Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?


....hebu tuonyeshe ni wapi JK alilenga Wanyarwanda........hivi ulisikiliza hotuba yake kweli wewe?.........au unataka kutuambia kuwa sherehe za Mashujaa tulizipanga baada ya uhasama wa JK na PK kuwa zifanyikie Kagera?.........au kilio cha wananchi wa mikoa ya kanda ya maziwa makuu nacho kilipangwa......na kiliwalenga Wanyarwanda..........
 
Someone's emotions are not acting at the benefit of intellect
 
adolay,

..hivi kwani wahamiaji haramu huko Kagera ni wa-Nyarwanda peke yao?

..hakuna wahamiaji haramu toka Uganda, na Burundi?

..je, hizo habari toka independent sources kwamba ni wahamiaji haramu toka Rwanda peke yao ndiyo wanaoshughulikiwa?

..Mimi naendelea kusisitiza kwamba zoezi linaloendelea mkoani Kagera, lifanyike maeneo mengine ya mpakani, na hata mijini.
 
Last edited by a moderator:

......hivi wewe ni mfuatiliaji wa issue zinazotokea sehemu zilizo na zinazo athirika na wahamiaji haramu........the point is....at one point and time this hd to happen......
 
Hivi Mwanakijiji alivyofanya uchochezi wa kumtaka Kadinali pengo aitishe vita vya kidini sio njama ya uuaji?

Mwanakijiji inabidi ajue kuwa haya maandishi yake ya kichochezi siku kikilipuka atajumuishwa the Hegue kama yule mtangazaji wa Kenya...
Tuwekee hilo bandiko la kumtaka pengo kuanzisha vita vya kidini, failure to that itathibitisha kuwa wewe ni muongo na mzushi tu unaechumia tumbo kupotosha jamii.
 

Nikijaribu kuvuta kumbukumbu yangu vizuri kikwete alianzia kigoma kama sijakosea.

a) Hakuanza na kauli hii kwanini aliihifadhi hadi alipofika kwa wanyarwanda huko Kagera

b) Lakini kubwa zaidi ni pale ambapo amekuwa madarakani kwa miaka kama saba sasa haya matatizo hakuyaona? ( hoja

yangu hapa ni kupinga siasa chafu za visasi za kikwete) Kiwete Vs Kagame matokeo wasio husika wanataabika.

c) Kuna wale askari/wapinzani wa kabira DRC waliouwa wanajeshi wetu na kuzamisha chombo chetu ziwa tanganyika na mara kwa mara wakongomani hufanya hivyo. Mbona kikwete alikaa kimya? (Narejerea sio kwamba kikwete anasimamia sheria za uhamiaji bali anazitumia kwa maslahi yake kulipa visasi.
 
Nina umri mkubwa kumzidi mama yako mzazi, vipi niwe kamanda wa Bavicha?
ha haa ha ha, kamanda lete matusi mapya bana wewe ndiyo tegemeo la bavicha kwa matusi, tunasubiri.
 
......hivi wewe ni mfuatiliaji wa issue zinazotokea sehemu zilizo na zinazo athirika na wahamiaji haramu........the point is....at one point and time this hd to happen......
Utathibisha vipi kwamba hilo halijatokea kwa sababu ya ugomvi wake na Kagame?
 
......hivi wewe ni mfuatiliaji wa issue zinazotokea sehemu zilizo na zinazo athirika na wahamiaji haramu........the point is....at one point and time this hd to happen......

Why this had to wait political friction btn kagame and kikwete?
 
Hivi Mwanakijiji alivyofanya uchochezi wa kumtaka Kadinali pengo aitishe vita vya kidini sio njama ya uuaji?

we nawe na ubongo wako uliojifungafunga kama uyoga pori sijui tukusaidie vipi; kuna chuki kama utawala mbovu, wenye upendeleo, na wa kifisadi? Hata Hitler alikuwa na watu wanampenda, Idi Amin alikuwa na watu wanampenda, Sadam, Lenin, Milosevic, Mobutu n.k. Na wapo waliokuwa wanawapenda watu hao kwa sababu walikuwa wananufaika moja kwa moja na utawala huo na hivyo wakaamua kufumbia upofu vitendo ambavyo watawala walikuwa wanavifanya au wanaacha vifanywe!!
 
Tuwekee hilo bandiko la kumtaka pengo kuanzisha vita vya kidini, failure to that itathibitisha kuwa wewe ni muongo na mzushi tu unaechumia tumbo kupotosha jamii.

Hawezi hata kwa kutunga tu hawezi kulipata... ni katika hofu tu ya kuwa hatuwaachi watawale wapendavyo na kuwalisha watu sumu ya uzalendo wa uongo!
 


Swala la usalama wa nchi yetu na watu wetu lina manufaa kwa watu wote wenye nia njema na nchi yetu. Wewe si mmoja wao...
 
Tuwekee hilo bandiko la kumtaka pengo kuanzisha vita vya kidini, failure to that itathibitisha kuwa wewe ni muongo na mzushi tu unaechumia tumbo kupotosha jamii.

Kumbe hujui Mwanakijiji alifanya uchochezi gani baada ya tragic news za kutoka Zanzibar!!!

Mwambie yeye mwenyewe akutumie. Kumbe wewe humjui vizuri Mwanakijiji, basi ni bora ujiweke naye mbali kumtetea huyu mtu hatari kunaweza kukutia kwenye matatizo usiyoyatarajia...
 

Mkuu nakubaliana na hoja yako hususani mstari huo wa mwisho, lakini katika hili kuna mambo mengi yanaibuka siku za hivi

karibu kuhusiana na ushirikiano wetu EAC kwanini nchi za Rwanda, Kenya na uganda wanatutenga? nadhani wanyasa nao

nikama hao niliowataja tupanue wigo zaid wa mjadala huu kwa ruhusa yako.
 
I remember the story ya yule kanali wa jeshi letu kumbe ni mhamiaji haramu, hadi leo kapotezwa... familia yake inapata shida balaa....... majaoga
 
Swala la usalama wa nchi yetu na watu wetu lina manufaa kwa watu wote wenye nia njema na nchi yetu. Wewe si mmoja wao...
Kwa upeo wenu wa kijuha, mtu anaewakosoa mnamuona adui yenu?, mnataka ma "yes man" hata mnapofanya vitu vya kipuuzi?
Tayari ushambagua Mwanakijiji kwamba sio mmoja wao!!, ndio , sio mmoja wao hao wapuuzi wanaoshindwa kusema ukwrli kwa sababu wananufaika na mfumo mbovu na uongozi dhaifu, au wengine kwa sababu ya uoga tu wameamua kufunga midomo, but not him.
Hakuna mtu anayepinga hatua za kuhakikisha usalama wa nchi, tunachohoji ni hatua ya kumalizia hasira kwa wananchi wasiohusika na ugomvi wa JK na Kagame. Watanzania wapo kila sehemu ya dunia, Je, utafurahi wakifurushwa bila utaratibu?
 
ha haa ha ha, kamanda lete matusi mapya bana wewe ndiyo tegemeo la bavicha kwa matusi, tunasubiri.
Lete habari, hujasikia fununu kuwa DPPccm anampango wa kukata rufaa dhidi ya hukumu ya mahakama kuu kanda ya Tabora?
 

na mfano mzuri tunao kwa ndugu zetu wa kongo, waliwakaribisha kama majirani wema sasa wanaonekana kama kuku wa kienyeji kwa wema wao. watusi ni watu wachafu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…