasababu Warumi wenyewe hawakutupa, na mambo mengi ya uchumi wa Rumi hatuyafahamu. AU kwasababu wanahistoria hawakuishi kipindi hicho, ???
Mnamo Karne ya 19 wakati Uingereza inaenda kuanzisha utawala nchini India (The British Raj), wachumi wanasema India ilikuwa na uchumi asilimia 24% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Huku Uchina ikiwa na asilimia 34% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Hizi takwimu wahindi wala wachina hawakuzitoa, ila wanahostoria wameweza kutambua. Hapa napo tutakuwa sahihi, kusema tusizitegemee takwimu ambazo hatukuwahi kupewa na serikali ya nchi hizi mbili, ???
Pili, wachumi huweza hadi kutabiri uchumi wa miaka 50 ijayo ilhali wao wako leo. Mfano, hai The Peter G. Peterson Foundation, hivi karibuni wametoa takwimu za deni la Marekani kwa mwaka 2053, na kusema kwamba Marekani itakuwa inalipa asilimia 40% ya bajeti yake katika kulipa deni. Maana yake katika kila dola 10, Marekani atakuwa analipa dola 4 kwenye madeni. Hawa wametumia mbinu gani (Model)za kiuchumi katika kuweza kutabiri hivi, ilhali hata mwaka 2030 bado hatujafika, ???
Tatu, kama unasema tusiwaamini IMF kwasababu Urusi hawajatoa takwimu zotem basi utakuwa umesahau kilichotokea miaka miwili iliyopita. Duniani yote na taasisi kubwa zilikumbwa na uhaba wa takwimu sahihi za kiuchumi kutokana na nchi kufungwa na shughuli za kiuchumi kusimamishwa (Lockdowns). Nchi kama Uchina na Marekani hazikuweza kutoa baadhi ya takwimu muhimu kwasababu raia hawakuwepo katika maeneo yao ya kiuchumi. THE HARVARD BUSINESS REVIEW, kwenye makala yao ya tarehe 10 November 2020, iliyoandikwa na Demitry Estrin walilizungumzia hili.
Mbali na hizi changamoto zote za uhaba wa takwimu, taasisi kama IMF waliweza kutoa takwimu zao zilizotoa taswira sahihi kabisa za uchumi wa mataifa mbalimbali duniani. Kwenye hoja hii, maswali yangu ni haya yafuatayo:
A. Kama IMF waliweza kutoa taswira sahihi za uchumi wa nchi mbalimbali kipindi cha (Lockdown), na tukaziamini hata pale ambapo mataifa mengi yalishindwa kutoa takwimu, kwanini tushindwe kuziamini hizi takwimu zao za kipindi hiki, ???
B. Mbali na uhaba wa takwimu, taaisi za kiuchumi kama The International Monetary Fund (IMF), The World Bank (WB), The Economist Intelligence Unit, walitoa takwimu sahihi sana ambazo zilielezea kwamba dunia itaingia kwenye kipindi cha mdororo wa kiuchumi wa kimkakati (Technical Recession) kuanzia mwaka 2021, na kweli yalitokea na tukayashuhudia. Walitumia mbinu gani za kiuchumi kuweza kufanya utabiri kwa usahihi, ???
Nne na wisho, ndugu mhandishi, taasisi za kifedha kama The International Monetary Fund (IMF) na World Bank (WB) huwa zinategemea chanzo kimoja tu cha takwimu, ambacho ni takwimu kutoka kwa nchi. IMF katika kutoa taarifa zao, huwa na vyanzo mbalimbali (Primary Data Sources, Secondary Data Sources). Taarifa zote za kiuchumi huwa zinaeleza kuwa wametumia vyanzo gani vya taarifa na mbinu za zipi za kiuchumi ili kutoa taswira ya uchumi.
Mbali na nchi kuwa ndiyo chanzo kikubwa, taasisi kama World Trade Organization (WTO) na mashirika mengine ya kimataifa yanayohusika na biashara hutoa takwimu muhimu mno, hata kama nchi itajaribu kuficha. Taifa lolote lile ambalo linategemea biashara za kimataifa (International Trade) kama chanzo cha mapato, haliwezi kabisa kuficha taarifa zake zote muhimu. Hebu nieleweshe hapa ndugu yangu, kama Urusi wameficha takwimu, taasisi za kiuchumi zitashindwa hata kufanya makadirio ya uchumi (Economic Estimation) kwa kutumia mbinu mbalimbali, ???
Hebu nisaidie kuelewa ndugu yangu.....
Niseme tu, tangu nianze huu mjadala wewe umeonesha kwamba ni mtu makini sana. Unafuatilia mambo, unasoma kwelikweli na una uelewa wa haraka. Katika hili nakupa nyota zako kibao. Hivi ndivyo mijadala ya wasomi inatakiwa kuwa. Sasa naomba nirudi kwenye mada, na ntajikita kwenye suala muhimu sana la kiuchumi, hasahasa tunapozungumzia DATA INTEGRITY:
Umesema hatuwezi kupata taswira sahihi ya uchumi wa Urusi kwasababu serikali imeficha takwimu muhimu. Ukaleta na mifano ya kutosha ili kuwekea mashaka takwimu za shirika la fedha duniani (IMF) kuhusu uchumi wa Urusi kukua. Hivyo basi, kama hakuna takwimu sahihi na za kutosha, hatuwezi kuwa na taswira sahihi. Mimi hapa maswali yangu ni machache tu:
Mosi, wewe unasoma historia ya maendeleo ya dunia na uchumi wake tangu kipindi cha dola la Mrumi (The Roma Empire) hadi kufika leo hii. Katika kusoma kwetu, huwa tunapewa hadi takwimu za idadi ya watu na uchumi wa nchi za kale kama Rumi. Mfano, halisi wanahistoria kutoka CAMBRIDGE UNIVERSITY wanasema kwamba kipindi cha Kaisari Trajan (Emperor Trajan) dola la Rumi, lilikuwa ni asilimia 20% hadi 26% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Hizi takwimu za uchumi za miaka zaidi ya 2000 iliyopita wachumi na wanahistoria wanazitoa wapi, ilhali Warumi wenyewe hawakuwapa, ???
Je, tutakuwa sahihi kusema kwamba takwimu hizi zina walakini (The Lack Integrity) kwasababu Warumi wenyewe hawakutupa, na mambo mengi ya uchumi wa Rumi hatuyafahamu. AU kwasababu wanahistoria hawakuishi kipindi hicho, ???
Mnamo Karne ya 19 wakati Uingereza inaenda kuanzisha utawala nchini India (The British Raj), wachumi wanasema India ilikuwa na uchumi asilimia 24% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Huku Uchina ikiwa na asilimia 34% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Hizi takwimu wahindi wala wachina hawakuzitoa, ila wanahostoria wameweza kutambua. Hapa napo tutakuwa sahihi, kusema tusizitegemee takwimu ambazo hatukuwahi kupewa na serikali ya nchi hizi mbili, ???
Pili, wachumi huweza hadi kutabiri uchumi wa miaka 50 ijayo ilhali wao wako leo. Mfano, hai The Peter G. Peterson Foundation, hivi karibuni wametoa takwimu za deni la Marekani kwa mwaka 2053, na kusema kwamba Marekani itakuwa inalipa asilimia 40% ya bajeti yake katika kulipa deni. Maana yake katika kila dola 10, Marekani atakuwa analipa dola 4 kwenye madeni. Hawa wametumia mbinu gani (Model)za kiuchumi katika kuweza kutabiri hivi, ilhali hata mwaka 2030 bado hatujafika, ???
Tatu, kama unasema tusiwaamini IMF kwasababu Urusi hawajatoa takwimu zotem basi utakuwa umesahau kilichotokea miaka miwili iliyopita. Duniani yote na taasisi kubwa zilikumbwa na uhaba wa takwimu sahihi za kiuchumi kutokana na nchi kufungwa na shughuli za kiuchumi kusimamishwa (Lockdowns). Nchi kama Uchina na Marekani hazikuweza kutoa baadhi ya takwimu muhimu kwasababu raia hawakuwepo katika maeneo yao ya kiuchumi. THE HARVARD BUSINESS REVIEW, kwenye makala yao ya tarehe 10 November 2020, iliyoandikwa na Demitry Estrin walilizungumzia hili.
Mbali na hizi changamoto zote za uhaba wa takwimu, taasisi kama IMF waliweza kutoa takwimu zao zilizotoa taswira sahihi kabisa za uchumi wa mataifa mbalimbali duniani. Kwenye hoja hii, maswali yangu ni haya yafuatayo:
A. Kama IMF waliweza kutoa taswira sahihi za uchumi wa nchi mbalimbali kipindi cha (Lockdown), na tukaziamini hata pale ambapo mataifa mengi yalishindwa kutoa takwimu, kwanini tushindwe kuziamini hizi takwimu zao za kipindi hiki, ???
B. Mbali na uhaba wa takwimu, taaisi za kiuchumi kama The International Monetary Fund (IMF), The World Bank (WB), The Economist Intelligence Unit, walitoa takwimu sahihi sana ambazo zilielezea kwamba dunia itaingia kwenye kipindi cha mdororo wa kiuchumi wa kimkakati (Technical Recession) kuanzia mwaka 2021, na kweli yalitokea na tukayashuhudia. Walitumia mbinu gani za kiuchumi kuweza kufanya utabiri kwa usahihi, ???
Nne na wisho, ndugu mhandishi, taasisi za kifedha kama The International Monetary Fund (IMF) na World Bank (WB) huwa zinategemea chanzo kimoja tu cha takwimu, ambacho ni takwimu kutoka kwa nchi. IMF katika kutoa taarifa zao, huwa na vyanzo mbalimbali (Primary Data Sources, Secondary Data Sources). Taarifa zote za kiuchumi huwa zinaeleza kuwa wametumia vyanzo gani vya taarifa na mbinu za zipi za kiuchumi ili kutoa taswira ya uchumi.
Mbali na nchi kuwa ndiyo chanzo kikubwa, taasisi kama World Trade Organization (WTO) na mashirika mengine ya kimataifa yanayohusika na biashara hutoa takwimu muhimu mno, hata kama nchi itajaribu kuficha. Taifa lolote lile ambalo linategemea biashara za kimataifa (International Trade) kama chanzo cha mapato, haliwezi kabisa kuficha taarifa zake zote muhimu. Hebu nieleweshe hapa ndugu yangu, kama Urusi wameficha takwimu, taasisi za kiuchumi zitashindwa hata kufanya makadirio ya uchumi (Economic Estimation) kwa kutumia mbinu mbalimbali, ???
Hebu nisaidie kuelewa ndugu yangu.....